Jan 04, 2021 11:03
Januari 3 mwaka uliomalizika hivi majuzi wa 2020, kwa amri ya Rais Donald Trump, utawala wa kigaidi wa Marekani ulifanya jinai ya kumuua kigaidi Luteni Jenerali Qassim Suleimani, Mkuu wa Kikosi cha Quds, cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (SEPAH) na Abu Mahdi al Muhandis, Naibu wa Mkuu wa Harakati ya al Hashd al-Shaabi katika shambulio la anga lililofanywa jirani na uwanja wa ndege wa Baghdad nchini Iraq.