-
Kamanda mkuu wa Iran aonya Marekani kuhusu 'mzunguko usio na maana' wa uongo na migongano
Jun 13, 2026 03:06Kamanda wa Makao Makuu ya Majeshi ya Iran, Khatamul-Anbiya (SAW) ameionya Marekani kuhusu "mzunguko wa uongo, tasa na wenye migongano" katika mienendo yake, baada ya Washington kutishia kwanza kwamba itashambulia miundombinu ya nishati ya Iran na kisha kudai mazungumzo yameidhinishwa.
-
Baqaei: Mashambulizi ya Marekani dhidi ya meli za India ni uharamia wa serikali
Jun 13, 2026 02:41Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Esmaeil Baqaei amelaani mashambulizi ya kikatili ya Marekani dhidi ya meli za kibiashara za India, na kusisitiza kuwa mashambulizi hayo ya Marekani katika Bahari ya Oman ni uharamia wa serikali.
-
Hatibu wa Swala ya Ijumaa Tehran: Adui akikosea, atazabwa kibao kikali
Jun 12, 2026 14:13Hatibu wa Swala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran amesema: "Adui wa taifa haelewi lugha ya mazungumzo wala lugha ya kusitisha mapigano, bali anaelewa lugha ya mabavu, ambayo majeshi yetu yamemfanya aielewe vizuri sana na yataendelea kumfanya adui ielewe vizuri zaidi."
-
Rais Pezeshkian: Wairani wameungana kuilinda nchi yao dhidi ya vitisho
Jun 12, 2026 12:44Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amesema kwamba taifa litalinda uhuru na mamlaka yake ya kitaifa licha ya kuongezeka vitisho na mashinikizo.
-
Handala yadukua mifumo ya maji ya California baada ya Marekani kushambulia maghala ya maji ya Iran
Jun 12, 2026 11:23Kundi la wadukuzi wanaopinga uvamizi wa kivita wa Marekani limetangaza kwamba limedukua vituo vya maji vya California kama kulipiza kisasi cha moja kwa moja kwa shambulio la anga la Marekani lililoharibu maghala ya maji ya kunywa kusini mwa Iran.
-
Iran: Makubaliano ya kumaliza vita yanakaribia lakini Marekani ina misimamo kinzani na inaendeleza uchokozi
Jun 12, 2026 04:45Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa sehemu muhimu za maelewano yanyolenga kumaliza vita vilivyolazimishwa zinakaribia kukamilika, pamoja na kuwepo misimamo kinzani ya Washington na vitendo vya mara kwa mara vya uchokozi wa kijeshi vinavyolenga kuvuruga mchakato wa kidiplomasia.
-
Majeshi ya Iran yashambulia ngome za kijeshi za Marekani kujibu uchokozi
Jun 11, 2026 11:42Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) likishirikiana na Jeshi la Taifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (Artesh), limetangaza mfululizo wa operesheni za kijeshi za kulipiza kisasi zilizoratibiwa vyema dhidi ya kambi za kijeshi za Marekani katika eneo la Asia Magharibi.
-
Ulaya na vikwazo vipya dhidi ya Iran; Kutetea ubaharia au muendelezo wa mashinikizo ya kisiasa?
Jun 11, 2026 10:44Akizungumzia vikwazo vilivyowekwa karibuni na Umoja wa Ulaya dhidi ya baadhi ya shakhsia na taasisi za Iran, Kazem Gharibabadi Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayeshughulikia Sheria na Masuala ya Kimataifa amesema: 'Iran haiipi thamani yoyote hatua hiyo ya kimaonyesho ya Ulaya.'
-
Kamandi Kuu ya Jeshi la Iran yaamuru kufungwa Mlango Bahari wa Hormuz kwa meli zote baada ya mashambulizi mapya ya Marekani
Jun 11, 2026 03:18Kamandi Kuu ya Jeshi la Iran imeamuru kufungwa Mlango-Bahari wa Kistratejia wa Hormuz muda mfupi baada ya kuanza hujuma mpya ya kijeshi ya Marekani dhidi ya Iran, licha ya Jamhuri ya Kiislamu kuonya juu ya chokochoko hizo.
-
IRGC yaangusha droni ya kivita ya Marekani aina ya MQ 9 karibu na Hormuz
Jun 11, 2026 03:15Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limesema kuwa liliangusha droni ya kivita ya Marekani aina ya MQ 9 karibu na Mlango Bahari wa Hormuz, wakati mvutano wa kijeshi ukiongezeka kufuatia vitendo vya kijeshi vya Marekani na ukiukaji wa mara kwa mara wa makubaliano ya kusitisha mapigano.