-
Iran yatangaza kufikiwa makubaliano ya kumaliza vita na Marekani
Jun 15, 2026 04:29Sekretarieti ya Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran (SNSC) imethibitisha kuwa Iran na Marekani zimekamilisha maandishi ya hati ya makubaliano (MoU) yanayolenga kumaliza vita, kusimamisha mara moja na kwa kudumu operesheni zote za kijeshi katika nyanja zote, ikiwemo Lebanon, na pia kuondoa mzingiro wa baharini uliowekwa na Marekani dhidi ya Iran.
-
Makumi ya magaidi, majasusi na wachochezi wa ghasia wamekamatwa wakati wa uvamizi wa Marekani na Israel dhidi ya Iran
Jun 15, 2026 04:20Wizara ya Intelijensia ya Iran imesema imefanikiwa kutekeleza operesheni za kupambana na ugaidi, ujasusi na hujuma nchini wakati wa uvamizi wa siku 39 wa Marekani na Israel ambao ulisitishwa mapema Aprili.
-
Jenerali wa IRGC: Iran inajitayarisha kujibu vitendo vya uchokozi
Jun 14, 2026 12:05Kamanda mwandamizi wa Jeshi la Iran laWalinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema vikosi vya ulinzi vya Iran viko tayari kikamilifu kukabiliana na hatua yoyote ya uadui, akionya maadui kwamba nchi hiyo iko tayari kutoa jibu la haraka kwa shambulio lolote.
-
Vita na Iran vimefichua vipi mwanzo wa kudhoofika nguvu ya kimkakati ya Marekani?
Jun 14, 2026 12:02Vita wakati mwingine huweka wazi washindi wake wa kweli na walioshindwa sio kwenye uwanja wa vita, bali katika vyumba vya kifikra na vituo vya kimkakati.
-
Shahidi Imam Khamenei kuzikwa katika Haram ya Imam Ridha (AS) tarehe 9 Julai
Jun 14, 2026 03:19Ofisi inayohusika na kuhifadhi na kuchapisha kazi za Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu imetangaza ratiba ya hafla za kuaga, mazishi, na kuzikwa kwa Shahidi Ayatullah Imam Sayyid Ali Khamenei.
-
Iran yaadhimisha mwaka mmoja tangu Vita vya Siku 12
Jun 14, 2026 03:11Maafisa wakuu wa Iran wameadhimisha mwaka mmoja tangu kuanza kwa Vita vya Siku 12, vilivyoanza tarehe 13 Juni mwaka uliopita kufuatia mashambulizi ya kichokozi ya anga ya utawala haramu wa Israel, na ambayo yaliua makamanda kadhaa wa juu wa kijeshi, maafisa wa serikali, pamoja na wanasayansi wa nyuklia.
-
Kamanda wa Khatamul-Anbiya (SAW): Hivi karibuni ulimwengu utasikia mwangwi wa ushindi wa Iran
Jun 13, 2026 11:18Kamanda wa Makao Makuu ya Majeshi ya Iran, Khatamul-Anbiya (SAW) amesema kuwa hivi karibuni ulimwengu utasikia mwangwi wa ushindi wa Iran, na ushindi wa muqawama dhidi ya adui mchokozi na gaidi.
-
Kwa nini Trump anaendelea kukariri mkakati ulioshindwa mara nyingi huko nyuma?
Jun 13, 2026 10:59Rais Donald Trump wa Marekani kwa mara nyingine tena amekiuka makubaliano legevu ya kusitisha mapigano kati ya nchi hiyo na Iran kwa kushambulia upya maeneo kadhaa ndani ya ardhi ya Iran, ikiwa ni pamoja na miundombinu ya kiraia, hii ikiwa ni siku chache tu baada ya kudai kuwa makubaliano na Iran yalikuwa yanakaribia.
-
Araqchi: Jukumu la diplomasia ni kuimarisha mafanikio ya uwanja wa vita
Jun 13, 2026 03:11Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi, ameelezea muundo wa makubaliano tarajiwa kati ya Iran na Marekani na kusisitiza kwamba diplomasia inakusudia kuimarisha mafanikio ya Jamhuri ya Kiislamu katika uwanja wa vita.
-
Kamanda mkuu wa Iran aonya Marekani kuhusu 'mzunguko usio na maana' wa uongo na migongano
Jun 13, 2026 03:06Kamanda wa Makao Makuu ya Majeshi ya Iran, Khatamul-Anbiya (SAW) ameionya Marekani kuhusu "mzunguko wa uongo, tasa na wenye migongano" katika mienendo yake, baada ya Washington kutishia kwanza kwamba itashambulia miundombinu ya nishati ya Iran na kisha kudai mazungumzo yameidhinishwa.