-
Waafrika wazidi kuonesha ubinadamu, wampa tunzo maalumu Yahya Sinwar
May 28, 2025 10:47Waafrika kwa mara nyingine wameonesha hisia zao za kuthamini ubinadamu kwa kuenzi nafasi muhimu ya wanamapambano wa Palestina. Tuzo ya ya kila mwaka ya "Kwame Tour" kwa mwaka huu 2025 amepewa kiongozi wa Palestina shujaa shahid Yahya Sinwar (Abu Ibrahim) wakati wa sherehe za kuadhimisha Siku ya Uhuru wa Afrika.
-
Mgogoro wa kibinadamu Sudan unazidi kuongezeka, mapigano yanaendelea
May 28, 2025 10:46Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) imesema kuwa mgogoro wa kibinadamu nchini Sudan unazidi kuongezeka huku mapigano yakiendelea, watu wanazidi kuhama makazi yao na udharura wa kuchukuliwa hatua za kiafya umezidi kuwa mkubwa.
-
Spika wa Bunge la Mashariki Libya atoa mwito wa umoja wa kitaifa
May 28, 2025 10:46Spika wa Bunge lenye makao yake mashariki mwa Libya, Aguila Saleh ametoa mwito wa kuundwa serikali mpya ya umoja wa kitaifa ili kusimamia uchaguzi uliocheleweshwa kwa muda mrefu, na hivyo kuzidisha mzozo kati yake na serikali yenye makao yake makuu mjini Tripoli hasa kwa vile Aquila Saleh amemtaka Waziri Mkuu wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, ajiuzulu.
-
Kipindupindu chaua watu zaidi ya 170 ndani ya wiki moja Sudan
May 28, 2025 06:55Zaidi ya watu 170 wameripotiwa kufariki dunia kutokana na ugonjwa wa kipindupindu ndani ya wiki moja katika nchi ya Sudan iliyogubikwa na mapigano kwa zaidi ya miaka miwili sasa.
-
WFP: Watu milioni kumi wakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula DRC
May 28, 2025 02:09Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limesema kuwa, watu milioni 28 sasa wanakabiliwa na njaa kali katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
-
Lavrov: Russia ni mshirika wa kuaminika kwa Afrika katika kuimarisha mamlaka
May 27, 2025 11:52Sergey Lavrov, Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema Moscow imebaki kuwa mshirika wa kweli na wa kuaminika kwa mataifa ya Afrika kwa kusaidia juhudi za kuimarisha mamlaka zao, ambazo zinatishiwa na aina za kisasa za ukoloni.
-
Ghana: Afrika ipo tayari kushirikiana na Russia kuunda mustakabali wa kimataifa
May 27, 2025 07:05Mbunge wa Ghana amesema Afrika iko tayari kuwa nguvu muhimu katika maendeleo ya kimataifa, akikaribisha uhusiano unaozidi kustawi wa bara hilo na Russia, alioutaja kama njia ya maendeleo endelevu.
-
Kenya yasimama na Morocco mgogoro wa Sahara Magharibi
May 27, 2025 06:33Kenya imesema inaunga mkono mpango wa Morocco wa kulipa eneo linalozozaniwa la Sahara Magharibi uhuru wa kujitawala chini ya mamlaka ya utawala wa kifalme wa nchi hiyo ya Afrika Kaskazini, ikiungana na idadi inayoongezeka ya nchi za Kiafrika, Kiarabu na Magharibi ambazo zimeelekeza uungaji mkono wao kwa Rabat katika mzozo huo wa miongo mitano.
-
Rais wa zamani wa DRC Joseph Kabila awasili Goma
May 27, 2025 02:55Joseph Kabila Rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo amewasili katika mji wa Goma wa mashariki mwa nchi hiyo licha ya kutuhumiwa kushirikiana na makundi ya waasi.
-
Afrika Kusini yaadhimisha Siku ya Afrika kwa mwito wa umoja na ushirikiano
May 26, 2025 10:22Afrika Kusini jana Jumapili iliadhimisha Siku ya Afrika kwa mwito wa kusisitizia umoja na ushirikiano wa kikanda na mshikamano wa kiutamaduni kwenye bara zima.