-
Lango-Bahari la Hormuz liko chini ya udhibiti kamili wa IRGC
Apr 02, 2026 04:27Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) limetangaza kuwa Lango-Bahari la Hormuz sasa liko chini ya udhibiti kamili wa vikosi vyake vya majini, huku likitoa maelezo ya mfululizo wa operesheni za makombora na ndege zisizo na rubani dhidi ya malengo ya Marekani na Israel katika maeneo mbalimbali ya kanda.
-
Rais Pezeshkian: Shambulio dhidi ya miundombinu ya Iran ni dalili ya udhaifu wa Marekani
Apr 02, 2026 04:22Rais wa Iran, amehoji katika ujumbe aliouelekeza kwa wananchi wa Marekani kwamba: Vita vinavyoendelea sasa vinanufaisha vipi maslahi halisi ya watu wa Marekani? Amesisitiza kuwa mashambulio dhidi ya miundombinu muhimu ya Iran, ikiwemo vituo vya nishati na viwanda, ni hatua inayolenga moja kwa moja kuvuruga maisha ya watu wa Iran.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu aiambia Hizbullah: Iran itaendelea kuunga mkono Muqawama dhidi ya Marekani na Wazayuni
Apr 01, 2026 05:32Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Mojtaba Ali Khamenei amemwandikia barua Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon, Sheikh Naim Qassem, akiahidi kuendeleza uungaji mkono wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa harakati hiyo ya Muqawama na mapambano katika kukabiliana na adui, Marekani na Uzayuni.
-
Brigedia Jenerali Fadavi: Ujinga wa Marekani umewaletea matatizo walimwengu
Apr 01, 2026 04:13Mshauri wa Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema: “Walimwengu sasa wanakabiliwa na matatizo makubwa ya nishati kutokana na upumbavu wa shetani mkubwa, Marekani.”
-
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje: Marekani inataka kuhuisha fikra ya ufashisti ya kabla ya Vita vya Pili vya Dunia
Apr 01, 2026 04:00Akijibu kauli za Seneta wa chama cha Republican, Lindsey Graham, na mshauri wa zamani wa Donald Trump, Steve Bannon kuhusu kutumia mifano ya kihistoria kuhalalisha vita, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje wa Iran amesema: "Marejeleo haya ya kihistoria yanafanana waziwazi na mawazo ya Wanazi na Wafashisti."
-
Kiongozi Muadhamu awashukuru wanazuoni wa Kisuni wa Kurdistan kwa uungaji mkono wao
Apr 01, 2026 03:20Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, ametoa shukrani kwa wanazuoni wa Kisuni katika Mkoa wa Kurdistan nchini Iran kufuatia ujumbe wao wa pole na mshikamano baada ya kuuawa shahidi aliyekuwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei.
-
Mwakilishi wa Iran UN alaani shambulio la US na Israel dhidi ya ofisi za Umoja wa Mataifa mjini Tehran
Apr 01, 2026 03:13Balozi na mwakilishi wa Iran katika Umoja wa Mataifa amemwandikia barua Katibu Mkuu na Rais wa Baraza la Usalama la umoja huo, akilaani mashambulizi ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya ofisi za Umoja wa Mataifa mjini Tehran na kutoa wito wa ufuatiliaji wa haraka na kutolewa ripoti rasmi kuhusu tukio hilo.
-
Araghchi: Iran haijatoa jibu lolote kwa mapendekezo 15 ya Marekani
Apr 01, 2026 03:07Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema: Tehran hadi sasa haijatoa jibu kwa mapendekezo 15 ya Marekani, wala haijawasilisha sharti lolote.
-
Ahadi ya Kweli 4, Wimbi la 88: Jeshi la Wanamaji la IRGC laharibu mfumo wa kukabiliana na droni wa US Fifth Fleet
Mar 31, 2026 06:18Kikosi cha Wanamaji la Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) mapema leo Jumanne kimefanya operesheni nne dhidi ya shabaha za magaidi wa Kimarekani na Israel na kutoa vipigo vikali ikiwa ni sehemu ya wimbi la 88 la Operesheni Ahadi ya Kweli-4.
-
Pezeshkian alishukuru taifa la Iraq kwa kuwa bega kwa bega na Iran katika mapambano dhidi ya Marekani, Israel
Mar 31, 2026 06:17Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amesifu na kupongeza ujasiri wa taifa la Iraq wa kusimama bega kwa bega na watu wa Iran katika kipindi hiki cha uvamizi wa Marekani na Israel dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.