-
Iran: Trump hana haki ya kuzungumzia amani wakati anaisaidia Israel kuua watu kwa umati
Oct 14, 2025 06:22Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imejibu matamshi ya kibazazi ya Trump dhidi ya Tehran wakati alipolihutubia Bunge la Israel Knesset na imesema kuwa, Marekani ndiye nchi mzalishaji mkubwa wa ugaidi duniani na muungaji mkono mkuu wa wa utawala wa kigaidi umaofanya mauaji ya umati huko Ghaza, vipi inajipa mamlaka ya kimaadili ya kuwatuhumu watu wengine? Taarifa hiyo imesema kamwe wananchi wa Iran hawatasamehe wala kusahau jinai ya kinyama ya Marekani dhidi yao.
-
Iran: Dunia iwe macho, isikubali Israel ikiuke usitishaji vita Gaza
Oct 13, 2025 12:17Iran imesisitiza uungaji mkono wake usioyumba kwa juhudi zozote zinazolenga kukomesha mauaji na mauaji ya halaiki ya Israel huko Gaza, ikionya kuhusu historia ya utawala unaoikalia kwa mabavu Quds ya kukanyaga mikataba na makubaliano.
-
Ripoti: Iran yauza bidhaa za kilimo katika nchi 80 duniani
Oct 13, 2025 06:26Imeelezwa kuwa, mazao ya kilimo ya Iran yanasafirishwa kwenda nchi 80 duniani. Kwa kurekodi ukuaji mkubwa wa uzalishaji wa kilimo, Iran imejitambulisha kama mmoja wa wahusika wakuu katika soko la chakula la kimataifa.
-
Iran yakataa mwaliko wa mkutano wa Gaza; yasema haiwezi kuketi meza moja na walioishambulia
Oct 13, 2025 03:10Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amekataa mwaliko uliotolewa kwa Tehran kwa ajili ya kushiriki katika Mkutano kuhusu Gaza uliopangwa kufanyika huko Sharm el Sheikh, Misri akisema kuwa hawezi kuketi pamoja na viongozi waliowashambulia wananchi wa Iran na wanaoendelea kuitishia nchi hii na kuiwekea vikwazo.
-
Mkutano wa 8 wa Kimataifa wa Mshikamano na Watoto wa Palestina umefanyika Tehran
Oct 12, 2025 12:29Mkutano wa 8 wa Kimataifa wa Mshikamano na Watoto na mabarobaro wa Kipalestina, umefanyika leo Jumapili kwenye Ukumbi wa Mikutano ya Kiislamu mjini Tehran, kwa kuhudhuriwa na maafisa wa ndani, wageni kutoka nchi za nje na wanaharakati wa Kipalestina.
-
Spika Qalibaf: Serikali na mahakama za kimataifa zifuatilie kesi ya wahusika wa mauaji ya kimbari Gaza
Oct 12, 2025 12:10Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) sambamba na kueleza kuwa usitishaji vita wa Gaza ni kushindwa kwa mipango michafu ya Waziri Mkuu wa utawala wa kizayuni amesema: "Serikali na mahakama za kimataifa zinapaswa kufuatilia kesi ya wahusika wa mauaji ya kimbari huko Gaza."
-
Iran mstari wa mbele katika kulinda mazingira ya Bahari ya Kaspi
Oct 12, 2025 10:39Jamhuri ya Kiislamu ya Iran siku zote imekuwa na nafasi athirifu na chanya katika kulinda mazingira ya Bahari ya Kaspi na aina mbalimbali za wanyama, ikiwa ni pamoja na Caspian Seal; mamalia adimu zaidi duniani na viumbe wengine wa baharini.
-
Iran yalaani vikali shambulio la Israel kusini mwa Lebanon lililoua watu na kusababisha hasara kubwa
Oct 12, 2025 06:25Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani vikali mashambulio ya kijeshi yanayofanywa kila mara na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Lebanon na kuendelea kukiuka mamlaka ya utawala na umoja wa ardhi ya nchi hiyo hususan shambulio la jana Jumamosi la ndege zisizo na rubani lililolenga kijiji cha Al-Musayleh.
-
"Israel haiaminiki; Iran inaunga mkono kusimamishwa mauaji ya kimbari Gaza"
Oct 12, 2025 02:59Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi amesema Jamhuri ya Kiislamu inakaribisha kusitishwa kwa mauaji ya kimbari ya utawala wa Israel katika Ukanda wa Gaza, huku akitoa indhari juu ya tabia ya kutokuwa na muamana Tel Aviv kwa kukiuka makubaliano kadhaa ya huko nyuma.
-
Iran: Tutalinda maslahi yetu Ghuba ya Uajemi hadi tone la mwisho la damu
Oct 11, 2025 05:37Kamanda wa Jeshi la Wanamaji la Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH amegusia uwezekano wa kutokea vita vya moja kwa moja vya kijeshi baina ya Iran na Marekani katika Ghuba ya Uajemi na kusema: Tutajihami na kulinda maslahi yetu katika Ghuba ya Uajemi hadi tone la mwisho la damu.