Mar 26, 2024 02:09
Marekani, ikiwa ni mshirika muhimu zaidi na muungaji mkono asiye na masharti wa utawala wa Kizayuni wa Israel, inatekeleza sera ya undumakuwili kuhusu utawala huo na jinai zake. Kwa upande mmoja, katika kitendo cha kuonyesha mshikamano na Israel, Washington imetangaza msaada mpya wa kijeshi kwa utawala huo sambamba na kukata misaada kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Wapalestina UNRWA.