-
Kwa mara ya kwanza katika muongo mmoja, idadi ya wakimbizi duniani ilipungua mwaka 2025
Jun 12, 2026 04:41Kamisheni Kuu ya Wakimbizi ya Umoja wa Mataifa (UNHCR) imetangaza kwamba idadi ya watu waliolazimika kuhama makwao duniani kote ilipungua mwaka wa 2025, ikiwa ni mara ya kwanza kurekodiwa punguo kama hilo katika muongo mmoja, licha ya viwango vya juu vya wakimbizi wa muda mrefu.
-
Ni kosa kubwa... Blatter amkosoa Infantino na Marekani kuhusu mwamuzi wa Somalia FIFA 2026
Jun 12, 2026 04:32Wakati ambapo macho yote yameelekezwa kwenye viwanja vya mashindano ya Kombe la Dunia huko Marekani, Mexico na Canada, Mswizi Joseph Blatter, rais wa zamani wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), ameelekeza mishale ya hasira yake kwa mrithi wake Gianni Infantino na nchi mwenyeji mwenza Marekani, akiimbusha dunia kuwa "shujaa wa FIFA" anafuatilia mashindano hayo kwa uchungu.
-
Bei za mafuta zapanda duniani kutokana na ukiukaji wa usitishaji vita wa Marekani dhidi ya Iran
Jun 11, 2026 11:38Bei za mafuta ghafi ya petroli zilipanda Alhamisi duniani kufuatia kurejea kwa mashambulizi ya kijeshi baada ya uchokozi wa Marekani na ukiukaji wake wa makubaliano ya kusitisha mapigano na Iran. Mvutano huo umeongeza wasiwasi kuhusu usambazaji wa nishati duniani pamoja na kuendelea kwa usumbufu wa usafirishaji kupitia Mlango wa Hormuz.
-
Gazeti la NYT: Shambulio la Marekani dhidi ya miundombinu ya maji nchini Iran ni uhalifu wa kivita
Jun 11, 2026 11:09Gazeti mashuhuri la The New York Times limesema kuwa mashambulizi ya hivi karibuni ya Marekani dhidi ya miundombinu ya maji kusini mwa Iran yanaweza kuhesabika kama uhalifu wa kivita, kwani kulenga miundombinu ya kiraia ni kinyume kabisa na sheria za kimataifa.
-
Je, siasa zinapoingizwa michezoni, FIFA bado huwa ndiyo inayochukua maamuzi?
Jun 11, 2026 10:38Kombe la Dunia la mchezo wa kandanda, ambalo waasisi wake wamekuwa wakidai kuheshimu maadili na thamani za kimataifa pamoja na kutenganishwa siasa na mchezo huo, sasa limekuwa mateka wa siasa za mabavu na ubaguzi wa serikali ya Marekani, ambapo hata Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) lenyewe limeshindwa kutetea na kuwalinda maafisa wake mbele ya siasa hizo.
-
Guterres: Wafanyakazi 80 wa Umoja wa Mataifa waliuawa mwaka jana huko Gaza
Jun 09, 2026 11:46Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, ametangaza kwamba wafanyakazi 136 wa shirika hilo la kimataifa waliuawa wakitekeleza majukumu yao katika mwaka uliopita, wakiwemo wafanyakazi 80 waliokuwa wakifanya kazi katika Ukanda wa Gaza huko Palestina.
-
ICC yamsimamisha Kazi Mwendesha Mashtaka Mkuu kwa tuhuma za utovu wa nidhamu wa kingono
Jun 09, 2026 09:48Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imemsimamisha kazi Mwendesha Mashtaka Mkuu, Karim Khan, kwa madai ya utovu wa nidhamu wa kingono na msaidizi wake.
-
Lavrov: Guterres anashirikiana na Magharibi, Washington haina nia ya kurudi kwenye makubaliano ya Anchorage
Jun 09, 2026 04:18Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia, Sergey Lavrov amekosoa utendaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, akisisitiza haja ya kutekelezwa kanuni za Mkataba wa Umoja wa Mataifa "bila kubagua".
-
Vita dhidi ya Iran havikidhi vigezo vya “Vita vya Haki”, asema Papa Leo
Jun 08, 2026 03:15Katika kauli yenye ukali dhidi ya sera za Rais wa Marekani Donald Trump, Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani amesema kwamba vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran havina uhalali wa maadili.
-
Sanders: Netanyahu anashirikiana na Kongresi kuficha msaada wa kijeshi kwa Israel katika mikataba ya Pentagon
Jun 07, 2026 09:22Seneta wa kujitegemea kutoka Vermont, Bernie Sanders, ametangaza kwamba atapinga sheria inayochunguzwa bungeni ambayo itaongeza ushawishi wa Israel katika taasisi za kijeshi na viwanda vya Marekani.