-
Maelfu waandamana kupinga usajili vitani kwa vijana Tigray
Jul 20, 2026 03:59Maelfu ya watu walikusanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia, kushiriki maandamano ya kuunga mkono serikali na kupinga madai ya kampeni ya mamlaka katika eneo la Tigray kuwasajili kwa lazima vijana kupigana vitani.
-
Raia 114 wauawa mashariki mwa Kongo mwezi Juni
Jul 19, 2026 12:44Waasi wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo mwezi uliopita waliwauwa watu wasiopungua 114 kuwatekanyara wengine 17. Haya yameelezwa Shirika la Ufuatiliaji Usalama la Kivu Security Tracker.
-
Tunisia inakabiliwa na joto kali huku viwango vya joto vikikaribia nyuzi joto 50
Jul 19, 2026 12:40Wimbi kali la joto lisilo la kawaida limeikumba Tunisia, na kusababisha viwango vya joto kupanda hadi karibu nyuzi joto 50 Selsiasi na kuvunja rekodi za kihistoria katika maeneo kadhaa nchini humo.
-
Ripoti: Watoto laki tano walio na umri chini ya miaka 5 nchini Madagascar wana utapiamlo
Jul 19, 2026 02:26Zaidi ya watu milioni 3.7 nchini Madagascar wanatarajiwa kukabiliwa na njaa kali huku hatari ya utapiamlo ikiongezeka miongoni mwa watoto na makundi yaliyo katika mazingira magumu.
-
UNICEF yahimiza ulinzi wa watoto wakati wa migogoro ya usalama na binadamu
Jul 18, 2026 11:51Mkuu wa Shirika la Watoto la Umoja wa Mataifa (UNICEF) ametembelea kaskazini magharibi mwa Nigeria, wakati migogoro, umaskini na ukosefu wa usalama wa chakula vikiwalazimisha mamilioni ya watoto katika eneo hilo kuhitaji msaada ya dharura.
-
Khartoum yatoa ushahidi dhidi ya UAE na kuikosoa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai
Jul 18, 2026 09:07Waziri wa Sheria wa Sudan, Abdullah Darf, amewasilisha kifurushi cha njia za kisheria "zisizo za kawaida" ambazo serikali ya Khartoum inakusudia kuchukua ili kufungua mashtaka dhidi ya serikali ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na kundi la waasi la Rapid Support Forces (RSF), akisisitiza kwamba Khartoum ina "ushahidi wa kutosha na data kamili" kuhusu "ushiriki wa Abu Dhabi katika vita na uhalifu uliofanywa na pande hizo mbili dhidi ya watu wa Sudan."
-
Vurugu uchaguzi mdogo Kenya zaibua wasiwasi kuelekea uchaguzi mkuu 2027
Jul 18, 2026 03:30Mashambulio dhidi ya wapiga kura wakati wa uchaguzi mdogo katika eneo bunge la Ol Kalou katika mkoa wa kati nchini Kenya, yameibua hofu kuhusu hali ya usalama kuelekea uchaguzi mkuu hapo mwakani 2027.
-
Ajali mbaya ya basi la shule Uganda yaua watoto 20
Jul 17, 2026 11:41Watoto wasiopungua 20 na mtu mmoja mzima wamefariki dunia baada ya basi la shule walilokuwa wakisafiria kupata ajali katika Wilaya ya Kapchorwa, mashariki mwa Uganda, polisi wamesema.
-
Ebola yazidi kuwa tishio katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
Jul 17, 2026 02:57Mlipuko wa maradhi ya Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo unasambaa zaidi ya juhudi zinazochukuliwa za kuudhibiti huku zaidi ya watu 2,000 wakiambukizwa na zaidi ya 750 wakiwa wameaga dunia.
-
Eritrea yajizatiti kukabiliana na tamaa ya Ethiopia; wasiwasi waongezeka kuhusu kurejea mvutano Pembe ya Afrika
Jul 17, 2026 02:48Dalili za kuongezeka kwa mvutano kati ya Eritrea na Ethiopia zimeibua wasiwasi wa uwezekano wa kurejea mgogoro kati ya mataifa hayo mawili ya Pembe ya Afrika.