Spika wa zamani wa Baraza la Wawakilishi la Marekani Nancy Pelosi amesema, waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel ni kizuizi cha kupatikana amani Ghaza na anapaswa ajiuzulu.
Shirika la Kimataifa la Msamaha Duniani la Amnesty International limetangaza kuwa, haki za binadamu zingali zinakabiliwa na tishio kubwa katika maeneo mbalimbali duniani.
Utafiti wa hivi karibuni katika zaidi ya nchi 130 uliofanywa na shirika la uchunguzi wa maoni la Marekani la Gallup umebaini kuwa umashuhuri wa Marekani umeshuka katika nchi nyingi za bara Afrika.
Jamaica inasema imeamua kuitambua rasmi Palestina kama taifa huku kukiwa na wasiwasi wa muda mrefu juu ya vita vya Israel vinavyoendelea katika Ukanda wa Gaza na mzozo mbaya wa binadamu katika eneo hilo lililozingirwa.
Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya amesema kuwa vita vya Israel dhidi ya Gaza vimesababisha uharibifu mkubwa kwenye miji ya eneo hilo kuliko ule uliosababishwa na Vita vya Pili vya Dunia kwenye miji ya Ujerumani.
Summer Lee kutoka jimbo la Pennsylvania amefanikiwa kuibuka na ushindi katika uchaguzi wa wagombea wa Baraza la Wawakilishi la Marekani kwa kuungwa mkono kwa kura za wananchi wa Marekani wanaowatetea wananchi madhlumu wa Palestina licha ukwamishaji na vizuizi vya Lobi ya Kizayuni ya AIPAC.
Watu wasiopungua 5 wamekufa walipokuwa wakivuka njia ya majini ya English Channel, saa chache baada ya Uingereza kuidhinisha muswada wa kuwafukuza wahamiaji nchini humo na kuwapeleka Rwanda.
Ripoti mpya ya Shirika la Fedha la Maendeleo ya Kimataifa imefichua kuwa karibu nusu ya watu duniani wanaishi katika nchi ambako fedha zinazotolewa kulipa madeni zinazidi fedha za matumizi ya huduma za msingi za kijamii kkama elimu na afya.
Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa amekemea vikali mashambulio ya kinyama na ya mfululizo yaliyofanywa hivi karibuni na jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda Gaza na kuua zaidi wanawake na watoto.
Waziri wa Ulinzi wa Russia Sergey Shoigu amesema, hasara za kijeshi ilizopata Ukraine za kuuawa askari wake tangu Februari 2022 hadi sasa zimefikia karibu wanajeshi 500,000.