-
Tume ya Uchunguzi ya Umoja wa Mataifa: Marekani imetenda uhalifu wa kivita nchini Iran
Sep 18, 2026 03:54Tume ya Kutafuta Ukweli ya Umoja wa Mataifa imetangaza kwamba, baada ya kufanya uchunguzi na kuchambua ushahidi, imefikia hitimisho kwamba mashambulizi ya Marekani dhidi ya Minab na Lamerd yalikuwa ni uhalifu wa kivita.
-
Baghaei ajibu madai ya Saudi Arabia kuhusu kushambuliwa mji mtakatifu wa Makka
Sep 18, 2026 03:52Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, madai ya kuzuia ndege isiyo na rubani iliyokuwa ikielekea katika mji mtakatifu wa Makka hayawezi kuwa msingi wa kuutuhumu upande wowote.
-
Iran yajibu mapigo, yamtimua mwanadiplomasia wa Sweden
Sep 18, 2026 03:50Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, sanjari na kukanusha madai ya Sweden dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu, imempa mwanadiplomasia wa nchi hiyo aliyeko Tehran muda wa saa 48 kuondoka nchini, ikiwa ni hatua ya kulipiza kisasi kwa uamuzi wa Stockholm wa kukataa kumruhusu mwanadiplomasia wa Iran kuendelea na shughuli zake.
-
Araghchi: Mashauriano ya Beijing yamefanikiwa; Iran yathamini “ushirikiano wa kimkakati” na China
Sep 17, 2026 12:09Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, ameelezea mashauriano yake mjini Beijing kama “yaliyofanikiwa,” akizungumzia maudhui ya safari yake katika mji mkuu huo wa China, ambapo alikutana na mwenzake, Wang Yi.
-
Kamanda wa IRGC: Iran itajibu vikali kosa lolote la kimahesabu la adui
Sep 17, 2026 10:59Kamanda wa Kikosi cha Nchi Kavu cha Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) ameonya kuwa kitendo chochote cha uchokozi kutoka kwa adui kitakabiliwa na jibu kali na thabiti kutoka kwa vikosi vya ulinzi vya Iran.
-
Waziri wa Sayansi wa Iran atahadharisha kuhusu hatari ya Akili Mnemba kuwa "udikteta usioonekana"
Sep 17, 2026 02:49Waziri wa Sayansi, Utafiti na Teknolojia wa Iran, akitoa tahadhari kuhusu madhara ya ufuatiliaji mpana unaotumia Akili Mnemba amesema, hali hiyo inaweza kuweka mazingira ya kubadilisha udhibiti wa data kuwa udhibiti wa watu na hatimaye kusababisha kuibuka “udikteta usioonekana.”
-
Meja Jenerali Amir Hatami: Nguvu halisi ya Iran ni umoja na azma ya wananchi
Sep 16, 2026 12:13Meja Jenerali Amir Hatami Kamanda Mkuu wa Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika ujumbe wake wa kupongeza siku 200 za uwepo wa kishujaa wa wananchi wa Iran na kusisitiza kwamba uwepo huo ni dhihirisho la kudumu la imani, mshikamano na azma ya kitaifa, pamoja na kuwa kielelezo cha nguvu na uimara wa ndani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
China: Tuko tayari kutetea kwa nguvu haki za Iran
Sep 16, 2026 12:10Waziri wa Mambo ya Nje wa China amesema kuwa uhusiano na ushirikiano wa nchi yake na Iran ni wa kimkakati na kwamba Beijing inatangaza rasmi kwamba iko tayari kuimarisha mazungumzo na ushirikiano na Iran, na kutetea kwa dhati haki na maslahi halali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Pakistan: Makubaliano yetu na Saudia hayatoathiri uhusiano wetu na Iran
Sep 16, 2026 12:00Msemaji wa Jeshi la Pakistan amesema kuwa makubaliano ya kijeshi ya nchi yake na Saudi Arabia pamoja na Uturuki maarufu kwa jina la Makubaliano ya Makka, hayatoathiri uhusiano wa Tehran na Islamabad.
-
Iran yashika nafasi ya tatu duniani katika kutibu ugumba, yakamilisha mpango wa chanjo
Sep 16, 2026 02:56Mkuu wa Shirika la Madaktari la Iran amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu imeshika nafasi ya kwanza duniani katika utoaji wa chanjo na nafasi ya tatu duniani katika kutibuu tatizo la ugumba.