-
AU yahimiza kuchukuliwa hatua madhubuti za kudhamini chakula Afrika
Oct 26, 2025 12:00Kamishna wa Kilimo, Maendeleo Vijijini, Uchumi wa Bluu na Mazingira Endelevu wa Umoja wa Afrika (AU), Moses Vilakati ametaka kuchukuliwe juhudi zaidi na zilizoratibiwa vyema kwenye bara zima la Afrika ili kushughulikia changamoto kubwa za usalama wa chakula barani humo.
-
Zimbabwe yatoa mwito wa kuondolewa vikwazo vya Magharibi bila ya masharti
Oct 26, 2025 11:59Jana Zimbabwe ilifanya maadhimisho ya Siku ya Kikanda ya Kupinga Vikwazo huko Harare, mji mkuu wa nchi hiyo. Wananchi wa Zimbwe wametaka kuondolewa vikwazo vya nchi za Magharibi bila ya masharti na kuruhusiwa taifa lao kufanikisha malengo yake ya ustawi wa kiuchumi.
-
Jeshi la Sudan lapambana na waasi wa RSF katika miji ya el-Fasher na Bara
Oct 26, 2025 08:05Mapigano yamezidi kushadidi maeneo kadhaa ya Sudan baada ya waasi wa RSF kuendeleza mashambulizi dhidi ya mji wa el-Fasher ulioko Kaskazini mwa Darfur, pamoja na mji wa Bara katika mkoa wa Kordofan Kaskazini.
-
Ethiopia na Somalia zaahidi amani katika eneo wakati wa Jukwaa la 11 la Tana
Oct 26, 2025 08:03Ethiopia na Somalia zimeithibitishia dunia dhamira yao ya kudumisha amani ya kikanda wakati wa Jukwaa la 11 la Tana ambalo limejadili jukumu la kimkakati la Pembe ya Afrika.
-
Kufanyishwa kazi watoto Sudan Kusini kwafikia viwango vya kutisha
Oct 26, 2025 04:44Ripoti iliyotolewa na serikali ya Sudan Kusini kwa ushirikiano na Save the Children imefichua kwamba takriban 64% ya watoto wa Sudan Kusini wenye umri wa kati ya miaka 5 na 17 wanahusika katika aina mbaya zaidi za ajira kwa watoto, ikiwa ni pamoja na ajira ya kulazimishwa, ukatili wa kingono, wizi, na kuhusika katika migogoro ya silaha.
-
Serikali ya Tanzania yasikitishwa na ripoti ya Amnesty International kuhusu madai ya kukandamiza haki za binadamu
Oct 26, 2025 04:09Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeeleza kusikitishwa kwake na chapisho la shirika la Amnesty International lenye kichwa cha habari 'Wimbi la Ugaidi' Laikumba Tanzania Kabla ya Kura ya 2025".
-
Madagascar yamvua uraia aliyekuwa rais wa nchi hiyo Rajoelina
Oct 25, 2025 14:51Rais wa zamani wa Madagascar, Andry Rajoelina, amevuliwa uraia wake baada ya kuikimbia nchi hiyo mapema mwezi huu kufuatia maandamano makubwa yaliyoongozwa na vijana dhidi ya utawala wake.
-
Rais wa Nigeria ateua makamanda wapya wa kijeshi baada ya njama ya mapinduzi
Oct 25, 2025 12:50Rais wa Nigeria, Bola Tinubu, ameteua makamanda wapya wa kijeshi Ijumaa katika mabadiliko makubwa, wiki chache baada ya maafisa 16 wa kijeshi kukamatwa kwa tuhuma za kupanga mapinduzi ya kijeshi, hatua iliyosababisha pia mamlaka kufuta sherehe za Siku ya Uhuru za nchi hiyo zilizopangwa kufanyika Oktoba 1.
-
Watu wa Ivory Coast washiriki katika uchaguzi wa urais huku kukiwa na mvutano wa kisiasa
Oct 25, 2025 12:46Wapiga kura nchini Ivory Coast wamejitokeza leo Jumamosi kushiriki katika uchaguzi wa urais, wakati mvutano wa kisiasa ukiendelea kutawala hali ya taifa.
-
Zaidi ya watu milioni 30 wanahitaji misaada ya kibinadamu Sudan
Oct 25, 2025 05:20Sudan imekumbwa na moja ya mambo ya dharura mno ya kibinadamu duniani. Zaidi ya watu milioni 30 wanahitaji msaada wa kibinadamu, ikiwa ni pamoja na zaidi ya watu milioni 9.6 wakimbizi wa ndani wakiwemo karibu watoto milioni 15.