-
Spika Qalibaf: Iran itatumia vita na diplomasia kutetea haki za watu wake
Jun 09, 2026 12:21Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf anasema mkakati wa nchi wa kukomesha uchokozi wa Marekani na Israel ni kutumia vita na diplomasia kwa wakati mmoja ili kutetea haki za taifa la Iran.
-
Gazeti la Kizayuni: Iran ilikuwa na kauli ya mwisho katika vita vya sasa
Jun 09, 2026 11:18Gazeti la Kiebrania huko Israel limekiri kwamba nguvu ya Iran imethibitishwa katika majibu yake ya hivi karibuni ya makombora dhidi ya utawala wa Israel.
-
Maprofesa 12 wa Chuo Kikuu cha Amirkabir watajwa miongoni mwa 1% ya watafiti watajika sana duniani
Jun 09, 2026 04:39Maprofesa 12 wa Chuo Kikuu cha Teknolojia cha Amirkabir cha Iran wametambuliwa miongoni mwa asilimia moja bora zaidi ya watafiti waliotajwa sana duniani, kwa mujibu wa ripoti ya hivi karibuni iliyotolewa na Taasisi ya Unukuzi na Ufuatiliaji wa Sayansi ya Ulimwengu wa Kiislamu (Islamic World Science Citation and Monitoring Institute (ISC)).
-
Pezeshkian: Iran haitalegeza kamba, itasimama kidete kulinda taifa dhidi ya vitisho
Jun 09, 2026 04:37Rais Masoud Pezeshkian ametilia mkazo msimamo thabiti wa Iran dhidi ya tishio lolote, akisema Jamhuri ya Kiislamu haitarudi nyuma wala kusita kulinda usalama na amani ya taifa lake.
-
Rais wa Colombia asema 'ufashisti katika Ikulu ya White House unapofusha mantiki na akili
Jun 09, 2026 04:23Rais wa Colombia, Gustavo Petro, ameikosoa Marekani kuhusu "ufashisti ulioenea katika Ikulu ya White House" huku mvutano ukiongezeka kati ya Bogota na Washington.
-
Bab al-Mandab, mstari mpya wa kuzuia hujuma na kuimarisha uwiano wa "Umoja wa Medani"
Jun 08, 2026 12:10Msemaji wa Jeshi la Yemen ametangaza kwamba kuanzia sasa jeshi hilo limeanza kutekeleza amri ya kupiga marufuku kikamilifu meli zote za utawala haramu wa Israel kupita katika maji ya Bahari ya Shamu au kwa Kiingereza Red Sea na kwamba kuanzia wakati wa kutangazwa marufuku hiyo na kuendelea urambazaji wa baharini wa Israel katika Bahari Nyekundu utakuwa shabaha halali ya jeshi la wanajeshi wa Yemen.
-
Jeshi la Iran lashambulia kambi za kimkakati za anga za jeshi la anga la Israel kujibu uchokozi
Jun 08, 2026 11:23Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuanzisha “Operesheni Nasr” (Ushindi), likisema limezilenga kambi za kimkakati za anga za utawala wa Israel za Nevatim na Tel Nof, kama hatua ya kujibu mashambulizi ya makombora yaliyolenga vituo vya rada vya Iran.
-
Araghchi afanya mazungumzo ya kidiplomasia kuhusu uchokozi wa Israel
Jun 08, 2026 11:20Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi, amefanya mfululizo wa mazungumzo kwa njia ya simu na baadhi ya mawaziri wenzake wa maeneo mbali mbali duniani pamoja na kamanda wa jeshi, kufuatia hatua ya Iran kujibu ukiukaji wa mara kwa mara wa makubaliano ya usitishaji mapigano nchini Lebanon unaotekelezwa na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Jibu kali la makombora la Iran kwa ukiukaji wa mara kwa mara wa usitishaji vita na jinai za Israel nchini Lebanon
Jun 08, 2026 08:03Iikiwa ni katika kunufaika na haki yake ya kujilinda na kujibu ukiukaji wa mara kwa mara wa usitishaji vita na jinai za kinyama zinazofanywa na utawala dhalimu wa Israel dhidi ya watu wa Lebanon, vikosi vya jeshi la Iran Jumapili usiku vilitoa jibu kali la makombora katika maeneo ya utawala huo katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu. Maeneo yaliyolengwa katika shambulio hilo kubwa la makombora kimsingi ni ya kijeshi na kistratijia ya utawala wa Israel.
-
Iran yashambulia maeneo yanayokaliwa kwa mabavu, yatahadharisha kuhusu vipigo vikali zaidi' iwapo mashambulizi dhidi ya Lebanon yataendelea
Jun 08, 2026 03:23Vikosi vya ulinzi vya Iran jana usiku viliyatangwa kwa makombora maeneo kadhaa ya Israel, ikiwa ni katika kujibu mashambulizi yanayoendelea ya Israel dhidi ya Lebanon kwa kukiuka makubaliano ya kusitisha mapigano.