Mar 28, 2024 10:08
Ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira UNEP imesema, wakati theluthi moja ya watu duniani wanakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula, milo bilioni moja, ambayo ni sawa na moja ya tano ya chakula chote hutupwa kila siku na kuishia jalalani.