HAMAS kuwaachia askari 4 wanawake wa Israel kwa Wapalestina 200 akiwemo kamanda wa Muqawama
Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema kamanda maarufu wa Palestina ataachiliwa leo ikiwa ni sehemu ya mabadilishano ya pili ya wafungwa na utawala wa Kizayuni wa Israel baada ya usitishaji vita katika Ukanda wa Ghaza kuanza kutekelezwa wiki iliyopita.

Abu Obeida amemtaja Zubeidi kuwa ni mmoja wa wafungwa wa Kipalestina, ambaye alitekeleza operesheni ya kihistoria ya kutoroka gereza la Gilboa la utawala wa wa Kizayuni wa Israel mwaka 2021 kwa kutumia vijiko tu kuchimba shimo kwenye sakafu ya gereza hilo.
Mfungwa huyo anatambuliwa pia kama nembo ya Intifadha ya Pili ya Palestina dhidi ya utawala ghasibu wa Israel.
Kwa mujibu wa Abu Obeida, askari wa jeshi la Kizayuni walivamia nyumba ya Zakaria Zubeidi katika kambi ya wakimbizi ya Jenin kufuatia taarifa za kuwepo matarajio ya yeye kuachiliwa huru, wakampiga na kumfunga mkewe na watoto wake.../