Nov 26, 2021 02:47
Fernand de Varennes, ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya haki za binadamu za jamii za wachache, ametahadharisha juu ya kuzidi kupanuka ufa wa kukosekana usawa na uenezaji chuki dhidi ya jamii za wachache katika mfumo wa vyombo vya mahakama na vyombo vya habari vya Marekani na kutilia mkazo udharura wa kuanzishwa sheria ya kimataifa ya kukabiliana na uenezaji chuki.