-
Araghchi: Kimya na misimamo ya kinafiki kwa mashambulizi dhidi ya Iran kunawapa kiburi wavamizi kuendeleza uhalifu
Jul 24, 2026 08:46Abbas Araghchi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, ukimya na misimamo ya kindumakuwili kuhusu mashambulizi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kunawapa nguvu na kuwahamasisha wavamizi kuendelea kutekeleza vitendo vyao.
-
Jeshi la SEPAH laionya Uingereza na kuitaka isizidi kulichafua faili lake
Jul 24, 2026 08:44Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) limetoa onyo kali kwa serikali ya kifalme ya Uingereza, likiitaja kuwa miongoni mwa nchi zilizokuwa na mchango mkubwa katika mashambulizi ya hivi karibuni yaliyofanywa na Marekani na utawala wa Kizayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Baqaei aionya GCC na Jordan: Kushiriki uchokozi dhidi ya Iran ni kielelezo cha uvamizi
Jul 24, 2026 08:43Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baqaei, amelionya Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi (GCC) pamoja na Jordan kwamba, ushiriki wowote katika mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Iran utachukuliwa kuwa ni kitendo cha uchokozi wa kijeshi.
-
Msishiriki katika uchokozi dhidi ya Iran, Gharibabadi azionya nchi za Ulaya
Jul 24, 2026 02:51Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Kazem Gharibabadi, amezionya nchi za Ulaya kwamba kutoa kambi au maeneo ya kijeshi kwa Marekani kutaziweka "katika safu ya wavamizi."
-
Iran iko tayari kuanzisha awamu mpya ya vita na kutumia mikakati mipya
Jul 24, 2026 02:42Msemaji wa jeshi la Iran jana Alhamisi alitahadharisha kuwa Tehran itatumia mikakati na mbinu mpya ili kuifanya Marekani ishindwe kuendeleza vita iwapo mashambulio ya nchi hiyo dhidi ya miundombinu ya kusini mwa Iran yataendelea.
-
Iran yaapa kulipiza kisasi iwapo Marekani itashambulia miundombinu
Jul 23, 2026 11:51Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Sayyid Abbas Araghchi, ameweka bayana msimamo thabiti wa Iran kwamba shambulio lolote dhidi ya miundombinu ya Iran litajibiwa kwa hatua stahiki na za maamuzi dhidi ya wachokozi na wale wote wanaowasaidia.
-
Viongozi wa Iran na Iraq wasisitiza kuimarisha mahusiano ya kimkakati
Jul 23, 2026 11:49Viongozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Iraq wamesisitiza juu ya mafungamano marefu ya kihistoria, kiutamaduni, kidini, na ya kijamii yaliyopo baina ya nchi hizo mbili, wakibainisha ulazima wa kuhifadhi na kuimarisha rasilimali hii yenye thamani kuu kama nguzo imara ya kutanua ushirikiano wa kimkakati.
-
Mashambulizi Makali ya Iran dhidi ya Vituo vya Marekani nchini Jordan
Jul 23, 2026 08:20Mashambulizi ya Iran dhidi ya vituo vya Marekani nchini Jordan yanachukuliwa kuwa miongoni mwa operesheni zilizofanikiwa zaidi katika mzozo wa kijeshi wa hivi karibuni kati ya Iran na Marekani.
-
Dkt. Pezeshkian: Hakuna sababu wala mpaka unaoweza kuvunja uhusiano wa Iran na Iraq
Jul 23, 2026 03:15Rais Masoud Pezeshkian wa Iran, amesema kuwa hakuna sababu yoyote wala mipaka ya kijiografia inayoweza kuvunja uhusiano wa kindugu na wa kihistoria uliopo kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Iraq.
-
Mkuu wa Majeshi Iran aionya Marekani kuhusu hujuma ya kijeshi ya nchi kavu
Jul 23, 2026 03:07Mkuu wa Majeshi ya Iran, Meja Jenerali Amir Hatami, ametoa onyo kali kwamba uvamizi wowote wa nchi kavu wa jeshi la Marekani utakabiliwa na jibu la kijeshi la kuangamiza. Amesisitiza kuwa mamilioni ya Wairani wako tayari kuwakabili wavamizi kwa kila nyenzo waliyo nayo, huku Majeshi ya Ulinzi yakiwa katika utayari wa hali ya juu dhidi ya uchokozi wowote.