-
Watu 12 wauawa shahidi katika mashambulizi ya anga ya Israel katika ardhi ya Lebanon
Jun 01, 2026 11:24Ikiwa ni katika muendelezo wa ukiukaji wa makubaliano ya usitishaji vita na mashambulizi ya utawala wa Israel dhidi ya miji na vijiji vya kusini mwa Lebanon yaliyotekelezwa zaidi ya mara 36 mchana na Jumapili usiku, watu 12 wameuawa shahidi na wengine 35 kujeruhiwa katika mashambulizi hayo ya jinai.
-
Yemen: Kupiga marufuku Hamas na Jihad Islami kunaonyesha jinsi Ulaya inavyoukingia kifua Uzayuni wa kimataifa.
Jun 01, 2026 09:24Wizara ya Mambo ya Nje ya Yemen imelaani vikali hatua ya Umoja wa Ulaya ya kuimarisha vikwazo dhidi ya harakati za ukombozi wa Palestina, Hamas na Jihad Islami, ikiitaja kuwa ni ishara ya utiifu kwa Uzayuni wa kimataifa.
-
Waziri wa Israeli Ben-Gvir amhimiza Netanyahu 'kusawazisha vitongoji vya Beirut na ardhi'
May 31, 2026 12:48Waziri anayejiita wa usalama wa Israel, Itamar Ben-Gvir, amemtaka Waziri Mkuu wa utawaka huo katili, Benjamin Netanyahu, kusawazisha na ardhi vitongoji vya mji mkuu wa Lebanon, Beirut huku utawala huo ukizidisha mashambulizi yake dhidi ya nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Hamas: EU imewawekea vikwazo viongozi wa Gaza lakini 'imepuuza' ukatili wa Israel
May 31, 2026 04:18Harakati ya Hamas imelaani vikwazo vya Umoja wa Ulaya, ikiikosoa kambi hiyo kwa "kufumbia macho" ukiukaji wa sheria za kimataifa unaofanywa na Israel huku ikiyalenga makundi na viongozi wa mapambano ya ukombozi wa Palestina.
-
UN: Asilimia 100 ya Gaza ni mali ya Wapalestina, yataka Israel ikomeshe uvamizi haramu
May 30, 2026 10:29Umoja wa Mataifa umekosoa vikali mipango ya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ya kupanua udhibiti juu ya Ukanda wa Gaza, na kusisitiza kuwa eneo lote ni haki ya watu wa Palestina.
-
Kwa nini utawala wa Kizayuni unasisitiza kuendeleza vita huko Lebanon?
May 30, 2026 07:00Moja ya vikwazo muhimu katika mazungumzo ya Iran na Marekani ni sisitizo la utawala wa Kizayuni wa Israel la kuondolewa medani ya vita vya Lebanon kwenye mazungumzo hayo na kuendeleza vita dhidi ya harakati ya Hizbullah. Hii ni katika hali ambayo Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetangaza kuwa moja ya masharti muhimu ya kufikiwa mapatano na Marekani ni kusimamishwa kikamilifu vita katika ngome zote za mhimili wa muqawama na hasa nchini Lebanon.
-
Hizbullah: Hakuna njia nyingine isipokuwa mapambano dhidi ya Israel
May 30, 2026 03:27Mbunge mwandamizi wa Lebanon amesema kuwa harakati ya Hizbullah itaendeleza operesheni zake za kijeshi dhidi ya vikosi vya utawala dhalimu wa Israel.
-
IRIB yalaani mauaji ya Israel dhidi ya mwandishi habari wa al-Alam kusini mwa Lebanon
May 29, 2026 12:39Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (IRIB), Peyman Jebelli, na Kitengo cha Matangazo ya Ng'ambo cha IRIB wamelaani vikali mauaji ya Hesam Zidan, mwandishi wa habari wa zamani wa chaneli ya televisheni ya al-Alam ya Iran nchini Syria, ambaye ameuawa katika shambulio la Israel kusini mwa Lebanon.
-
UN yaanika uhalifu wa kutisha wa Israel... Ripoti ya Guterres kuhusu unyanyasaji wa kingono imefichua nini?
May 29, 2026 12:38Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, Alkhamisi ya jana aliwasilisha ripoti yake ya kila mwaka kwa wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu ukatili wa kingono unaohusiana na migogoro, ambayo inarekodi ukiukwaji mkubwa na wa kutisha wa sheria uliofanywa na Israel dhidi ya Wapalestina.
-
Washington Post: Israel imetengwa duniani kutokana na vita vya mara kwa mara vya Netanyahu
May 29, 2026 02:57Gazeti la Washington Post limeandika kuwa: Vita vya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza, Lebanon, Syria, Iran na Yemen vimeiweka Israel katika njia ya mmomonyoko wa kijeshi, kushindwa kimkakati na kutengwa kimataifa.