Apr 20, 2024 02:57
Balozi wa Afrika Kusini mjini Doha, Ghulam Hussein Asmal, amesema nchi yake ilifungua kesi ya kuitetea Palestina mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki dhidi ya utawala vamizi wa Israel unaoendelea kuua watu wa Ukanda wa Gaza tangu tarehe saba mwezi Oktoba mwaka jana kwa dhamira ya kutenda haki, akisisitiza kuwa hakuna sababu ya kuachana na kadhia hiyo.