-
Kengele ya hatari ya Russia kuhusu matokeo mabaya ya chokochoko yoyote dhidi ya Iran
Feb 11, 2026 10:29Serikali ya Russia imeonya kuhusu matokeo mabaya ya kuanzisha chokochoko yoyote dhidi ya Iran.
-
Rais wa Colombia asema amenusurika jaribio la mauaji
Feb 11, 2026 09:32Rais Gustavo Petro wa Colombia amesema alinusurika jaribio la mauaji jana Jumanne, baada ya miezi kadhaa ya maonyo kuhusu njama inayomlenga ya wafanyabiashara wa dawa za kulevya.
-
Maelfu waandamana Australia kupinga ziara ya rais wa utawala wa Israel
Feb 11, 2026 07:02Ziara rasmi ya rais wa utawala wa Israel, Isaac Herzog, nchini Australia ilikumbwa na maandamano makubwa siku ya Jumatatu, huku maelfu ya waandamanaji wakijitokeza katika miji kadhaa, hali iliyopelekea kuwepo makabiliano na polisi.
-
Mgombea ugavana wa Republican huko Florida: Ukuta wa Kuomboleza huko Israel ni ukuta wa kijinga
Feb 11, 2026 06:56Mgombea wa chama cha Republican katika nafasi ya gavana wa Florida, James Fishbach, amezua mzozo wa kisiasa baada ya shambulio lake la moja kwa moja dhidi ya Ukuta wa Magharibi (Wailing Wall) na ahadi yake ya kukata uhusiano wote wa kiuchumi na Israel kama atashinda kiti hicho.
-
Ramaphosa na Putin wajadili suala la kuhitimisha vita kati ya Russia na Ukraine
Feb 11, 2026 06:55Rais wa Vladimir Putin wa Russia amefanya mazungumzo ya simu na mwenzake wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa ambapo pande hizo mbili zimejadili kuhusu suluhu inyoweza kufikiwa nchini Ukraine.
-
Macron: Utawala wa Trump una uadui na Umoja wa Ulaya na unataka kuuvunja
Feb 11, 2026 06:55Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, amesema kwamba utawala wa Rais wa Marekani, Donald Trump unaonyesha uadui dhidi ya Umoja wa Ulaya na unataka kuuvunja.
-
Lavrov: Kadhia ya Epstein imedhihirisha sura halisi ya 'kuabudu shetani' ya watu mashuhuri wa Magharibi
Feb 10, 2026 03:15Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia Sergey Lavrov amesema, mtindo mchafu wa maisha wa mfadhili na mhalifu wa vitendo vya ngono wa Marekani Jeffrey Epstein pamoja na tapo lake ni ushuhuda wa kuporomoka kimaadili shakhsia muhimu na maarufu wa Magharibi.
-
Maandamano katika miji mikuu mingi ya kutaka kuingizwa misaada Gaza na kulaani jinai za Israel
Feb 09, 2026 06:38Miji mikuu mingi ya dunia imeendelea kushuhudia maandamano ya kulaani ukiukaji unaoendelea wa utawala wa Kizayuni wa makubaliano ya kusitisha mapigano katika Ukanda wa Gaza.
-
Kwa nini China inatetea "haki ya nyuklia" ya Iran?
Feb 09, 2026 02:23China kwa mara nyingine tena imesisitiza juu ya kutetea haki ya nyuklia ya Iran.
-
Italia yasema haiwezi kujiunga na 'Bodi ya Amani' ya Trump, sababu ni kukinzana na katiba yake
Feb 08, 2026 06:18Italia imesema haiwezi kujiunga na kinachoitwa "Bodi ya Amani" ya Rais wa Marekani Donald Trump kutokana na "mpaka wa kikatiba" ukiwa ni mkwamo mpya na wa karibuni zaidi kukikabili "chombo hicho cha kimataifa cha kujenga amani", alichojibunia rais wa Marekani.