-
Mamdani achaguliwa Meya wa kwanza Mwislamu wa Jiji la New York katika ushindi wa kihistoria
Nov 05, 2025 07:10Zohran Mamdani mbunge Muislamu amechaguliwa kuwa Meya wa 111 wa jiji la New York, mtu wa kwanza mwenye asili ya Asia Kusini na wa kwanza aliyezaliwa barani Afrika kuongoza jiji kubwa zaidi nchini Marekani.
-
Padri Mfaransa atuhumiwa kuwadhalilisha kingono wakimbizi watoto
Nov 05, 2025 03:06Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki la Rabat nchini Morocco jana aliliambia shirika la habari la AFP kuwa "ameshirikiana kikamilifu" na mamlaka za Morocco na nje ya nchi baada ya kasisi wa Ufaransa kutuhumiwa kwa kuwadhalilisha kingono wakimbizi watoto huko Casablanca.
-
Trump asema siku za Rais Maduro wa Venezuela kuweko madarakani zinakaribia ukingoni
Nov 04, 2025 02:24Katika kile kinachotafsiriwa kama harakati ya kibeberu na ya kuingilia masuala ya ndani ya mataifa mengine, Rais wa Marekani Donald Trump ameashiria kuwa siku za Rais Nicolas Maduro wa Venezuela kuweko madarakani zinakaribia ukingoni, huku mvutano kati ya nchi hizo mbili ukiwa unaongezeka sambamba na Washington kushamirisha kuwepo kwake kijeshi katika eneo la Carribean.
-
Marekani haina uwezo wa kukabiliana na kombora la Burevestnik la Russia
Nov 03, 2025 02:22Afisa wa zamani wa masuala ya kijasusi wa Marekani ambaye pia ni mkaguzi wa zamani wa Umoja wa Mataifa amesema kwamba Marekani haina mfumo wa ulinzi wa makombora unaoweza kukabiliana na shambulio la kombora la Burevestnik la Russia.
-
Kuna taathira gani za kufukuzwa Mwanamfalme Andrew katika mfumo wa ufalme wa Uingereza?
Nov 02, 2025 11:34Mapema usiku wa Ijumaa, Kasri ya Buckingham ilitoa taarifa rasmi ikitangaza kwamba Mwanamfalme Andrew amevuliwa vyeo vyote vya kifalme, majukumu rasmi na fursa za heshima, uamuzi ambao Mfalme Charles III aliutaja kuwa "usioepukika" kwa ajili ya kuepusha taasisi ya ufalme kuzama kwenye wimbi la kutoaminika nchini Uingereza.
-
Obama: Nyakati za giza zinatawala Marekani
Nov 02, 2025 11:09Rais wa zamani wa Marekani, Barack Obama amemkosoa vikali Donald Trump, akiutaja utawala wake kuwa ni "kielelezo cha uasi na mparaganyiko" na kuwashutumu Warepublican kwa kukaa kimya mbele ya mienendo yake ya kutowajibika.
-
Mauaji ya halaiki ya El-Fasher yachochea tena miito ya kutaka UAE isusiwe kwa kuiunga mkono RSF
Nov 02, 2025 06:49Wito wa kuususia Muungano wa Falme za Kiarabu (UAE) pamoja na makampuni yenye mfungamano na nchi hiyo ya kifalme unazidi kuongezeka kwenye mitandao ya kijamii, ukichochewa na hasira zinazotokana na uungaji mkono wa serikali ya Abu Dhabi kwa Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF) katika vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Sudan.
-
UNSC yapitisha azimio la US la kuunga mkono mpango wa Morocco kuhusu Sahara Magharibi
Nov 02, 2025 06:23Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepiga kura ya kurefusha kwa mwaka mmoja muda wa kazi za ujumbe wake ulioko Sahara Magharibi (MINURSO), sambamba na kuidhinisha rasmi mpango wa serikali ya Morocco wa kutoa mamlaka ya ndani kwa eneo hilo kama msingi pekee wa kutatua mgogoro huo wa miongo kadhaa, hatua ambayo imesababisha mpasuko mkubwa katika jamii ya kimataifa.
-
Kwa nini UN inayataja mashambulizi ya Marekani katika Bahari ya Karibi kuwa ni kinyume na sheria za kimataifa?
Nov 02, 2025 04:50Kamishna wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa ametangaza kuwa mashambulizi ya Marekani katika eneo la Caribbean yanakiuka sheria za kimataifa.
-
Jinsi himaya isiyo na masharti ya Ujerumani kwa Israel inavyoakisi unafiki wa vigezo vya Magharibi vya haki za binadamu
Nov 01, 2025 12:29Msemaji wa harakati ya Hamas amekosoa kauli za Kansela wa Ujerumani Friedrich Mertz za kujaribu kutetea uhalifu na jinai za utawala haramu wa Israel dhidi ya watu wa Palestina.