-
Iran: Hujuma dhidi ya madaraja ni uhalifu wa kivita
Apr 04, 2026 03:18Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani vikali Marekani na utawala wa Israel kwa kutekeleza “uhalifu wa kivita wa kigaidi wa mtindo wa Daesh” wakati wa vita vyao vya kichokozi vinavyoendelea dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu, akisema maadui hao wawili hawatapata nguvu kwa kuharibu madaraja makubwa nchini Iran.
-
Pezeshkian: Tutailinda Iran kwa azma thabiti na uwezo wetu wote
Apr 04, 2026 02:56Rais Mahmoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran huku akiashiria kwamba Iran ilishambuliwa kijeshi na Marekani na utawala haramu wa Israel wakati ilipokuwa kwenye mazungumzo na Marekani, amesema: "Sisis tunasisitiza juu ya azma thabiti ya kujilinda."
-
Uchina: Tehran haitasalimu amri mbele ya mashinikizo
Apr 04, 2026 02:52Huku akielezea upinzani wa Beijing kuhusu kushambuliwa miundombinu ya Iran, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China, amesema Tehran kamwe haitapigishwa magoti na mashinikizo yoyote ya kijeshi na kwamba hatua hizi zitachochea tu moto wa mivutano.
-
Marekani na Israel zalenga Chuo Kikuu cha Shahid Beheshti katika hujuma dhidi ya sayansi Iran
Apr 03, 2026 22:58Muungano wa kijinai wa Marekani na Israel unaendelea na mashambulizi yake dhidi ya miundombinu ya kitaaluma na ya kiraia nchini Iran, huku shambulizi la karibuni likiharibu vibaya kituo cha utafiti katika Chuo Kikuu cha Shahid Beheshti mjini Tehran.
-
Jeshi la Iran laapa kuendelea na vita hadi Marekani na Israel ‘zitakapojutia’ uchokozi wao
Apr 03, 2026 06:39Msemaji mkuu wa Jeshi la Iran amesema Tehran itaendelea na vita vilivyoanzishwa na Marekani na Israel hadi kuifanya Marekani na utawala wa Israel "zijutie" kitendo chao cha uchokozi kinyume cha sheria.
-
IRGC yashambulia kampuni ya Kimarekani ya Oracle nchini Imarati
Apr 03, 2026 05:24Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu limetangaza katika taarifa yake kuwa: Limetoa kipigo kikali kwa Kampuni ya Kimarekani ya Oracle kufuatia mauaji ya kigaidi ya Mkuu wa Baraza la Kistratejia la Uhusiano wa Nje la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na mkewe.
-
IRGC yatungua ndege ya pili ya kivita ya Marekani aina ya F-35 katika anga ya katikati mwa nchi
Apr 03, 2026 04:45Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa limetungua ndege ya pili ya kisasa ya Marekani aina ya F-35 ikiwa katika anga katikati ya Iran kwa kutumia mfumo mpya wa ulinzi wa anga wa Kikosi cha Anga cha jeshi hilo.
-
Pezeshkian: Nchi za Ulaya zinawajibika kujibu uchokozi wa Marekani na Israel dhidi ya Iran
Apr 03, 2026 04:41Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amekosoa utendaji wa Umoja wa Ulaya mkabala wa ukiukwaji wa wazi wa sheria unaofanywa na Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel, akisema: "Nchi chache za Ulaya zimechukua msimamo wa kuwajibika dhidi ya uchokozi huo, na nyingi zimekuwa na mtazamo wa kutojali na hata wa upendeleo."
-
Iran na Oman kuandaa itifaki ya Lango Bahari la Hormuz
Apr 03, 2026 03:38Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa Iran na Oman zinashirikiana kuandaa itifaki ya pamoja ili kuhakikisha usafiri salama wa majini katika Lango Bahari la Hormuz katika kipindi cha baada ya vita.
-
Amir Hatami: Hakuna adui hata mmoja anayepaswa kubakia hai
Apr 02, 2026 07:17Kamanda wa Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameiagiza Makao Makuu ya Operesheni ya Jeshi kufuatilia nyendo na vitendo vya adui kwa jicho la kushuku na usahihi mkubwa, mara kwa mara, na kutekeleza mipango ya kukabiliana na mbinu za mashambulizi ya adui kwa wakati unaofaa.