-
Ansarullah ya Yemen: Saudi Arabia inahudumia miradi ya Wamarekani-Wazayuni
Jul 19, 2026 03:24Mjumbe wa ngazi za juu wa harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema kwamba Saudi Arabia imeweka uwezo na suhula zake za kisiasa, kifedha na kijeshi katika huduma ya miradi ya Marekani eneo la Asia Magharibi na inafanya kazi ya kudhoofisha mataifa ambayo yana misimamo dhidi ya Israel.
-
Israel yafanya mauaji makubwa huko Nuseirat, janga la binadamu linazidi kuwa baya Gaza
Jul 18, 2026 10:59Wapalestina 14 wameuawa na wengine 37 kujeruhiwa, wengi wao wakiwa katika kambi ya Nuseirat katikati mwa Ukanda wa Gaza, kutokana na mashambulizi mtawalia ya Israel yaliyolenga maeneo mbalimbali ya ukanda huo, huku hali ya kibinadamu ikizidi kuwa mbaya.
-
Mossad, Epstein na operesheni za siri: Vance aishambulia Israel na kusema umaarufu wake umeporomoka
Jul 18, 2026 03:16Katika mahojiano yake ya hivi karibuni, Makamu wa Rais wa Marekani J.D. Vance aliishambulia Israel na kuishutumu kuwa inajaribu kushawishi siasa za Marekani, akisisitiza kuwa umaarufu wake umepungua nchini Marekani.
-
Mateka wa zamani Muisraeli huko Gaza: Ninapata amani ninaposikiliza Qur'ani
Jul 18, 2026 03:15Hadithi ya mateka wa zamani wa Hamas, Emily Damari imevuma tena katika vyombo vya habari katika tukio lililozua dhoruba ya hasira ndani ya duru za Israel na kwenda mbali zaidi hadi kutolewa wito mwanamke huyo arudishwe matekani huko Gaza!
-
Mkurugenzi wa Huduma za Dharura Gaza: Asilimia 80 ya uwezo wa uokoaji umeharibiwa
Jul 17, 2026 11:46Mkurugenzi wa Huduma za Dharura katika Ukanda wa Gaza amesema kuwa takribani asilimia 80 ya uwezo wa huduma za uokoaji na misaada ya dharura umeangamizwa kutokana na mashambulizi na uharibifu unaoendelea kufanywa na utawala ghasibu wa Israel katika eneo hilo.
-
Mpango wa kuvunjwa Bunge la utawala wa Kizayuni (Knesset) wapitishwa rasmi
Jul 17, 2026 11:45Rasimu ya sheria ya kuvunjwa Bunge la utawala wa Kizayuni (Knesset) imepitishwa rasmi, hatua inayofungua njia ya kuitisha uchaguzi mpya wa mapema Israel.
-
Wagonjwa wa saratani Gaza wakabiliwa na uhaba mkubwa wa dawa na vifaa tiba
Jul 17, 2026 02:53Wagonjwa wa saratani katika Ukanda wa Gaza wanakabiliwa na hali ngumu kutokana na uhaba mkubwa wa dawa na vifaa vya matibabu, hali inayozidi kuhatarisha maisha yao huku mfumo wa afya ukiendelea kulemewa na athari za mzingiro na vita.
-
Oman: Tishio hatari zaidi halitokani na Tehran bali Tel Aviv
Jul 15, 2026 03:52Serikali ya Oman imesema tishio kubwa zaidi kwa usalama na utulivu wa eneo halitokani na Tehran, bali linatoka Tel Aviv.
-
Yemen yaionya Saudia: Shambulio dhidi ya uwanja wa ndege wa Sana’a ni mwisho wa usitishaji vita
Jul 14, 2026 04:42Wizara ya Mambo ya Nje ya Yemen mjini Sana’a imelaani vikali shambulio la Saudi Arabia dhidi ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Sana’a, ikisisitiza kuwa hatua hiyo ya kijeshi inahitimisha rasmi kipindi cha usitishaji vita na kuashiria kuanza kwa awamu mpya ya vita.
-
Mfungwa wa Kipalestina aelezea unyanyasaji wa wanawake katika magereza ya Israel
Jul 12, 2026 12:26Mfungwa mwanamke Mpalestina amesimulia uvamizi wa mara kwa mara, unyanyasaji wa kimwili na hali mbaya ya kizuizini inayowaathiri wanawake Wapalestina waliofungwa katika magereza ya Israel.