-
Kenya kufungua tena mpaka wake na Somalia baada ya kufungwa kwa miaka 15
Feb 13, 2026 10:48Rais wa Kenya William Ruto ametangaza kuwa Kenya itafungua tena mpaka wake na Somalia mwezi Aprili, baada ya kufungwa kwa muda wa miaka 15 kufuatia mashambulizi ya mara kwa mara ya kigaidi. Hatua hiyo inaashiria jaribio jipya la kurejesha harakati za mpakani na kuimarisha ushirikiano wa kikanda.
-
Umoja wa Afrika wapongeza mapatano ya kusitisha vita kati ya Serikali ya DRC na waasi wa M23
Feb 13, 2026 10:32Tume ya Umoja wa Afrika (AU) imekaribisha kutiwa saini kwa kanuni za marejeo ya mfumo wa kusitisha mapigano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na muungano wa waasi wa AFC/M23.
-
Takriban watu 21 wameaga dunia baada ya boti kuzama katika Mto Nile, Sudan
Feb 13, 2026 07:20Takriban watu 21 wamekufa maji wakati boti iliyokuwa ikiwasafirisha ilipozama katika Mto Nile kaskazini mwa Sudan.
-
Mashambulizi ya droni ya wanamgambo wa RSF yaua watu 2 na kujeruhi 4 Kordofan, Sudan
Feb 13, 2026 07:20Mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (droni) za wanamgambo wa kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) yameuwa raia wawili na kujeruhi wanne katika jimbo la Kordofan Kusini. Haya yamebainishwa jana Mtandao wa Madaktari wa Sudan.
-
Afrika Kusini: Ramaphosa atangaza kutumwa jeshi kukabiliana na jinai
Feb 13, 2026 07:19Katika jitihada za kupunguza viwango vya juu vya magenge ya uhalifu na jinai nyingine, Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini ametangaza kuwa atatuma jeshi ili kushirikiana na polisi katika suala hilo.
-
AU yasisitiza kuunga mkono umoja wa Somalia; yalaani kuingiliwa masuala ya ndani ya Sudan
Feb 13, 2026 02:49Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika (AU) kwa mara nyingine tena jana Alhamisi lilithibitisha kuhusu mamlaka ya kujitawala na umoja wa ardhi nzima ya Somalia na kutupilia mbali suala la kutambuliwa rasmi eneo la Somaliland kama nchi huru.
-
Sudan yataka irejeshewe uanachama katika Umoja wa Afrika
Feb 13, 2026 02:02Waziri wa Mambo ya Nje wa Sudan, Muhi al-Din Salem Ahmed amekariri wito wake kwa Umoja wa Afrika, akiitaka AU kufuta hatua yake ya kuisimamishia uanachama nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika katika umoja huo.
-
Wazimbabwe watofautiana baada ya mawaziri kupitisha mswada wa kuongeza muda wa rais kusalia madarakani
Feb 12, 2026 11:22Wazimbabwe wametofautiana kuhusu hatua ya baraza la mawaziri ya kuunga mkono muswada unaokusudia kubadilisha katiba ili kumruhusu Rais Emmerson Mnangagwa mwenye umri wa miaka 83 kubakia madarakani hadi angalau mwaka 2030.
-
Libya yatoa leseni za kwanza za mafuta kwa makampuni ya nishati ya nje tangu kupinduliwa Gaddafi
Feb 12, 2026 11:21Libya imetoa leseni kwa ajili ya uchimbaji na uzalishaji mafuta kwa makampuni kadhaa za nishati za kigeni, ikiwa ni pamoja na makampuni makubwa ya Chevron na BP kwa mara ya kwanza tangu kupinduliwa mamlakani kiongozi wa muda mrefu wa nchi hiyo Kanali Muammar Gaddafi.
-
Serikali ya Kenya yamuongezea mchungaji Mackenzie mashtaka kwa vifo vya watu wengine 52
Feb 12, 2026 06:30Paul Mackenzie, kiongozi wa tapo la kikristo nchini Kenya aliyewaamuru wafuasi wake wajiue kwa njaa wao na watoto wao ili waende mbinguni amesomewa shtaka jengine jipya yeye na wenzake saba la kusababisha vifo vingine 52, kupitia mahubiri yake.