Mar 22, 2024 07:04
Katika hotuba yake ya siku ya kwanza ya mwaka mpya wa 1403 Hijria Shamsia, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Ali Khamenei, amesema suala la Palestina na Gaza ni suala la daraja ya kwanza la kimataifa na kusisitiza kuwa: Kadhia ya Gaza imeonesha jinsi ulimwengu eti uliostaarabika na unaodai kutetea haki za binadamu, unavyofanya dhulma kubwa dhidi ya watu wa Gaza.