-
Malaki waandamana Hague, Brussels kuonyesha mshikamano na Gaza
Jun 16, 2025 10:22Makumi ya maelfu ya watu waliovalia mavazi mekundu wameandamana katika mitaa ya mji wa Hague nchini Uholanzi na mjini Brussels huko Ubelgiji kuonyesha mshikamano na Wapalestina wa Gaza sanjari na kushinikiza hatua zaidi kutoka kwa serikali zao dhidi ya mauaji ya kimbari katika eneo hilo la Palestina lililozingirwa.
-
Balozi wa Marekani Israel: Nilikimbilia kwenye mahandaki mara tano jana usiku
Jun 14, 2025 10:48Balozi wa Marekani huko Israel amesema kwamba usiku uliopita ulikuwa usiku mzito sana kwake wakati Iran ilipofanya mashambulizi ya kulipiza kisasi na kupiga maeneo muhimu na nyeti ya Israel kiasi kwamba yeye na wenzake walilazimika kukimbilia kujificha kwenye mahandaki mara tano kwa hofu ya makombora ya Iran.
-
Dunia yalaani mashambulio ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Iran
Jun 14, 2025 02:22Hujuma za mapema alfajiri ya jana za utawala wa Kizayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zimeendelea kulaaniwa katika kila pembe ya dunia.
-
Korea Kaskazini, China, Russia: Tuko pamoja na Iran
Jun 14, 2025 02:22Nchi za Korea Kaskazini, China na Russia zimetangaza kuwa ziko pamoja na Iran katika mashambulizi ya jana Ijumaa ya Israel dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Zaidi ya watu 200 waaga dunia katika ajali ya ndege ya abiria nchini India
Jun 12, 2025 12:27Ndege ya India, Air India, iliyokuwa inaelekea London ikiwa na abiria 242 imepata ajali na kuanguka dakika chache tu baada ya kupaa kutoka mji wa magharibi mwa India wa Ahmedabad Alkhamisi.
-
Waandamanaji 330 watiwa mbaroni Los Angeles Marekani
Jun 12, 2025 10:42Msemaji wa Ikulu ya Marekani amezungumzia hali ya mji wa Los Angeles baada ya kuzuka maandamano makubwa ya wananchi dhidi ya sera za uhamiaji za utawala wa Trump na kuosema kuwa, hadi hivi sasa wahajiri 330 wametiwa mbaroni mjini Los Angeles (pekee) ikiwa ni sehemu ya kukandamiza kilio cha wananchi.
-
IOM: Haiti inakabiliwa na janga la kihistoria la wakimbizi wa ndani huku machafuko yakizidi kupanuka
Jun 12, 2025 02:10Idadi ya watu waliolazimika kuyakimbia makazi yao ndani ya Haiti imefikia takriban milioni 1.3, ikiwa ni ongezeko la asilimia 24 tangu Desemba 2024, na sasa ndiyo idadi kubwa zaidi kuwahi kurekodiwa kutokana na machafuko nchini humo, kwa mujibu wa taarifa ya Jumatano kutoka Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM).
-
Marufuku ya kutembea usiku yatangazwa Los Angeles. maandamano yaenea Marekani
Jun 11, 2025 13:05Watawala wa jiji la Los Angeles wametangaza marufuku ya kutembea usiku katikati mwa jiji hilo ili kudhibiti maandamano yanayochochewa na msako mkali dhidi ya wahamiaji, hali ambayo sasa imeenea hadi miji mingine ya Marekani.
-
Pep Guardiola asikitishwa sana na masaibu ya Wapalestina Gaza
Jun 11, 2025 12:34Pep Guardiola, Kocha wa timu ya Manchester City nchini Uingereza, ameelezea kwa uchungu hali ya mateso ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, akisema ni jambo linalomuumiza sana kila anapofikiria yanayoendelea katika eneo hilo.
-
Utafiti: Uislamu ndiyo dini inayokuwa kwa kasi zaidi duniani
Jun 11, 2025 07:53Utafiti mpya umebainisha kuwa, idadi ya Waislamu duniani imeongezeka zaidi kuliko dini nyingine zote kwa pamoja, katika kipindi cha muongo mmoja uliopita.