-
Kamishna wa Haki za Binadamu UN: Mapigano yasitishwe Gaza na Lebanon, aonya kuhusu ukiukwaji wa haki za binadamu Sudan
Jun 15, 2026 12:26Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa amesisitiza haja ya kuimarishwa usitishaji mapigano huko Gaza na kufikiwa makubaliano endelevu ya kusitisha mapigano, akibainisha kuwa vikosi vya jeshi la Israel vimewaua Wapalestina wapatao 1,000 tangu usitishaji mapigano Oktoba mwaka jana, pamoja na kuimarisha vizingiti vya kuzuia misaada ya kibinadamu kwa watu wa Gaza, jambo ambalo amesema limezidisha mgogoro wa binadamu katika sekta hiyo.
-
Wapiga picha wa Gaza washinda Tuzo ya Kalamu ya Dhahabu ya Uhuru
Jun 15, 2026 11:19Jumuiya ya Wachapishaji Habari Duniani imetangaza kwamba tuzo ya Kalamu ya Dhahabu ya Uhuru 2026 itatolewa kwa wapiga picha na wakurugenzi wa video kutoka Ukanda wa Gaza ulioharibiwa na vita.
-
Washington Post: Trump anasherehekea kurudi katika hali ya kabla ya vita na Iran
Jun 15, 2026 10:09Gazeti la Washington Post, katika ripoti yake kuhusu hati ya makubaliano kati ya Iran na Marekani, limekejeli hatua ya Rais Donald Trump wa Marekani ya kusherehekea kurejea Washington kwenye hali ya kabla ya Februari 28, hatua ambayo baadhi ya wataalamu wanaamini ni kurudi nyuma kwa maana halisi ya neno hilo mkabala wa Iran.
-
Viongozi wa dunia wakaribisha makubaliano ya kumaliza vita vya Marekani dhidi ya Iran
Jun 15, 2026 04:28Viongozi mbalimbali duniani wamekaribisha hati ya makubaliano (MoU) kati ya Iran na Marekani, ambayo inahitimisha mara moja vita vya kichokozi vilivyoanzishwa na Marekani na Israel dhidi ya Iran, kuondoa mzingiro wa baharini, na kufungua tena Lango Bahari la Hormuz kwa usafiri wa kimataifa.
-
Jezi za Kombe la Dunia zilizopewa jina la mtoto wa Kipalestina aliyeuawa na Isral zazinduliwa
Jun 15, 2026 04:27Fulana za michezo zenye jina la "Jezi ya Kombe la Dunia ya Hind Rajab" zimezinduliwa rasmi sambamba na mashindano ya kombe hilo yanayoendelea katika nchi za Marekani, Canada na Mexico; jezi ambazo zimebuniwa na kutengenezwa kwa idhini ya mama wa "Hind Rajab", mtoto wa Kipalestina aliyeuawa shahidi na askari wa Israel.
-
Waziri Mkuu wa Pakistan: Makubaliano kati ya Iran na Marekani 'yanatarajiwa ndani ya saa 24'
Jun 14, 2026 03:14Waziri Mkuu wa Pakistan Shehbaz Sharif amesema kuwa makubaliano kati ya Iran na Marekani kwa lengo la kukumaliza vita yapo "karibu zaidi kuliko wakati mwingine wowote," huku yakitarajiwa kukamilika ndani ya saa 24 zijazo.
-
Rais wa Cuba atangaza mageuzi mapya ya kiuchumi ili kukabiliana na mzingiro wa kijinai wa Marekani
Jun 13, 2026 11:14Rais wa Cuba atangaza mageuzi mapya ya kiuchumi ili kukabiliana na mzingiro wa kijinai wa Marekani
-
Tucker Carlson: Marekani imeshindwa kufungua Lango-Bahari la Hormuz
Jun 13, 2026 07:57Tucker Carlson, mwanahabari maarufu wa kihafidhina wa Marekani, amesema kwamba matukio ya sasa katika mzozo wa Asia Magharibi yanaonyesha mapungufu ya nguvu ya kijeshi ya Marekani, akisisitiza kwamba Washington imeshindwa kufungua tena Lango-Bahari la Hormuz licha ya kutumia gharama kubwa.
-
'Nchi inayoshiriki mauaji ya kimbari Gaza inataka kusafisha sura yake chafu kwa kuandaa Kombe la Dunia 2026'
Jun 12, 2026 13:52Nyota wa zamani wa soka wa Misri na mchambuzi wa masuala ya michezo, Mohamed Aboutrika, ameibua wimbi kubwa la majibizano na mijadala kwenye mitandao ya kijamii, baada ya kukosoa sera za undumakuwili katika kuandaa mashindano makubwa ya michezo, na jitihada za baadhi ya nchi za kutumia michezo kama wenzo wa kutakasa na kusafisha sura zao chafu za kisiasa.
-
Rais wa Colombia aishambulia Israel katika Baraza la Usalama la UN, asema ni utawala wa kinazi
Jun 12, 2026 04:44Rais wa Colombia, Gustavo Petro, ameifananisha Israel na "utawala wa Nazi" katika maoni yake kuhusu vita vya kuangamiza vya Tel Aviv katika Ukanda wa Gaza.