Apr 17, 2024 11:41
Hatua ya Iran kujitetea kihalali dhidi ya shambulio la kichokozi la utawala wa Kizayuni katika ubalozi mdogo wake nchini Syria, ambayo ilifanyika kwa utaratibu wa hali ya juu na kupitia silaha tofauti za mashambulio, imekuwa na athari na matokeo ya kieneo na kimataifa angalau imepelekea wakaazi wa Gaza kupata usiku mmoja wa amani na utulivu.