-
Ripoti ya Umoja wa Mataifa yafichua: Afrika imeipiku Asia kama kitovu cha njaa duniani
Jul 22, 2026 03:20Mkuu wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) wenye makao yake makuu huko Roma ameonya kuwa, migogoro na machafuko katika masoko ya nishati duniani vinaweza kuwasukuma mamilioni zaidi ya watu kwenye njaa kwa kuzidisha gharama za mafuta, mbolea na chakula. Taarifa hii imetolewa huku ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa ikionyesha kuwa maendeleo ya kimataifa dhidi ya njaa bado yako tete.
-
Misri yaishutumu Ethiopia kuwa inasimamia Bwawa la Grand Ethiopian Renaissance kwa "njia ya kisiasa"
Jul 22, 2026 03:03Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, Badr Abdelatty ameituhumu Ethiopia kuwa inasimamia Bwawa Kuu la Renaissance (GERD) kwenye Mto Nile "kwa njia ya kisiasa" kupitia hatua za upande mmoja dhidi ya Misri na Sudan.
-
Upinzani Cameroon wataka kuchukuliwe hatua ya kikatiba na kutangazwa nafasi wazi ya urais
Jul 22, 2026 03:01Kutokuwepo nchini kwa muda mrefu Rais wa Cameroon, Paul Biya, kunasababisha utata mkubwa nchini humo, zaidi ya siku 44 baada ya kuondoka nchini Juni 7, 2026, katika safari iliyoelezwa rasmi kama "kukaa kwa muda mfupi faraghani barani Ulaya," bila ya kurudi nyumbani hadi sasa.
-
UN: Wakimbizi 144 wamefariki au kutoweka pwani ya Mauritania wakijaribu kufika Ulaya
Jul 21, 2026 11:21Wakala wa Umoja wa Mataifa wa Wakimbizi (UNHCR) umetangaza kuwa watu 144 wameripotiwa kufariki dunia au kutoweka katika pwani ya Mauritania walipokuwa wakijaribu kuelwkea Ulaya.
-
Wanaharakati Kenya waituhumu serikali kwa kupuuza amri ya mahakama
Jul 21, 2026 03:31Wanaharakati nchini Kenya wamezituhumu mamlaka za nchi hiyo kwa kukiuka amri ya mahakama iliyozuia kuanzishwa kituo cha karantini kwa wagonjwa wa Ebola
-
Makumi ya watu wanahofiwa kupoteza maisha baada ya boti kupinduka na kuzama Nigeria
Jul 21, 2026 02:57Wafanyakazi wa huduma za uokoaji kaskazini-magharibi mwa Nigeria jana waliendelea kuwatafuta manusura baada ya boti iliyokuwa imebeba watu kadhaa kupinduka na kuzama katika jimbo la Jigawa.
-
Idadi ya waliofariki dunia kwa Ebola DRC yapindukia 900
Jul 20, 2026 11:08Takribani watu 930 wamefariki dunia kutokana na ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Hiyo ni kwa mujibu wa Wizara ya Afya nchini humo.
-
Maelfu waandamana kupinga usajili vitani kwa vijana Tigray
Jul 20, 2026 03:59Maelfu ya watu walikusanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia, kushiriki maandamano ya kuunga mkono serikali na kupinga madai ya kampeni ya mamlaka katika eneo la Tigray kuwasajili kwa lazima vijana kupigana vitani.
-
Raia 114 wauawa mashariki mwa Kongo mwezi Juni
Jul 19, 2026 12:44Waasi wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo mwezi uliopita waliwauwa watu wasiopungua 114 kuwatekanyara wengine 17. Haya yameelezwa Shirika la Ufuatiliaji Usalama la Kivu Security Tracker.
-
Tunisia inakabiliwa na joto kali huku viwango vya joto vikikaribia nyuzi joto 50
Jul 19, 2026 12:40Wimbi kali la joto lisilo la kawaida limeikumba Tunisia, na kusababisha viwango vya joto kupanda hadi karibu nyuzi joto 50 Selsiasi na kuvunja rekodi za kihistoria katika maeneo kadhaa nchini humo.