-
Uhusiano wa kibiashara wa Iran na Oman wazidi kustawi
Jan 29, 2025 00:06Waziri wa Viwanda, Madini na Biashara wa Iran ametangaza habari ya kuzidi kustawi na kuimarika uhusiano wa kibiashara baina ya Jamhuri ya Kiislamu na Oman.
-
Iran yasikitishwa na shambulio la droni lililoua 70 hospitalini Darfur, Sudan
Jan 27, 2025 08:56Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmail Baghaei amelaani shambulio la ndege isiyo na rubani dhidi ya hospitali moja katika mji wa El Fasher katika mkoa wa magharibi wa Darfur nchini Sudan, na kusababisha vifo vya makumi ya watu.
-
Iran yakanusha tuhuma za Israel za kupeleka silaha Lebanon
Jan 25, 2025 08:05Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amepuuzilia mbali madai ya Israel kamba Jamhuri ya Kiislamu inasafirisha kimagendo silaha kwenda Lebanon.
-
Afkham: Azimio la Bunge la Ulaya dhidi ya Iran halina msingi wa kisheria
Jan 25, 2025 07:51Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Haki za Binadamu na Masuala ya Wanawake ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema azimio lililopasishwa hivi karibuni na Bunge la Ulaya dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu halina msingi wowote wa kisheria na linaonyesha tabia ya uingiliaji ya chombo hicho.
-
Pezeshkian: Iran na Russia hazitakubali kuburuzwa na maadui
Jan 24, 2025 23:33Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amesema kuwa, mapatano kamili ya ushirikiano wa kistratejia kati ya Iran na Russia yanaonyesha kwamba Tehran na Moscow kamwe hazitakubali matakwa ya kupindukia ya maadui, akisisitiza kuwa nchi mbili hizi zitashirikiana kuunda sera zinazotoa kipaumbele kwa masuala ya utulivu, usalama, maendeleo na ustawi wa uchumi katika eneo.
-
Pezeshkian awataka Wairani kuwa macho mkabala wa njama za maadui
Jan 23, 2025 04:18Rais wa Iran amesisitiza haja ya kudumisha umoja wa kitaifa nchini, wakati huu ambapo maadui wa taifa hili wanakula njama na kutaka kutumia vibaya mizozo ya ndani.
-
Zarif: Iran sio tishio la usalama kwa nchi yoyote ile
Jan 23, 2025 04:07Makamu wa Rais katika Masuala ya Kistratejia wa Iran, Mohammad Javad Zarif amesema Jamhuri ya Kiislamu si tishio la usalama kwa nchi yoyote ile duniani, akisisitiza kwamba kama Tehran ingelikusudia kutengeneza silaha za nyuklia, ingelikuwa imefanya hivyo zamani.
-
Iran: Tuko tayari kuanzisha upya mazungumzo ya kuondoa vikwazo
Jan 21, 2025 23:20Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayehusika na Masuala ya Kisheria, Kazem Gharibabadi amesema kuna misingi na fursa zinazofaa za kuanzisha tena mazungumzo na pande nyingine.
-
Iran yasisitiza kuwa uwezo wake wa kiulinzi na kijeshi hauwezi katu kuwa suala la kujadiliwa
Jan 20, 2025 23:08Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Esmaeil Baghaei amesema, uwezo wa kiulinzi wa Iran hauwezi katu kuwa suala la kujadiliwa na kuzungumziwa.
-
Kutekelezwa Makubaliano ya Kifedha kati ya Iran na Russia
Jan 20, 2025 23:03Gavana wa Benki Kuu ya Iran, Mohammadreza Farzin, amesema kuwa kupitia utekelezaji wa makubaliano ya kifedha kati ya Iran na Russia, sarafu za mataifa haya mawili zitakuwa msingi wa biashara kati ya nchi hizo kwa mujibu wa kiwango cha mabadilishano kilichokubaliwa sokoni.