-
Mkutano wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu waanza mjini Tehran
Aug 27, 2026 12:02Mkutano wa 40 wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu umeanza mjini Tehran, ukijikita zaidi kwenye maono ya Kiongozi marehemu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Shahidi Sayyid Ali Khamenei kuhusu kuimarisha umoja katika Ulimwengu wa Kiislamu.
-
Iran yapendekeza 'mkataba wa usalama wa pande zote' miongoni mwa mataifa ya Kiislamu
Aug 27, 2026 11:59Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amependekeza "mkataba wa usalama wa pande zote na kutokuchokozana" miongoni mwa nchi za Kiislamu ili kulinda usalama wa kikanda, hasa katika kipindi hiki ambapo Marekani na Israel zinaendeleza uchokozi wao katika eneo la Asia Magharibi.
-
Kwa nini vita vya kiuchumi vya Trump dhidi ya Iran vinaiathiri Marekani yenyewe?
Aug 27, 2026 06:06Mohammad Bagher Ghalibaf, Spika wa Bunge la Iran, amefananisha mpango mpya wa Marekani wa kutoa mashinikizo ya kiuchumi dhidi ya Iran na 'boomerang,' ambacho ni kifaa cha kurushwa ambacho humrudia aliyekirusha, kwa maana kuwa utawadhuru tu waasisi wake wenyewe.
-
Pezeshkian: Marekani haitapata chochote kupitia mashinikizo ya kiuchumi dhidi ya Iran
Aug 27, 2026 04:32Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa Marekani haitaweza kufanikisha lolote kupitia mashinikizo ya kiuchumi, akisisitiza kuwa Iran itaendelea kusimama imara.
-
Iran yataka UN na nchi wanachama zikatae “ugaidi wa kiuchumi” wa Marekani
Aug 27, 2026 04:28Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi, amelitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na nchi wanachama wa umoja huo kukataa kampeni mpya ya Marekani ya ugaidi wa kiuchumi dhidi ya Iran, akisema Washington inalenga kuzilazimisha nchi nyingine kuacha mahusiano halali ya kiuchumi na Tehran kwa kutumia vitisho vya vikwazo.
-
Kamanda wa Kikosi cha Ulinzi wa Anga cha Jeshi la Iran: Iran kupanua kwa mafanikio mifumo ya ulinzi
Aug 27, 2026 04:24Kamanda wa Kikosi cha Ulinzi wa Anga cha Jeshi la Iran amesema kuwa Iran inapiga hatua mbele kwa kutegemea kikamilifu uwezo wake wa ndani, ikipanua mifumo yake ya ulinzi wa anga na kuzalisha nakala za mifumo ile iliyofanya vyema wakati wa vita vya siku 40.
-
Iran yafafanua ilivyokubaliana na Oman kuhusu utaratibu wa muda utakaotumika kwenye Mlango-Bahari wa Hormuz
Aug 26, 2026 11:22Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran wa masuala ya sheria na kimataifa ametoa ufafanuzi kuhusu makubaliano ya muda yaliyofikiwa kati ya Jamhuri ya Kiislamu na Oman kuhusu Mlango-Bahari wa Hormuz, akisisitiza kwamba, kufunguliwa tena kwa njia hiyo ya majini kunategemea kutekelezwa kwa matakwa ya Tehran.
-
Pezeshkian: Kuimarisha mshikamano wa nchi za Kiislamu ni jambo la msingi katika kudumisha utulivu
Aug 26, 2026 03:33Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameonya kwamba maadui, wenye tamaa ya utajiri na rasilimali za eneo la Magharibi mwa Asia, wanataka kuibua hitilafu, vita na migogoro ili kunyakua utajiri huo, na njia pekee ya kukabiliana nao ni kudumisha umakini na umoja miongoni mwa mataifa ya Waislamu.
-
Taasisi ya Royan ya Iran ni miongoni mwa vituo 10 bora duniani vya tiba ya uzazi
Aug 26, 2026 03:22Kwa mujibu wa takwimu za SCImago; Taasisi ya Royan ya Iran ni miongoni mwa vituo 10 bora duniani katika nyanja ya tiba ya uzazi. Haya yameelezwa na Naibu Mkuu wa taasisi hiyo anayesimamia masuala ya utafiti.
-
Kwa nini sera ya Marekani ya "mashinikizo ya juu zaidi" ni marudio ya mkakati uliofeli?
Aug 25, 2026 10:17Richard Nephew, mmoja wa wabunifu wakuu wa mfumo wa vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran, amekosoa mbinu ya sasa ya Washington, akisema sera ya "kuongeza mashinikizo ya kiuchumi" haina tija wala msingi mzuri wa kimkakati.