Kinyume na uongo wa Netanyahu, UN yasema: Israel imezuia 90% ya misaada ya kuingizwa Ghaza
Umoja wa Mataifa umesema, kuna changamoto kadhaa zinazokabili shughuli za ufikishaji misaada ya kibinadamu kaskazini na kusini mwa Ukanda wa Ghaza, na kubainisha kuwa 90% ya misaada hiyo iliyokuwa imeratibiwa kufikishwa kwenye maeneo hayo ama imekataliwa au kuzuiliwa hadi sasa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika mwezi huu wa Septemba.
Aidha, Dujarric ametoa indhari kuwa, watu huko Ghaza wanaendelea kuishi katika hali mbaya ambayo inaweza kuharibika na kuwa mbaya zaidi katika hali ya hewa ya baridi na mvua ya msimu unaokaribia wa baridi kali.
Utawala dhalimu wa Kizayuni ungali unaendeleza vita vya kinyama na mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina wa Ghaza ulivyoanzishwa Oktoba 7 mwaka jana licha ya azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kutaka kusitishwa mara moja mapigano katika eneo hilo.
Hadi sasa Wapalestina zaidi ya 41,500, wengi wao wakiwa wanawake na watoto, wameuawa shahidi na zaidi ya 96,000 wamejeruhiwa katika Ukanda wa Ghaza.
Mashambulizi ya kinyama ya Israel yamewafanya karibu wakazi wote wa Ghaza kuwa wakimbizi kutokana na mzingiro unaoendelea ambao umesababisha uhaba mkubwa wa chakula, maji safi na dawa.
Ikumbukwe kuwa, utawala wa Kizayuni unakabiliwa na kesi ya mauaji ya kimbari katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) kwa vitendo vya kinyama unavyoendeleza huko Ghaza.../