-
Hamas yapinga kutumwa jeshi la kigeni Gaza mbadala wa jeshi vamizi la Israel
Nov 05, 2025 07:09Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas katika Ukanda wa Gaza imesema kuwa haiwezakani kutumwa kikosi chakijeshicha kigeni katika eneo hilo ambacho kitahudumu kama mbadala wa jeshi vamizi la Israel.
-
Yemen: Tumejiandaa kwa vita vikubwa na Israel
Nov 05, 2025 03:17Kiongozi wa harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema kuwa, harakati za Muqawamaa zimejiandaa kwa ajili ya awamu ijayo ya mapambano na utawala wa Kizayuni wa Israel, kwani zinaamini kwamba eneo hili halitakuwa imara kwa muda mrefu maadamu Palestina inaendelea kukaliwa kwa maabavu na dola pandikizi la Kizayuni ambalo muda wote linapanga njama dhidi ya Waislamu.
-
Utafiti: Vita vya mauaji ya kimbari vya Israel vimegharimu zaidi ya miaka milioni 3 ya maisha ya mwanadamu huko Gaza
Nov 05, 2025 03:06Utafiti wa hivi karibuni uliochapishwa katika jarida la Lancet umefichua kuwa zaidi ya miaka milioni tatu ya maisha ya binadamu yamepotea katika Ukanda wa Gaza tangu utawala ghasibu wa Israel uanzishe kampeni yake ya mauaji ya kimbari dhidi ya watu Ukanda wa Gaza ulio chini ya mzingiro, mwezi Oktoba mwaka 2023.
-
Nyaraka za jeshi la Israel zafichua: Mfungwa wa Kipalestina aliyebakwa alikuwa raia, si mpiganaji
Nov 04, 2025 11:18Waraka wa siri wa jeshi la Israel umefichua kwamba mtu aliyeshambuliwa kikatili na kubakwa na kundi la wanajeshi wa Israel katika gereza maarufu la Sde Teiman mnamo Julai mwaka jana hajawahi kushtakiwa kwa uhalifu wowote na alikuwa raia, kinyume na madai kwamba alikuwa na mwanachama harakati za mapambano ya Hamas.
-
Israel inatumia wanasesere waliotegwa mabomu kuua watoto wachanga huko Gaza
Nov 04, 2025 10:20Wizara ya Afya ya Serikali ya Palestina katika Ukanda wa Gaza imetangaza kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel umetega mabomu kwenye wanasesere ili kuwaua watoto wa Palestina.
-
Duru za Israel: Hizbullah imeshajijenga upya, sasa tusubiri vita
Nov 04, 2025 07:00Mashirika ya usalama ya Israel yametangaza kwamba yanajiandaa kwa ajili ya kuingia kwenye vita vikubwa na Hizbullah ya Lebanon yakidai kuwa harakati hiyo imeshajijenga upya kijeshi na sasa lazima wasubiri majibu makali kutoka kwa harakati hiyo.
-
Majasusi watano wa Israel watiwa mbaroni Ghaza
Nov 04, 2025 07:00Kikosi cha kujihami kiitwacho "Rad'e" kinachoshirikiana na Muqawama kwa ajili ya kulinda usalama huko Ghaza, jana Jumatatu kilifanya operesheni ya kiusalama kusini mwa mji wa Khan Yunis na kuwatia mbaroni majasusi watano wa Israel.
-
Waziri al Sudani: Wananchi wataendelea kubeba silaha madamu Marekani bado ipo Iraq
Nov 04, 2025 06:58Waziri Mkuu wa Iraq, Mohammed al-Sudani alisema jana Jumatatu kwamba kuondoka kikamilifu Marekani na muungano wake unaodaiwa wa kupambana na Daesh huko Iraq ndiko kutakakopelekea kupokonywa silaha makundi ya kujihami ya wananchi. Kwa mujibu wa makubaliano, Marekani lazima iondoke Iraq mwezi Septemba mwaka ujao wa 2026.
-
UNICEF yaonya kuhusu mzozo wa kibinadamu kwa watoto Gaza licha ya kusitishwa mapigano
Nov 04, 2025 02:26Msemaji wa Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) ameashiria hali mbaya inayowakabili zaidi ya watoto milioni moja huko Gaza, ambao wanaendelea kuhitaji chakula na maji kwa dharura.
-
Israel yaandaa muswada wa 'kifashisti' wa kuruhusu utoaji wa hukumu ya adhabu ya kifo kwa Wapalestina
Nov 04, 2025 02:25Kamati moja ya wabunge wa utawala wa kizayuni wa Israel imeidhinisha muswada wa kuanzisha utoaji wa adhabu ya kifo kwa Wapalestina wanaoshikiliwa kwenye magereza ya utawala huo, na kufungua njia ya kusomwa hoja hiyo kwa mara ya kwanza bungeni licha ya kuandamwa na lawama nyingi.