-
Baghaei amhoji Guterres; kwa nini unahepa kuwataja wavurugaji wawili wakuu wa sheria za kimataifa?
Jul 31, 2026 03:40Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria matamshi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu kupuuzwa kwa sheria za kimataifa kwa namna inayotisha, na kumhutubu yeye kwa kumwambia: "Sasa ni wakati wa kutimiza jukumu lako zito na kusaidia kuzuia Umoja wa Mataifa na mfumo wa kanuni zake kutofikwa na hatima ya Jumuiya ya Mataifa."
-
Zaidi ya watu milioni 2 wavuka mipaka ya Iran kwa ajili ya Arubaini ya Imam Hussein (AS)
Jul 31, 2026 03:33Zaidi ya mazuwari milioni mbili wa Iran wamevuka salama mipaka ya nchi ili kuhudhuria shughuli ya kila mwaka ya Arubaini ya Imam Hussein, mojawapo ya mikusanyiko mikubwa zaidi ya kidini duniani, inayofanyika katika mji mtakatifu wa Karbala nchini Iraq.
-
Mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Iran yaharibu ndege tatu za F-35 katika kambi ya Marekani huko Jordan
Jul 30, 2026 14:59Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (IRGC) limetangaza kuwa limefanya mashambulizi ya makombora ya balestiki kwenye Kituo cha Anga cha Muwaffaq Salti kinachoendeshwa na jeshi la Marekani huko Azraq, nchini Jordan, na kuharibu ndege tatu za kivita za Marekani aina ya F-35 na kusababisha madhara makubwa kwa ndege nyingine tatu, katika operesheni ya kulipiza kisasi kwa shambulio la anga la Marekani lililoua watu watatu wa familia moja kwenye Kisiwa cha Qeshm nchini Iran.
-
Shambulio la kinyama la US kisiwani Qeshm, Iran laua wazazi na mtoto wao mdogo
Jul 30, 2026 11:09Wanafamilia watatu, wakiwemo mama, baba na mtoto wao wa kiume wa miaka miwili, wameuawa shahidi katika shambulio la kinyama la anga la jeshi la kigaidi la Marekani lililolenga jengo la makazi kwenye Kisiwa cha Qeshm kusini mwa Iran.
-
Kwa nini Marekani ilisimamisha vita dhidi ya Iran baada ya wiki mbili?
Jul 30, 2026 07:55Kufuatia wiki mbili za uhasama na baada ya Rais Donald Trump wa Marekani kuzungumzia uwezekano wa kupanua mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Iran, mapigano kati ya pande hizi yalisimama ghafla.
-
Namna Nguvu Dhaniwa ya Ulaya Ilivyosambaratika?
Jul 30, 2026 04:34Esmaeil Baghaei, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, huku akijibu karibuni hivi hatua ya Umoja wa Ulaya ya kuiwekea Iran vikwazo vipya kwa kisingizio cha kutetea haki za binadamu, amesema: "Madai ya Umoja wa Ulaya kuhusu kutetea haki za binadamu za wananchi wa Iran ni unafiki mtupu."
-
Jeshi la Iran lashambulia kambi ya anga ya Marekani Jordan, lasimamisha meli Hormuz
Jul 29, 2026 14:33Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetekeleza shambulizi la kulipiza kisasi kwa makombora ya balistiki dhidi ya kambi ya Jeshi la Anga la Marekani nchini Jordan, sambamba na kusimamisha meli tatu zilizoingia kinyume cha sheria katika Lango Bahari la Hormuz.
-
Iran yaonya: Hujuma za Marekani na Israsel ni tishio kwa amani duniani
Jul 29, 2026 14:28Iran imeonya kuwa kuendelea kwa hujuma za kijeshi za utawala wa Kizayuni wa Israel huko Gaza, mashambulizi dhidi ya nchi jirani, na upanuzi wa makazi haramu, sambamba na hujuma zisizo halali za Marekani dhidi ya Iran, kunaleta tishio kubwa kwa amani ya kikanda na ya kimataifa huku ikisisitiza tena haki yake ya kujilinda.
-
Taasisi ya Royan ya Iran ni miongoni mwa taasisi 10 bora duniani katika kutibu ugumba
Jul 29, 2026 14:25Taasisi ya Utafiti ya Royan ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetajwa kuwa miongoni mwa taasisi kumi zenye ushawishi mkubwa zaidi duniani katika masuala ya utafiti wa ugumba wa kiume na teknolojia ya usaidizi wa uzazi (ART) ikishika nafasi ya tisa kimataifa.
-
Ripoti: Iran inadhihirisha uwezo unaoongezeka wa kushambulia shabaha za kijeshi za US kupitia operesheni za pamoja
Jul 29, 2026 02:59Iran imeonyesha uwezo unaoongezeka wa kushambulia vituo vya kijeshi vya Marekani kote Asia Magharibi kwa kuchanganya ndege zisizo na rubani za mashambulizi na makombora ya kisasa ya balestiki. Hii ni kwa mujibu wa ripoti iliyomnukuu ripoti afisa wa ngazi ya juu wa Marekani.