Bab al-Mandab, mstari mpya wa kuzuia hujuma na kuimarisha uwiano wa

Bab al-Mandab, mstari mpya wa kuzuia hujuma na kuimarisha uwiano wa "Umoja wa Medani"

Msemaji wa Jeshi la Yemen ametangaza kwamba kuanzia sasa jeshi hilo limeanza kutekeleza amri ya kupiga marufuku kikamilifu meli zote za utawala haramu wa Israel kupita katika maji ya Bahari ya Shamu au kwa Kiingereza Red Sea na kwamba kuanzia wakati wa kutangazwa marufuku hiyo na kuendelea urambazaji wa baharini wa Israel katika Bahari Nyekundu utakuwa shabaha halali ya jeshi la wanajeshi wa Yemen.

Jibu kali la makombora la Iran kwa ukiukaji wa mara kwa mara wa usitishaji vita na jinai za Israel nchini Lebanon

Jibu kali la makombora la Iran kwa ukiukaji wa mara kwa mara wa usitishaji vita na jinai za Israel nchini Lebanon

Iikiwa ni katika kunufaika na haki yake ya kujilinda na kujibu ukiukaji wa mara kwa mara wa usitishaji vita na jinai za kinyama zinazofanywa na utawala dhalimu wa Israel dhidi ya watu wa Lebanon, vikosi vya jeshi la Iran Jumapili usiku vilitoa jibu kali la makombora katika maeneo ya utawala huo katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu. Maeneo yaliyolengwa katika shambulio hilo kubwa la makombora kimsingi ni ya kijeshi na kistratijia ya utawala wa Israel.

Kwa nini washirika wa Washington sasa wana wasiwasi kuhusu uwepo wa kambi za Marekani katika ardhi zao?

Kwa nini washirika wa Washington sasa wana wasiwasi kuhusu uwepo wa kambi za Marekani katika ardhi zao?

Kwa mujibu wa jarida la Foreign Affairs la nchini Marekani, vita na Iran vinaweza kutoa changamoto kubwa kwa jeshi la Marekani na hasa kuhusu hatari ya kushambuliwa kambi zake za kijeshi katika siku zijazo.

Kwa nini Ulaya inataka kufafanua upya uhusiano wake na China?

Kwa nini Ulaya inataka kufafanua upya uhusiano wake na China?

Ufaransa na nchi nyingine nne za Ulaya, katika mkesha wa mkutano wa kimkakati wa Kamisheni ya Ulaya kuhusu China, zilitoa wito wa kuundwa vyombo vipya vya kutetea biashara ili kulinda viwanda vya Ulaya na kukabiliana na ushindani kutoka kwa makampuni yanayoungwa mkono na serikali ya Beijing.

Israel na Somaliland: Njama ya kudhibiti Bab al Mandeb

Israel na Somaliland: Njama ya kudhibiti Bab al Mandeb

Tarehe 26 Desemba, 2025, Israel ililitambua eneo lililotangaza kujitenga na Somalia la Somaliland kama taifa huru; licha ya kwamba, katika upeo wa kimataifa, eneo hilo inaendelea kutambuliwa kuwa sehemu ya Somalia.

Kwa nini Somaliland imeipa ofa Marekani ya kuanzisha kituo cha kijeshi katika ardhi yake?

Kwa nini Somaliland imeipa ofa Marekani ya kuanzisha kituo cha kijeshi katika ardhi yake?

Somaliland imeipa Marekani ofa na fursa ya kuanzisha kambi ya kijeshi katika ardhi yake. Vyanzo vya habari vimeripoti kwamba, maafisa wa Somaliland wameipa Washington ofa ya kutumia rasilimali za madini za eneo hilo na kuanzisha kambi ya kijeshi.

Machungu ya Ukoloni | Eritrea: Chini ya kivuli cha apathaidi ya Italia, simulizi ya udhalilishaji na mapambano

Machungu ya Ukoloni | Eritrea: Chini ya kivuli cha apathaidi ya Italia, simulizi ya udhalilishaji na mapambano

Ukandamizaji wa kikoloni wa Italia nchini Eritrea haukuwa tu mradi wa upanuzi wa ushawishi wa kisiasa, bali ulikuwa mfumo uliosimikwa juu ya uvamizi wa kijeshi, ubaguzi wa rangi au apathaidi, ukandamizaji wa upinzani, na utumwa. Mfumo huu wa kikoloni ulifikia kilele mwaka 1938, katikati ya jiji la Roma, hatua ya malalmiko iliyochukuliwa na Zerai Deres ilipofichua wazi unafiki na ukatili wa utawala huo.

Machungu ya ukoloni: Pamba, moto, na njaa; faili la umwagaji damu la Ujerumani Afrika Mashariki

Machungu ya ukoloni: Pamba, moto, na njaa; faili la umwagaji damu la Ujerumani Afrika Mashariki

Ukoloni katika karne ya 19 na 20 haukuwa tu ukihusiana na kueneza bendera katika ramani ya dunia; bali ulikuwa mradi uliopangwa wa kutwaa ardhi, rasilimali, na nguvukazi ambao ulibadilisha miundo ya kiuchumi na kijamii ya watu waliokuwa chini ya ukoloni.