Zaidi ya wafungwa 100 wametoroka jela baada ya mvua kali kubomoa ukuta mbovu wa jela hiyo iliyoko karibu na mji mkuu wa Nigeria Abuja.
Kassim Majaliwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alisema jana Alhamisi kuwa takriban watu 155 wamefariki dunia nchini humo kutokana na mvua kubwa inayoambatana na El Nino na hivyo kusababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi.
Jeshi la Burkina Faso limewauwa kiholela raia 223, wakiwemo watoto wachanga kadhaa na watoto wengine wengi, katika mashambulizi dhidi ya vijiji viwili vinavyotuhumiwa kushirikiana na wanamgambo wenye silaha. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya shirika la Human Rights Watch iliyotolewa jana Alhamisi.
Mjumbe Maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa Kanda ya Maziwa Makuu amewasilisha kwa Baraza la Usalama taswira ya kutisha ya hali ya Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC, inayoambatana na mvutano unaoendelea kati ya nchi hiyo na Rwanda, na hatari ya mzozo huo kusambaa kikanda.
Takriban watu 32 wamefariki dunia nchini Kenya na wawili hawajulikani walipo baada ya mafuriko kukumba karibu nusu ya taifa hilo la Afrika Mashariki. Watu 103,500 wanaripotiwa kuathiriwa na janga la mafuriko nchini Keya huku mvua zikiripotiwa kuendelea nchini humo.
Jamhuri ya Kongo imetangaza janga la homa ya MPOX, ugonjwa unaosababishwa na virusi vya monkeypox, baada ya kesi 19 kuthibitishwa katika mikoa mitano, ikiwa ni pamoja na mji mkuu, Brazzaville.
Waangalizi wa mambo wanahofia kuwa eneo la Darfur magharibi mwa Sudan litaingia kwenye machafuko na vita vya wenyewe kwa wenyewe baada ya gavana wa eneo hilo na mkuu wa Harakati ya Ukombozi wa Sudan, Minni Arko Minawi, kuwatuhumu wapiganaji wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) kuwa wanapanga kuunda serikali katika eneo hilo baada ya kabila la Zaghawa kutangaza kujiunga na jeshi la Sudan dhidi ya RSF.
Kwa akali miili 21 imeopolewa kufuatia ajali ya boti katikak pwani ya Djibouti.
Baada ya kugonga mwamba mazungumzo ya kisiasa ya Marekani ya kudumisha uwepo wake wa kijeshi nchini Niger, kwa mara nyingine tena raia katika nchi hiyo ya Kiafrika wametoa mwito wa kuondoka kwa wanajeshi wa Marekani katika nchi yao kwa kufanya maandamano mbele ya kambi ya kijeshi ya Marekani kaskazini mwa Niger.
Umoja wa Mataifa umefichua kuwa zaidi ya watu 50,000 wamekimbia makazi yao kaskazini mwa Ethiopia, kutokana na mapigano yanayojiri katika eneo linalozozaniwa kati ya majimbo ya Tigray na Amhara. Mapigano ya pande hizo mbilii yamezua wasiwasi wa kimataifa.