-
Rais Macron akabiliwa na upinzani baada ya matamshi yake makali kwenye mkutano wa Nairobi
May 13, 2026 12:14Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron anakabiliwa na upinzani mkali baada ya kukatiza kikao cha mjadala katika kongamano la Africa Forward Summit nchini Kenya akiwataka hadhirina wanyamaze kimya.
-
Ghana kuwarejesha nyumbani mamia ya raia walioko Afrika Kusini
May 13, 2026 12:05Ghana imetangaza kwamba imeanzisha mchakato wa kuwahamisha takriban raia wake 300 kutoka Afrika Kusini kufuatia wimbi la maandamano dhidi ya wageni.
-
Kenya yataka Afrika ipewe kiti cha kudumu katika Baraza la Usalama la UN
May 12, 2026 14:25Rais wa Kenya, William Ruto, ametoa wito kwa Afrika kupewa uanachama wa kudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, takwa ambalo limeungwa mkono na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres.
-
UN kujenga ofisi mpya yenye thamani ya dola milioni 340 Nairobi
May 12, 2026 09:01Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amshuhudia uwekezaji mkubwa wa Umoja wa Mataifa wenye thamani ya karibu dola milioni 340 katika ofisi yake katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi.
-
Macron asema Ufaransa “haikuwahi kufikiria” kupeleka jeshi Hormuz bila uratibu na Iran
May 12, 2026 04:28Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema Paris haijawahi kufikiria kupeleka vikosi vya kijeshi vya Ufaransa katika Mlango-Bahari wa Hormuz bila uratibu na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, wakati mvutano unaochochewa na vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran ukiendelea.
-
Ramaphosa: Hujuma dhidi ya wageni haziakisi maoni ya Afrika Kusini
May 12, 2026 04:04Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amesema kuwa "wahalifu walipanga mashambulizi dhidi ya wageni na kuzitoa hofu nchi nyingine za Afrika, ambazo zimeelezea wasiwasi wao kuhusu raia wake waliopo Afrika Kusini.
-
Zambia yapinga matakwa ya Marekani yanayohusiana na mkataba wa afya na madini
May 10, 2026 10:24Zambia imeishutumu hadharani Marekani kwa kuunganisha kifurushi cha afya kilichopendekezwa cha dola bilioni 2 na matakwa kupewa data na madini na muhimu, ikisema baadhi ya masharti yaliyoambatanishwa na makubaliano hayo "hayakubaliki".
-
Wananchi wa Mali waandamana kumuunga mkono kiongozi wao wa kijeshi
May 10, 2026 10:09Mamia ya waungaji mkono wa uongozi wa serikali ya kijeshi ya Mali Jumamosi walijumuika katika uwanja wa michezo katika mji mkuu, Bamako ili kuthibitisha uungaji mkono wao kwa serikali ya mpito ya nchi hiyo.
-
Niger yasimamisha vyombo tisa vya habari vya Ufaransa
May 10, 2026 09:28Serikali ya Niger imetangaza kusimamisha shughuli za vyombo tisa vya habari vya Ufaransa, ikieleza kuwa hatua hiyo imechukuliwa kutokana na “usambazaji wa mara kwa mara wa maudhui yanayoweza kuhatarisha kwa kiasi kikubwa utulivu wa umma, umoja wa taifa, mshikamano wa kijamii, na uthabiti wa taasisi za Jamhuri.”
-
Watu 70 wauawa kaskazini mashariki mwa Kongo; Umoja wa Mataifa walaani ghasia
May 10, 2026 07:37Kwa uchache watu 70, wengi wao wakiwa raia, wameuawa katika shambulio lililofanywa na watu wenye silaha waliohusishwa na wanamgambo wa CODECO, kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.