Marasimu ya Kimataifa ya "Watoto Wanaonyonya wa Hussein" yafanyika katika nchi zaidi ya 40
https://parstoday.ir/sw/news/iran-i55833
Marasimu ya Kimataifa kwa jina la "Watoto Wachanga Wanaonyonya wa Hussein a.s" yamefanyika leo Ijumaa katika zaidi ya maeneo elfu sita katika Iran ya Kiislamu na katika nchi 45 duniani sambamba na Ijumaa ya kwanza ya mwezi wa Muharram.
(last modified 2025-06-15T08:05:10+00:00 )
Sep 06, 2019 08:13 UTC
  • Marasimu ya Kimataifa ya

Marasimu ya Kimataifa kwa jina la "Watoto Wachanga Wanaonyonya wa Hussein a.s" yamefanyika leo Ijumaa katika zaidi ya maeneo elfu sita katika Iran ya Kiislamu na katika nchi 45 duniani sambamba na Ijumaa ya kwanza ya mwezi wa Muharram.

Marasimu hayo ya Kimataifa ya Watoto Wachanga wanaonyonya wa Hussein a.s ni mjumuiko wa kidini unaofanywa na Waislamu duniani ikiwemo hapa Iran, India, Pakistan, Iraq, Saudia, Uturuki na Afghanistan katika Ijumaa ya kwanza ya mwezi wa Muharram katika kuwakumbuka watoto waliouliwa shahidi katika Siku ya Ashura.

Katika marasimu haya, akina mama huwavalisha watoto wao wanaonyonya maziwa mavazi yenye kufanana na kisha huwafunga vipande vya vitambaa kichwani vilivyoandikwa jina tukufu la Ali Asghar a.s.; na hivyo kudhihirisha mapenzi na kujitolea kwao kwa familia  hiyo tukufu na adilifu. 

Kichanga kikiwa kimebebwa na kufungwa kitambaa usoni chenye jina la Ali asghari .a.s

 

Mtukufu Ali Asghari a.s alikuwa mtoto mdogo zaidi wa Imam Hussein a.s; Imamu wa tatu wa Waislamu wa Kishia ambaye aliuliwa shahidi tarehe Sita Muharram mwaka 61 Hijria huko Karbala  akiwa na umri wa miezi sita.