-
Serikali ya Kenya: Haturuhusu ICC kuchunguza visa vya mashambulizi ya “wahuni”
Aug 24, 2026 13:39Serikali ya Kenya imekataa wito wa upinzani na mashirika ya kiraia kwa Mahakama ya Kimataifa unaotaka Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) ichunguze ongezeko la ghasia za kisiasa nchini humo katia kipindi hiki cha kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2027.
-
Watu wasiopungua 30 wamefariki dunia kufuatia kuporomoka rundo kubwa la taka huko Conakry, Guinea
Aug 24, 2026 13:31Watu wasiopungua 30 wamefariki dunia baada ya rundo kubwa la taka kuporomoka katika dampo kubwa zaidi huko Conakry, nchini Guinea.
-
Malik Agar: Chaguo letu ni suluhisho la kijeshi hadi mazingira ya mazungumzo yatakapotimizwa
Aug 23, 2026 14:19Malik Agar, naibu mkuu wa Baraza Kuu la Utawala nchini Sudan, amesema kwamba chaguo la sasa ni suluhisho la kijeshi mpaka pale mazingira ya kufanyika mazungumzo yatakapotimizwa, akisisitiza kwamba Khartoum inalitaka kundi la Rapid Support Forces (RSF) kuondoka katika miji na maeneo ya makazi ya raia kabla ya mazungumzo yoyote kuanza.
-
Rais wa zamani wa Kongo, Joseph Kabila, apinga vikwazo vya US mahakamani
Aug 23, 2026 13:54Katika kesi iliyofanyika mahakamani huko Washington, Joseph Kabila ambaye aliongoza Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuanzia 2001 hadi 2019 ametaka jina lake liondolewe kwenye orodha nyeusi ya Wizara ya Fedha ya Marekani.
-
UNICEF: Mgogoro wa njaa kwa watoto Somalia wazidi kuwa mbaya baada ya kupunguzwa misaada
Aug 23, 2026 03:22Mfuko wa Kuhudumia Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) umeonya kuwa, utapiamlo unaotishia maisha miongoni mwa watoto nchini Somalia unaongezeka kwa kasi, huku zaidi ya vituo 200 vya afya na lishe vikilazimika kufungwa kutokana na kupunguzwa misaada ya kimataifa.
-
Tunisia yaopoa miili ya wahamiaji wanne baada ya boti kuzama karibu na pwani ya nchi hiyo
Aug 23, 2026 03:14Mamlaka za Tunisia imepata miili ya wahamiaji wanne wasio na vibali karibu na pwani ya Ben Guerdane, kusini-mashariki mwa nchi hiyo, baada ya boti iliyokuwa imebeba watu 15 kupinduka. Haya yameelezwa jana na Shirika la Kutetea Haki za Binadamu.
-
Rais Samia azindua mradi mkubwa utakaochangia nusu ya umeme unaozalishwa Tanzania
Aug 22, 2026 13:10Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amezindua Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Julius Nyerere, hatua inayofungua rasmi kuanza kwa kazi ya mojawapo ya miradi mikubwa zaidi ya miundombinu nchini humo na mradi mkubwa zaidi wa kuzalisha umeme unaofadhiliwa na serikali.
-
UN yaonya: Mlipuko wa Ebola nchini DR Congo 'unaongezeka kwa kasi' baada ya zaidi ya watu 2,500 kuaga dunia
Aug 22, 2026 03:29Umoja wa Mataifa ulitangaza jana Ijumaa kwamba virusi vya Ebola vinaenea kwa kasi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya kuua zaidi ya watu 2,500, ukitoa wito wa kutolewa misaada zaidi na kuonya kwamba ufadhili uliotolewa hadi sasa utaisha ndani ya wiki chache.
-
WFP: Mamilioni ya watu wanakabiliwa na baa la njaa nchini Somalia
Aug 22, 2026 02:49Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limetangaza kuwa, watu milioni sita nchini Somalia wanakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula.
-
Mahakama ya Tanzania: Tundu Lissu ana kesi ya kujibu ya uhaini
Aug 21, 2026 12:31Mahakama Kuu ya Tanzania imeamua kwamba Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA, Tundu Lissu, ana kesi ya kujibu katika kesi ya uhaini inayomkabili, hatua inayofungua njia kwa mwanasiasa huyo kuanza kujitetea.