Wabunge wa chama cha Democratic cha Marekani wamesema katika barua waliyomwandikia Rais Joe Biden wa nchi hiyo kwamba wanaamini kuna ushahidi wa kutosha wa kuthibitisha kwamba Israel imekiuka sheria za Marekani kwa kuzuia mtiririko wa misaada ya kibinadamu kwa watu wa Ukanda wa Gaza unaoendelea kushambuliwa kinyama na jeshi la utawala wa Kizayuni.
Ofisi ya Rais wa Russia jana Ijumaa ilishutumu kauli zilizotolewa na Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, kuhusu uwezekano wa Paris kuingia katika vita vya Ukraine, na kuzitaja kuwa ni "mwenendo hatari sana."
Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imetoa wito wa kusitishwa vitisho kwa wafanyakazi wa mahakama hiyo, ikisema kuwa vitisho hivyo vinaweza kuwa uhalifu dhidi ya mahakama hiyo inayoshughulikia uhalifu wa kivita.
Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO), limetoa tuzo yake ya mwaka kwa waandishi wa habari wa Gaza, kwa mnasaba wa Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani.
Huku maandamano ya wanafunzi wa vyuo vikuu vya Marekani yakiendelea kufanyika kwa lengo la kupinga jinai za utawala wa Kizayuni huko Gaza na vilevile kwa ajili ya kuwaunga mkono Wapalestina, polisi wa nchi hiyo wameongeza hatua zao za ukandamizaji dhidi ya wanafunzi hao.
Polisi wa kuzima ghasia nchini Marekani wameibomoa kambi ya wanafunzi wanaoandamana kwa amani kuunga mkono Palestina katika Chuo Kikuu cha California huko Los Angeles, siku moja baada ya wanafunzi hao kushambuliwa na wafuasi wanaounga mkono utawala haramu wa Israel.
Donald Trump mgombea anayetarajiwa kuteuliwa na chama cha Republican kuwania kkiti cha urais nchini Marekani amesema kuwa, akichaguliwa atarejesha tena marufuku ya kusafiri kwa baadhi ya nchi zenye Waislamu wengi katika siku ya kwanza ya utawala wake mpya.
Jumuiya kubwa ya kutetea haki za kiraia za Waislamu nchini Marekani imelishutumu Baraza la Wawakilishi (Congress) kwa kuidhinisha muswada wenye utata unapiga marufuku ukosoaji wowote dhidi ya Israel.
Mamlaka husika nchini Uingereza zimeanza kuwashikilia wahamiaji kama sehemu ya maandalizi ya kuwahamishia nchini Rwanda katika muda wa wiki 9 hadi 11 zijazo. Serikali ya London ilitangaza taarifa hiyo jana ikiashiria hatua muhimu katika mkakati wa uhamiaji unaotekelezwa na Waziri Mkuu Rishi Sunak.
Polisi wa kutuliza ghasia wa Ufaransa jana walikabiliana kwa mabavu na washiriki wa maandamano katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) katika mji mkuu wa nchi hiyo, Paris.