-
Hamas: Mwisho wa Abu Shabab ndio hatima isiyoepukika ya kila msaliti
Dec 05, 2025 10:50Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imeonya kwamba mauaji ya mshirika wa Israel na kiongozi wa genge lenye uhusiano na Daesh, Yasser Abu Shabab, ni hatima isiyoepukika ya kila mtu anayechagua kulisaliti taifa na nchi yake na kushirikiana na utawala ghasibu wa Israel.
-
Wairaqi waunga mkono Hizbullah na Ansarullah baada ya tangazo la kuzuiliwa mali zao kimakosa
Dec 05, 2025 07:51Mitaa ya mji mkuu wa Iraq, Baghdad usiku wa kuamkia leo ilishuhudia misafara mirefu ya magari, yaliyokuwa yakipeperusha bendera za harakati za Muqawama wa Kiislamu za Hizbullah ya Lebanon na Ansarullah ya Yemen, na kutangaza mshikamano wa umma na harakati hizo za Muqawama dhidi ya vitisho vya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Yasser Abu Shabab, mshirika wa Israel na msaliti wa Wapalestina wa Ghaza aripotiwa kuuawa
Dec 05, 2025 06:55Yasser Abu Shabab, mshirika wa kijeshi wa utawala wa kizayuni wa Israel mwenye uhusiano pia na kundi la kigaidi la DAESH (ISIS), maarufu kwa kuongoza uporaji wa misaada ya kibinadamu katika Ukanda wa Ghaza na kwa kuwalenga kwa kuwaua raia wa Palestina, ameripotiwa kuuawa katika eneo hilo.
-
Hamas: Israel iwajibishwe kwa kuzika mamia ya miili ya Wapalestina kwenye makaburi ya umati
Dec 05, 2025 02:57Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imezitaka mahakama za kimataifa na vyombo husika kuwafungulia mashtaka wale waliohusika wa uhalifu wa kivita baada ya uchunguzi kufichua kwamba wanajeshi wa Israel waliteketeza miili ya Wapalestina waliokuwa katika safu za kupokea misaada na kuizika katika makaburi yasiyo na kina huko Gaza.
-
Vita vya Kijasusi; Kadi ya Ushindi ya Iran dhidi ya Utawala wa Kizayuni
Dec 04, 2025 12:11Meya wa Bat Yam katikati ya ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu, zilizopachikwa jina bandia la Israel, amekiri kuongezeka kwa ushawishi wa kijasusi wa Iran.
-
Microsoft yalaumiwa kuhusika na jinai za Israel za maauaji kimbari dhidi ya Gaza
Dec 04, 2025 12:05Muungano wa makundi ya kisheria umelionya shirika la Microsoft kwamba utoaji wake wa huduma kwa Israel wakati wa vita vya mauaji ya kimbari huko Gaza huenda ukaifanya kampuni hiyo kubwa ya teknolojia ya Marekani ishtakiwe katika mahakama za kimataifa.
-
Baraza Kuu la UN lapasisha azimio linaloitaka Israel iondoke katika maeneo ya Wapalestina
Dec 04, 2025 07:45Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepitisha rasimu ya azimio llinaloitaka Israeli iondoke kwenye maeneo ya Palestina iliyoyavamia na kuyakaliwa kwa mabavu tangu 1967, ikiwa ni pamoja na al-Quds Mashariki. Rasimu ya azimipia imeitaka Israel itambue haki ya watu wa Palestina ya kujitawala na kuasisi nchi huru.
-
Azimio la UN: Israel inaikalia "kinyume cha sheria" Miinuko ya Golan ya Syria, iondoke kikamilifu
Dec 03, 2025 10:54Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepitisha azimio linalotangaza kuwa, kuendelea Israel kuikalia kwa mabavu na kuiunganisha na upande wake Miinuko ya Golan ya Syria ni "kinyume cha sheria" na limeutaka utawala huo uondoke kikamilifu katika eneo hilo hadi kwenye mstari wa mpaka wa Juni 4, 1967.
-
Netanyahu amramba miguu Trump amuokoe na kitanzi cha kesi mahakamani
Dec 03, 2025 06:37Duru za kuaminika za Marekani na Israel zimefichua kuwa, waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni, Benjamin Netanyahu amemuomba kwa kumsisitiza rais wa Marekani, Donald Trump afanye kila awezalo kuhakikisha kuwa anafutiwa kesi zake za ufisadi.
-
Utajiri wa madini ya Yemen na jicho la tamaa la madola ya kibeberu
Dec 03, 2025 02:22Yemen imegundua utajiri mkubwa wa rasilimali za madini, ikiwa ni pamoja na akiba kubwa ya dhahabu, chuma, titani na madini ya viwandani. Rasilimali hizi zinaweza kufungua njia ya maendeleo ya kiuchumi na kuimarisha nafasi ya kimkakati ya Yemen katika eneo hili zima.