Russia: Iran ina haki ya kujitetea mbele ya mashambulizi ya Marekani, Israel
https://parstoday.ir/sw/news/world-i137330-russia_iran_ina_haki_ya_kujitetea_mbele_ya_mashambulizi_ya_marekani_israel
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia amesisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ina haki ya kujitetea na kukabiliana na hujuma za Marekani na Israel na ametoa wito wa kusitishwa mashambulizi ya Marekani na Israel na kurejea kwenye meza ya mazungumzo.
(last modified 2026-03-13T04:06:19+00:00 )
Mar 13, 2026 04:06 UTC
  • Maria Zakharova
    Maria Zakharova

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia amesisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ina haki ya kujitetea na kukabiliana na hujuma za Marekani na Israel na ametoa wito wa kusitishwa mashambulizi ya Marekani na Israel na kurejea kwenye meza ya mazungumzo.

Maria Zakharova amesema, kwa mujibu wa Mada ya 51 ya Hati ya Umoja wa Mataifa, Iran kama zilivyo nchi nyingine, inayo haki ya kujitetea mbele ya hujuma za kijeshi za Marekani na Israel. Amesema: Moscow inaitaka Marekani na Israel kukomesha mashambulizi na kurudi kwenye meza ya mazungumzo.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia amesema, Moscow itaendeleza hatua zake kwa ajili ya kusitishwa mapigano haraka katika eneo la Magharibi mwa Asia na kutafuta suluhisho la hitilafu zilizopo kwa kutumia njia za amani.

Kuhusu mapendekezo ya Russia kwa ajili ya kusitishwa mashambulizi dhidi ya Iran na kukomeshwa mgogoro wa Asia Magharibi, Maria Zakharova amesema: “Tumetayarisha mapendekezo yanayofaa na kwa sasa tunafanya mawasiliano kuhusiana na kadhia hii.”