Asia Magharibi
-
Armenia yalitambua rasmi taifa huru la Palestina
Jun 21, 2024 12:20Serikali ya Armenia imetangaza kuwa, imelitambua rasmi taifa huru la Palestina.
-
Ansarullah: Operesheni za Yemen zinaashiria kuimarika kambi ya muqawama
Jun 21, 2024 07:39Msemaji wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema operesheni za nchi hiyo dhidi ya utawala haramu wa Israel ni ushahidi wa kupata nguvu na kuwa na umoja mrengo wa muqawama katika eneo la Asia Magharibi katika kuitetea Palestina.
-
Umoja wa Mataifa watoa onyo kali kuhusu kuongezeka majanga katika Ukanda wa Gaza
Jun 21, 2024 02:14Francesca Albanese, Ripota wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Palestina, amesema katika taarifa kwamba hali ya maafa huko Ukanda wa Gaza imezidi kuwa mbaya. Kwa kauli yake, utawala haramu wa Israel unalenga misafara ya misaada ya kibinadamu inayotumwa Gaza na kuzuia ufikaji wa misaada katika ukanda huo.
-
Wasiwasi unaozidi kuongezeka wa Biden kuhusu chokochoko za Netanyahu kusini mwa Lebanon
Jun 20, 2024 08:23Amos Hochstein, mjumbe wa Biden, amelitembelea tena eneo la Asia Magharibi ikiwa ni katika juhudi zake za kutuliza hali ya mambo katika eneo la kaskazini mwa Palestina inayokaliwa kwa mabavu (Israel).
-
Ushindi mwingine mkubwa kwa HAMAS, jeshi la Israel latangaza rasmi haliwezi kuifuta, Netanyahu aja juu
Jun 20, 2024 07:10Msemaji wa Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel (IDF), Daniel Hagari alisema jana Jumatano kwamba Hamas haiwezi kufutwa na amependekeza kufikiwe makubaliano ya kubadilishana mateka kwani hiyo ndiyo njia pekee ya kuhakikisha mateka wote wa Israel wanaoshikiliwa huko Ghaza wanaachiliwa huru.
-
Israel yaongeza maambukizi ya homa ya ini kwa wakimbizi wa Ghaza
Jun 20, 2024 02:56Duru za hospitali katika Ukanda wa Ghaza zimeonya kuhusu kuenea ugonjwa wa homa ya ini na jinsi utawala wa Kizayuni wa Israel unavyoeneza ugonjwa huo kati ya wakimbizi wa Palestina.
-
Hizbullah yashambulia kiwanda na kambi za kijeshi za Israel
Jun 19, 2024 11:16Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imeshambulia kwa makombora na ndege zisizo na rubani kiwanda na kambi kadhaa za kijeshi za utawala wa Kizayuni Israel huko kaskazini mwa ardhi za Palestina zilizopachikwa jina bandia la Israel, kujibu chokochoko za jeshi hilo katili.
-
HAMAS yaitaka jamii ya kimataifa kuwasaidia watu wa Gaza
Jun 19, 2024 03:21Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (Hamas) imetoa mwito wa kupitishwa maamuzi ya dharura na jamii ya kimataifa ya kusimamisha jinai za utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Gaza na kuwasaidia wananchi wa ukanda huo wanaokabiliwa na masaibu mengi.
-
Ndege za kivita za Marekani na Uingereza zashambulia tena magharibi mwa Yemen
Jun 18, 2024 08:16Ndege za kivita za Marekani na Uingereza kwa mara nyingine tena zimeshambulia kwa mabomu maeneo ya magharibi mwa Yemen.
-
Kamanda mwingine wa Hizbullah auawa shahidi na droni ya Wazayuni Lebanon
Jun 18, 2024 08:06Harakati ya Hizbullah ya Lebanon inatazamiwa kufanya mashambulizi ya kulipiza kisasi dhidi ya ngome za walowezi wa Kizayuni, baada ya kamanda mwingine mwandamizi wa kundi hilo la muqawama kuuawa shahidi kusini mwa Lebanon.