Oct 24, 2023 13:53
Maelfu kwa maelfu ya watu wamejitokeza mabarabarani katika mji mkuu wa Ufaransa, Paris kushiriki maandamano ya kulaani jinai zinazoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wananchi wa Palestina, huku idadi ya Wapalestina waliouawa shahidi hadi sasa ikipindukia 5,000.