Iran
-
Nafasi ya juu ya kielimu ya Iran katika nchi za Kiislamu na dunia
Oct 01, 2023 02:37Makamu wa Rais katika Masuala ya Elimu na Teknolojia wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema: Katika kivuli cha siasa za kistratijia za Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi, hivi sasa Iran ya Kiislamu imebadilika na kuwa nchi mashuhuri kielimu na yenye wasomi wakubwa na mashirika muhimu ya kiteknolojia.
-
Raisi: Magharibi wana wasiwasi wa kukabiliwa na ustaarabu mpya
Sep 30, 2023 15:48Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika toleo la tano la Tuzo ya al Mustafa (SAW) kuwa sayansi na elimu yenye manufaa ni elimu inayosababisha saada na ufanisi kwa mwanadamu na kuongeza kuwa, tangu hapo awali, Wamagharibi walikuwa na wasiwasi kwamba kutajitokeza ustaarabu mpya wa kukabiliana nao, na hii ndiyo sababu kuu ya vita dhidi ya Uislamu (Islamophobia) na hujuma dhidi ya Iran (Iranophobia).
-
Iran yatangaza utayari wa kuimarisha uhusiano wake na Tanzania
Sep 30, 2023 07:31Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Hossein Amir-Abdollahian amesema, Jamhuri ya Kiislamu iko tayari kuimarisha uhusiano na maelewano ya pande mbili kati yake na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
-
Satelaiti ya Iran Nour 3, thibitisho la kushindwa vikwazo dhidi ya irada ya wanasayansi wa Iran
Sep 30, 2023 06:55Kupitia ujumbe, rais wa Iran amesema kurushwa katika anga za mbali satelaiti ya Iran Nour 3 kwa kutumia kombora la Qased la Iran ni thibitisho la msemo kwamba "sisi tunaweza" na wakati huo huo ni dhihirisho la kufeli vikwazo dhidi ya irada ya wanasayansi vijana wa Iran.
-
Rais wa Iran alaani mashambulizi pacha ya kigaidi Pakistan
Sep 30, 2023 04:46Rais Ebrahim Raisi wa Iran amelaani mashambulizi mawili ya kigaidi yaliuoua makumi ya watu katika jimbo la kusini magharibi la Balochistan nchini Pakistan.
-
Jeshi la Wanamaji la Iran kujenga kambi ya kudumu barani Antaktika
Sep 29, 2023 13:10Mkuu wa Jeshi la Wanamaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Admeri Shahram Irani amedokeza kuwa jeshi hilo lina mpango wa kujenga kituo cha kudumu katika bara la Antaktika, ikiwa ni pamoja na kuanzisha kituo cha kudumu cha harakati za kijeshi na kisayansi.
-
Khatibu wa Sala ya Ijumaa Tehran asisitiza kuhusu umoja wa Waislamu
Sep 29, 2023 13:10Khatibu wa Sala ya Ijumaa jijini Tehran amesisitiza umuhimu wa umoja wa Waislamu.
-
Ukumbusho na indhari ya Iran kwa UN kuhusu utambulisho na matokeo ya vitisho vya utawala wa Kizayuni
Sep 29, 2023 03:59Amir Saeid Iravani Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amewaandikia barua Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Mwenyekiti wa Baraza Kuu la UN na Rais wa Baraza la Usalama la umoja huo kuhusu matamshi ya vitisho ya karibuni ya waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni dhidi ya Iran.
-
Ghalibaf: Nchi za Afrika kwa Iran ni muhimu sana kama ilivyo kundi la BRICS
Sep 28, 2023 15:24Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema katika mazungumzo na wanaharakati na wabunge wa Afrika Kusini kwamba, Tehran inaamini kuwa, umuhimu wa nchi za Afrika hususan Afrika Kusini ni mkuubwa na ni sawa na umuhimu wa kundi la BRICS, kwa Iran.
-
Raisi: Kurushwa kwa mafanikio satalaiti "Nour 3" ni ishara nyingine ya kushindwa mradi wa vikwazo vya adui
Sep 28, 2023 07:52Rais wa Iran, Ebrahim Raisi, amepongeza kurushwa kwa mafanikio satalaiti Nour-3 katika obiti akikutaja kuwa ni ushindi wa taifa na ushahidi wa kushindwa mradi wa vikwazo na vitisho vya adui.