-
Marais wa DRC na Rwanda wasaini makubaliano chini ya upatanishi wa US huku mapigano yakiendelea
Dec 05, 2025 07:10Rais wa Marekani Donald Trump amewasifu marais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Rwanda kwa kile alichokiita "ujasiri" wao wa kusaini makubaliano mapya yanayolenga kukomesha mzozo wa muda mrefu mashariki mwa Kongo DR na kufungua njia ya kuchotwa rasilimali muhimu za madini katika eneo hilo na Marekani na makampuni ya Kimarekani.
-
UN: Kuna hatari ya kuzuka wimbi jipya la mashambulizi na janga la kibinadamu Kordofan, Sudan
Dec 05, 2025 02:57Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, ametoa indhari kuhusu hatari ya kuzuka wimbi jipya la ukatili katika eneo la Kordofan, Sudan, baada ya kushadidi mapigano kati ya Jeshi la Sudan (SAF), Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF) na Kundi la Harakati ya Kaskazini ya Ukombozi wa Wananchi wa Sudan, (SPLM-N).
-
Wasomali wamjia juu Trump baada ya kuwaita "takataka", na kwamba nchi yao "inanuka"
Dec 05, 2025 02:36Matamshi ya dharau yaliyotolewa na Rais wa Marekani, Donald Trump, kuhusu watu na nchi ya Somalia yamesababisha wimbi la hasira na majibu makali.
-
Amnesty yataka uchunguzi wa uhalifu wa kivita wa RSF nchini Sudan.
Dec 04, 2025 12:14Shirika la kutetea haki za binadamu Amnesty International limetaka kufanyike uchunguzi wa uhalifu wa kivita kuhusu shambulio lililofanywa na kundi la waasi la Rapid Support Forces (RSF) nchini Sudan katika kambi ya wakimbizi wa ndani ya Zamzam, jimbo la Darfur Kaskazini, mapema mwaka huu.
-
Waziri Mkuu wa Somalia akosoa kauli za dharau za Trump kuhusu Somalia na wahamiaji wa Kisomali
Dec 04, 2025 12:05Waziri Mkuu wa Somalia, Hamza Abdi Barre, siku ya Jumatano alikosoa matamshi ya Rais wa Marekani Donald Trump yaliyolenga Somalia na wahamiaji wa Kisomali walioko Marekani.
-
Ethiopia yapinga madai ya 'kikoloni' ya Misri huku mzozo wa bwawa la Nile ukiongezeka
Dec 04, 2025 07:46Ethiopia jana iliikosoa vikali Misri na kuituhumu nchi hiyo kwa kuyumbisha utulivu wa eneo la Pembe ya Afrika ili kudumisha ukiritimba wa kikoloni mwa Mto Nile.
-
Wabunge Kenya wawatuhutumu wanajeshi wa Uingereza kwa unyanyasaji wa kingono na uharibifu wa mazingira
Dec 04, 2025 03:49Ripoti ya uchunguzi ya bunge la Kenya imewatuhumu wanajeshi wa Uingereza walioko nchini humo kwa unyanyasaji wa mara kwa mara wa kingono, mazoezi yasiyo salama na ukiukaji wa mazingira. Ripoti hiyo imebainisha kuwa mienenendo hiyo imewafanya wanajeshi hao ajinabi kujiona kama "kikosi vamizi".
-
Madaktari Sudan watahadharisha kuhusu hatima ya watoto na wanawake waliokwama Kordofan magharibi
Dec 04, 2025 03:48Kundi la madaktari wa Sudan limesema kuwa lina wasiwasi mkubwa kuhusu hatima ya makumi ya watoto na wanawake katika mji wa Babnousa huko Kordofan Magharibi, baada ya mapigano kati ya jeshi la Sudan na wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF).
-
Uchaguzi Uganda: UN yalaani ukandamizaji dhidi ya mgombea urais wa upinzani
Dec 04, 2025 03:47Umoja wa Mataifa jana Jumatano ulikosoa kuongezeka ukandamizaji dhidi ya upinzani na vyombo vya habari nchini Uganda kabla ya uchaguzi mkuu wa mwezi ujao, na kutaka uchunguzi ufanyike bila upendeleo kuhusu madai ya kukamatwa raia kiholela, kutoweka na "mateso".
-
Gabon inamshikilia Waziri wake wa utalii kwa madai ya ufisadi wa dola milioni 18
Dec 04, 2025 03:44Pascal Ogowé Siffon Waziri wa Utalii wa Gabon amewekwa katika kifungo cha nyumbani baada ya kukamatwa. Hatua hii imechukuliwa baada ya Waziri huyo wa Utalii wa Gabon kujaribu kuondoka Libreville.