-
Amnesty International: Upanuzi wa Israel wa vitongoji vya walowezi katika Ukingo wa Magharibi ni changamoto dhahiri kwa sheria za kimataifa
Feb 28, 2026 06:02Shirika la Amnesty International limetangaza kwamba tangu mwezi Disemba mwaka jana, serikali ya Israel imezidisha harakati zake katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu huko Palestina, ikiwa ni pamoja na Quds Mashariki (Yerusalemu Mashariki), kupitia mfululizo wa maamuzi ambayo imesema yanalenga kuimarisha unyakuzi wa ardhi hiyo.
-
Iran yahimiza kusitishwa mapigano mara moja kati ya Afghanistan na Pakistan
Feb 28, 2026 05:30Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imezitaka Pakistan na Afghanistan kuketi kwenye meza ya mazungumzo haraka iwezekanavyo ili kusimamisha mapigano na kupunguza mvutano, huku mapigano ya mpakani kati ya nchi hizo mbili yakizidi kupamba moto.
-
OIC yaonya dhidi ya vitisho vya kuishambulia kijeshi Iran
Feb 28, 2026 02:25Kamati ya Utendaji ya Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imeonyesha wasiwasi wake kuhusu vitisho vya hivi karibuni dhidi ya Iran.
-
Israel yaendelea kuwazuia Wapalestina kuswali Masjidul Aqsa
Feb 28, 2026 02:19Jeshi la Israel jana lilipeleka idadi kubwa ya wanajeshi katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu, hasa katika vituo vya ukaguzi vinavyoelekea katika mji wa Quds (Jerusalem), sanjari na kuimarisha vizuizi dhidi ya Wapalestina waliotaka kuingia katika Msikiti wa al-Aqsa kwa ajili ya Swala ya Ijumaa ya pili ya mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
CPJ: Israel ndiyo iliyoua wanahabari wengine zaidi duniani 2025
Feb 26, 2026 05:24Utawala haramu wa Israel uliwaua wanahabari wasiopungua 84 mwaka wa 2025 - idadi kubwa zaidi kuliko dola lolote duniani katika mwaka uliokuwa mbaya zaidi kuwahi kurekodiwa kwa vyombo vya habari.
-
Intelijinsia ya Israel: Jeshi la Marekani linaweza kumudu mashambulizi dhidi ya Iran kwa siku kadhaa tu
Feb 25, 2026 09:05Maafisa wa ujasusi wa Israel wanakadiria kuwa Marekani inaweza kuendeleza mashambulio ya kijeshi kwa "siku nne hadi tano" pekee dhidi ya Iran ikiwa itaanzisha mashambulizi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu. Hii ni kwa mujibu wa ripoti mpya.
-
Afisa mwandamizi wa PLO asema, HAMAS si kundi la kigaidi, apinga mpango wa kuipokonya silaha
Feb 25, 2026 06:58Katibu Mkuu wa Kamati ya Utendaji ya Chama cha Ukombozi wa Palestina (PLO), Azzam al-Ahmad amesema, Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS si shirika la kigaidi na ameukataa wito wa kupokonywa silaha zake huku akibainisha kuwepo mipango ya kufanya mazungumzo kuhusu uwezekano wa harakati hiyo kujumuishwa katika PLO.
-
Ripoti: Israel iliwamiminia risasi, kuwaua wafanyakazi wa misaada Tel al Sultan, Gaza
Feb 25, 2026 02:26Karibu risasi elfu moja zilifyatuliwa na wanajeshi wa Israel katika mauaji ya kiholela dhidi ya wafanyakazi wa misaada huko Tel al-Sultan, Gaza, huku baadhi yao wakiuawa kwa kupigwa risasi kwa karibu, kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa hivi karibuni.
-
Iraq yamueleza mjumbe wa Marekani: Uundaji wa serikali ni 'suala letu la ndani'
Feb 24, 2026 11:52Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq, Fuad Hussein amesema, uundaji wa serikali mpya ya nchi hiyo ni "suala la ndani," ukiwa ni mjibizo uliotolewa wiki chache baada ya Marekani kutishia kufuta msaada na uungaji mkono wake kwa nchi hiyo ya Asia Magharibi.
-
Israel imepeleka Ghaza maboksi yenye mafuvu na miili iliyonyofolewa ya wanawake Wapalestina
Feb 24, 2026 11:15Mbunge wa kujitegemea, ambaye pia ni kiongozi wa zamani wa chama cha Leba nchini Uingereza Jeremy Corbyn, ametoa simulizi za kutisha zilizotokana na maelezo ya mkurugenzi wa Hospitali ya Al-Shifa katika Ukanda wa Ghaza uliozingirwa, zinazobainisha kwa undani jinsi utawala wa kizayuni wa Israel ulivyopeleka katika eneo hilo masanduku kadhaa yenye mafuvu ya vichwa na mabaki ya Wapalestina yaliyokatwakatwa.