-
Milio ya risasi yasikika katika mji mkuu wa Niger, Niamey
Jun 18, 2026 10:06Milio ya risasi imesikika mapema leo Alkhamisi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Diori Hamani mjini Niamey, nchini Niger, miezi kadhaa baada ya shambulio kubwa la waasi katika eneo hilo hilo.
-
Afisa wa Yemen: Majeshi ya Iran ni mfano wa kuigwa katika ulimwengu wa Kiislamu
Jun 17, 2026 12:06Mkuu wa Baraza Kuu la Kisiasa la Yemen, Mahdi al Mashat, amesifu Majeshi ya Iran, hasa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), akisema utendaji wao wakati wa vita vya Marekani na Israel umeonyesha ustahimilivu, azma thabiti, na nguvu ya kijeshi.
-
Viongozi wa Afrika waunga mkono mpango wa dola milioni 518 kukabiliana na kuenea kwa Ebola
Jun 17, 2026 12:04Viongozi wa Afrika siku ya Jumanne walikutana katika mkutano wa dharura wa ngazi ya juu uliofanyika kwa njia ya mtandao, kwa lengo la kutafuta ufadhili wa dola milioni 518 za kudhibiti mlipuko wa Ebola unaoendelea huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Uganda.
-
Somalia yabainisha wasiwasi kufuatia uhusiano kati ya "Israel" na "Somaliland"
Jun 17, 2026 12:01Serikali ya Somalia imetoa wito kwa jamii ya kimataifa kuheshimu sheria za kimataifa, kutambua mamlaka yake ya kitaifa, na kulaani hatua zozote zinazodhoofisha umoja na uthabiti wa taifa hilo.
-
Huenda mlipuko wa Ebola nchini DRC ukadumu kwa mwaka mmoja
Jun 17, 2026 03:18Imebainika kuwa mlipuko wa ugonjwa hatari wa Ebola unaoendelea kuenea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) bado haujafikia kilele chake, na huenda ukadumu kwa takriban mwaka mmoja.
-
Jeshi la Jamhuri ya Afrika ya Kati lakanusha uvumi kuhusu njama ya mapinduzi
Jun 17, 2026 03:13Jeshi la Jamhuri ya Afrika ya Kati limekanusha taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa kuna njama ya kutaka kuipindua serikali, na kusisitiza kuwa nchi hiyo ina utulivu wa kutosha, na kwamba taasisi za serikali zinafanya kazi kama kawaida.
-
Kesi inayomkabili wa Rais wa zamani wa CAR yaanza kusikilizwa bila ya yeye kuwepo mahakamani
Jun 16, 2026 11:06Kesi inayomkabili aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Francois Bozize, imeanza kusikilizwa katika Mahakama Maalumu inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa katika mji mkuu wa nchi hiyo Bangui.
-
Nigeria: Karibu wapiganaji 10,000 wa zamani wa Boko Haram waunganishwa katika jamii
Jun 16, 2026 11:00Mamlaka husika katika Jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa Nigeria zimearifu kuwa karibu wapiganaji 10,000 wa zamani wa kundi la waamgambo wa Boko Haram sasa wameunganishwa tena katika jamii chini ya mpango unaofadhiliwa na serikali wa kurekebisha tabia na kuhimiza kuachana na makundi ya uasi.
-
Serikali ya Afrika Kusini yasema imewarejesha nyumbani wageni 2,745 ndani ya wiki moja
Jun 15, 2026 12:20Afrika Kusini imewarejesha nyumbani wageni 2,745 katika wiki moja baada ya Rais Cyril Ramaphosa kuapa kuchukua hatua kali dhidi ya uhamiaji haramu.
-
Sudan: RSF inafanya biashara haramu ya viungo vya binadamu
Jun 15, 2026 04:24Serikali ya Sudan imelituhumu kundi la Rapid Support Forces (RSF) kuwa linaendesha mtandao wa biashara haramu ya viungo vya binadamu ndani ya magereza ya Daqris na Shala huko El Fasher, mji mkuu wa jimbo la Darfur Kusini, ambalo kwa mujibu wa makadirio ya serikali ya Khartoum, lina wafungwa karibu 20,000 wa kijeshi na raia.