-
Mwandishi maarufu wa Kenya , Ngũgĩ wa Thiong’o, afariki dunia
May 29, 2025 09:55Ngũgĩ wa Thiong’o, gwiji wa fasihi ya Kiafrika na sauti isiyochoka ya ukombozi wa kiakili barani, ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 87, familia yake imethibitisha.
-
Jeshi la Marekani latafakari kuondoka Afrika
May 29, 2025 09:50Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Marekani barani Afrika (AFRICOM) ametangaza mpango wa kutathmini upya uwepo wa jeshi hilo katika bara la Afrika, huku mataifa mengi yakianza kupima upya ushirikiano wao wa kiulinzi na nchi za Magharibi na kuelekeza ushirikiano wao kwa nchi zingine zisizo za kibeberu.
-
Balozi wa Israel atimuliwa na waungaji mkono Palestina, Senegal
May 29, 2025 06:09Balozi wa Israel nchini Senegal, Yuval Waks, alilazimika kuondoka katika Chuo Kikuu cha Dakar baada ya wanafunzi kupinga uwepo wake na kupiga nara za kuunga mkono Palestina chuoni hapa.
-
Namibia yataka fidia ya 'maana' ya mauaji ya halaiki ya Ujerumani
May 29, 2025 06:01Namibia imefanya kumbukizi ya kuwaenzi wahanga wa mauaji ya kibari wakati wa utawala wa kikoloni wa Ujerumani, huku viongozi, wanasiasa na wakuu wa jamii zilizoathirika na ukatili huo wa askari wa Kijerumani wakitoa wito mpya wa kulipwa fidia na Berlin.
-
Waafrika wazidi kuonesha ubinadamu, wampa tunzo maalumu Yahya Sinwar
May 28, 2025 10:47Waafrika kwa mara nyingine wameonesha hisia zao za kuthamini ubinadamu kwa kuenzi nafasi muhimu ya wanamapambano wa Palestina. Tuzo ya ya kila mwaka ya "Kwame Tour" kwa mwaka huu 2025 amepewa kiongozi wa Palestina shujaa shahid Yahya Sinwar (Abu Ibrahim) wakati wa sherehe za kuadhimisha Siku ya Uhuru wa Afrika.
-
Mgogoro wa kibinadamu Sudan unazidi kuongezeka, mapigano yanaendelea
May 28, 2025 10:46Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) imesema kuwa mgogoro wa kibinadamu nchini Sudan unazidi kuongezeka huku mapigano yakiendelea, watu wanazidi kuhama makazi yao na udharura wa kuchukuliwa hatua za kiafya umezidi kuwa mkubwa.
-
Spika wa Bunge la Mashariki Libya atoa mwito wa umoja wa kitaifa
May 28, 2025 10:46Spika wa Bunge lenye makao yake mashariki mwa Libya, Aguila Saleh ametoa mwito wa kuundwa serikali mpya ya umoja wa kitaifa ili kusimamia uchaguzi uliocheleweshwa kwa muda mrefu, na hivyo kuzidisha mzozo kati yake na serikali yenye makao yake makuu mjini Tripoli hasa kwa vile Aquila Saleh amemtaka Waziri Mkuu wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, ajiuzulu.
-
Kipindupindu chaua watu zaidi ya 170 ndani ya wiki moja Sudan
May 28, 2025 06:55Zaidi ya watu 170 wameripotiwa kufariki dunia kutokana na ugonjwa wa kipindupindu ndani ya wiki moja katika nchi ya Sudan iliyogubikwa na mapigano kwa zaidi ya miaka miwili sasa.
-
WFP: Watu milioni kumi wakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula DRC
May 28, 2025 02:09Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limesema kuwa, watu milioni 28 sasa wanakabiliwa na njaa kali katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
-
Lavrov: Russia ni mshirika wa kuaminika kwa Afrika katika kuimarisha mamlaka
May 27, 2025 11:52Sergey Lavrov, Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema Moscow imebaki kuwa mshirika wa kweli na wa kuaminika kwa mataifa ya Afrika kwa kusaidia juhudi za kuimarisha mamlaka zao, ambazo zinatishiwa na aina za kisasa za ukoloni.