-
Jenerali Mousavi: Mapambano dhidi ya Iran yatakuwa funzo kwa Trump
Feb 16, 2026 03:32Mkuu wa Kamandi ya Majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa Donald Trump anapaswa kufahamu kwamba kuingia katika mapambano ya kijeshi na Iran kutakuwa funzo lenye athari kubwa, ambalo matokeo yake yatamzuia kufanya vitisho na majigambo kwenye jukwaa la kimataifa.
-
Iran yaingia kwenye klabu ya mataifa yenye bidhaa za juu za tiba ya seli
Feb 16, 2026 02:59Taasisi ya Utafiti ya Royan Research ya Iran imezindua bidhaa sita mpya zilizotengenezwa ndani ya nchi katika nyanja ya tiba ya seli na uhandisi wa tishu, hatua inayoiweka Iran miongoni mwa mataifa yanayozalisha bidhaa za kisasa za tiba zinazojulikana kama Advanced Therapy Medicinal Products (ATMPs).
-
Sheikh Maher Hammoud: Uvamizi wa kijeshi dhidi ya Iran utawasha moto Asia Magharibi
Feb 15, 2026 12:17Mkuu wa Umoja wa Kimataifa wa Maulamaa wa Muqawama amesema kuwa, uchokozi wowote mpya dhidi ya Iran utapelekea kuwaka moto katika eneo lote la Asia Magharibi.
-
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Iran: Mpira uko kwenye uwanja wa Marekani kuthibitisha azma ya kufikia makubaliano ya nyuklia
Feb 15, 2026 10:56Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayehusika na masuala ya kisiasa amesema ni zamu ya Marekani kuonyesha azma ya kufikia makubaliano yanayolenga kutatua suala la nyuklia la Tehran.
-
Araqchi: Sarakasi ya Munich dhidi ya Iran imedhihirisha namna Ulaya ilivyopoteza ushawishi wake wa kijiopolitiki
Feb 15, 2026 08:00Abbas Araqchi Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa Mkutano wa Usalama wa Munich uliokua na mtazamo dhidi ya Iran umegeuka na kuwa kongamano la sakarakasi na hivyo kudhihirisha namna Ulaya ilivyopoteza ushawishi wake wa kijiopolitiki na umuhimu wa kistratejia.
-
Baqaei: Mashinikizo ya kisiasa hayawezi kudhoofisha haki ya Iran ya kurutubisha urani
Feb 15, 2026 07:58Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa haki "isiyoweza kubatilishwa" ya Iran ya kurutubisha madini ya urani haiwezi kudhoofishwa na mashinikizo ya kisiasa.
-
Rais Pezeshkian: Nchi za eneo zinaweza kutatua matatizo yao bila kusimamiwa
Feb 15, 2026 03:27Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kwamba kuanzisha amani na utulivu ndiyo "njia ya maisha kwa sayari hii ndogo," akisisitiza kuwa nchi za eneo zinaweza kutatua matatizo yao bila kusimamiwa na kwamba, hakuna nchi itakayofaidika na vita, migogoro, vurugu, na umwagaji damu.
-
Tehran yahimiza marekebisho 'makubwa' katika mbinu 'zisizojenga' za EU
Feb 14, 2026 06:47Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi, amesema Umoja wa Ulaya unahitajika kufanya marekebisho makubwa katika mbinu zake "zisizo za kujenga" kuhusu Tehran.
-
Kwa nini Grossi amekiri haki ya Iran ya kurutubisha urani?
Feb 13, 2026 11:21Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) amekiri kwamba, Iran kama nchi iliyotia saini Mkataba wa Kuzuia Uenezaji wa Silaha za Nyuklia (NPT), ina haki ya kurutubisha urani.
-
Khatibu wa Sala ya Ijumaa Tehran: Nchi tatu za Ulaya zilishiriki katika ghasia za Iran
Feb 13, 2026 10:49Khatibu wa muda wa Sala ya Ijumaa mjini Tehran amesema kuwa nchi tatu za Ulaya, yaani Uingereza, Ufaransa, na Ujerumani, zimehusika katika uchochezi na machafuko ya karibuni dhidi ya Iran. Amesema kwamba, kwa mtazamo wa wananchi wa Iran, nchi hizo zimeshirikiana na watenda jinai wakuu katika machafuko hayo.