-
Jeshi, IRGC: Iran inawakabili maadui ambao hakuna taifa jengine linalothubutu 'kuwafyatulia hata risasi moja'
Sep 15, 2026 11:38Wasemaji wakuu wa Jeshi la Iran na Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) wameashiria umoja usioweza kuvunjika kati ya matawi hayo mawili ya kijeshi na kutangaza kwamba Iran inavishambulia kwa mafanikio vikosi vya Marekani na Israel, vilivyojizatiti kwa silaha nzito, ambazo hakuna nchi nyingine yoyote duniani inayothubutu kukabiliana nazo.
-
Iran yasema hakuna mazungumzo na Marekani hadi masharti yake yatimizwe
Sep 15, 2026 04:18Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (SNSC), Meja Jenerali Mohsen Rezaei, amesisitiza kuwa kauli za mkanganyiko na ujumbe unaotatanisha kutoka kwa Rais wa Marekani haupaswi kumpotosha yeyote kutoka kwenye uhalisia mpya uliopo sasa kuhusu mafuta na milango-bahari, akiongeza kuwa hakutakuwa na mazungumzo yoyote hadi masharti yaliyowekwa na Iran yatimizwe kikamilifu.
-
Meli kubwa ya mafuta yalipuka baada ya kukanyaga mabomu ya majini kwenye njia haramu kusini mwa Hormuz
Sep 15, 2026 04:15Kikosi cha Wanamaji cha Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) kimetangaza kuwa meli kubwa ya kubeba mafuta ghafi (supertanker) iliyojaribu kupita bila idhini katika eneo lililopigwa marufuku kusini mwa Lango Bahari la Hormuz imelipuka baada ya kukanyaga mabomu ya kutega majini, huku chombo hicho chote kikiwa kimeteketea na kufunikwa na miali mikubwa ya moto.
-
Jeshi la Iran laangusha ndege ya kivita isyo na rubani ya Marekani katika Lango la Hormuz
Sep 14, 2026 09:18Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa limetungua na kuiangamiza ndege nyingine isiyo na rubani (droni) ya kisasa ya kivita ya Marekani aina ya MQ-1 juu ya anga ya Lango-Bahari la Hormuz.
-
Iran: Haya ndiyo masharti yetu ya kufungua Lango Bahari la Hormuz
Sep 14, 2026 07:38Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ametangaza kuwa kufunguliwa upya Lango Bahari la Hormuz kunategemea Marekani kurejea na kuheshimu ahadi zake chini ya Mkataba wa Maelewano wa Islamabad.
-
Waziri wa Ulinzi: Iran itakuwa na teknolojia ya kisasa zaidi katika vita vyovyote vipya
Sep 14, 2026 04:02Kaimu Waziri wa Ulinzi wa Iran amesisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu itakuwa na maendeleo makubwa zaidi ya kiteknolojia iwapo vita vingine vitazuka.
-
Rais wa Iran aihimiza BRICS kulinda kanuni ya kutotumia mabavu
Sep 13, 2026 11:29Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Dkt. Masoud Pezeshkian, ametoa wito kwa kundi la mataifa yanayoinukia kiuchumi la BRICS kuchukua jukumu “lenye ufanisi zaidi” katika kulinda mamlaka ya kitaifa na kusimamia kanuni ya kimataifa ya kutotumia nguvu, hasa katika kipindi hiki cha sasa chenye changamoto nyingi.
-
Wairani 352,983 washtaki Marekani na Israel kwa vita vya kwanza dhidi ya Iran
Sep 13, 2026 11:18Kesi ya kwanza ya madai iliyofunguliwa na familia za waathiriwa wa “Vita vya Siku 12” vilivyoanzishwa na Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Iran mwezi Juni 2025, ilisikilizwa Jumapili asubuhi katika Mahakama ya Iran jijini Tehran.
-
Shambulio la Marekani dhidi ya Meli za Mafuta za Iran: Mvutano Wahama kutoka Shinikizo la Kiuchumi hadi Mapigano ya Kijeshi
Sep 13, 2026 09:22Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imesisitiza kupitia taarifa kuwa Majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran hayatasita kutumia haki yake ya kimsingi ya kujilinda kisheria na kwamba yatajibu vikali na ipaswavyo kitendo chochote cha uchokozi wa kijeshi wa adui.
-
Kwa nini Marekani Inahusisha Mgogoro wa Yemen na Iran?
Sep 13, 2026 09:19Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesisitiza kuwa madai ya uongo ya Marco Rubio, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, hayawezi kubadili uhalisia wa mambo kwamba Ansarallah ya Yemen ni kundi huru linalofanya maamuzi yake lenyewe, halipokei maagizo kutoka kwa mtu yeyote wala kufanya kazi kama kibaraka wa upande mwingine.