-
Trump apinga wito wa Putin wa kurefusha muda wa Mkataba wa New START
Feb 06, 2026 06:22Rais wa Marekani, Donald Trump amepinga pendekezo la Rais wa Russia, Vladimir Putin la kuongezwa kwa khiari muda wa Mkataba wa New START, unaoweka mipaka ya silaha za nyuklia, ambao muda wake ulimalizika jana Alkhamisi.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Brazil: Uanzishwe mfumo mpya wa kimataifa kupitia marekebisho ya Umoja wa Mataifa
Feb 06, 2026 02:28Waziri wa Mambo ya Nje wa Brazil, Mauro Vieira, amesisitiza haja ya kuanzishwa mfumo mpya wa kimataifa unaotegemea marekebisho ya mashirika ya kimataifa yaliyopo, ikiwa ni pamoja na Umoja wa Mataifa, Baraza la Usalama la umoja huo na Shirika la Biashara Duniani.
-
UN: ISIS inasasisha mbinu zake na kuzidisha vitishio tangu katikati ya 2025
Feb 06, 2026 02:26Umoja wa Mataifa umetahadharisha kuhusu kile ulichokielezea kama ongezeko la vitishio vya kundi la Daesh (ISIS) tangu katikati ya mwaka jana, ukieleza kuwa kundi hilo limekuwa "tata zaidi".
-
Nchi wanachama Watetezi wa Mkataba wa UN zalaani hatua ya EU dhidi ya Iran
Feb 05, 2026 07:07Nchi wanachama wa Kundi la Marafiki Watetezi wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa zimetoa taarifa ambayo imelaani hatua ya hivi karibuni ya Umoja wa Ulaya dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Jeshi Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, IRGC.
-
Russia: Mkataba wa nyuklia wa New START baina yetu na US unamalizika leo Feb. 5
Feb 05, 2026 06:03Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imetangaza kuwa, Mkataba wa New START, unaoweka mipaka ya silaha za nyuklia kwa madola mawili makubwa zaidi duniani yanayomiliki silaha hizo, yaani nchi hiyo na Marekani unamalizika rasmi leo tarehe 5 Februari, na kwamba hadi sasa Moscow haijapokea jibu lolote rasmi kutoka kwa Washington kuhusu kuuongezea muda mpya mkataba huo.
-
Wasomi na wanafikra duniani watangaza kumuunga mkono Ayatullah Khamenei
Feb 05, 2026 02:35Kundi la wasomi, wanafalsafa na wanaharakati kutoka sehemu mbalimbali za dunia limetangaza kumuunga mkono Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Seyyed Ali Khamenei, pamoja na juhudi zake za ujasiri na zenye upeo mpana katika kulinda utu wa binadamu na haki.
-
Ripoti ya kila mwaka ya Human Rights Watch: Idadi ya mashahidi waliouawa Gaza inazidi makadirio rasmi
Feb 04, 2026 07:31Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limethibitisha katika ripoti yake ya kila mwaka iliyotolewa leo Jumatano kwamba katika mwaka mzima wa 2025 Israel ilifanya uhalifu wa kivita, uhalifu dhidi ya ubinadamu, vitendo vya mauaji ya kimbari na maangamizii ya kizazi dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi, na kusababisha vifo, majeraha na kuhamishwa kwa lazima mamia ya maelfu ya watu, kwa kushirikiana na Marekani.
-
Duru za Kimataifa: Israel inatumia mrengo wa kulia wa Ulaya kupiga vita Uislamu
Feb 04, 2026 07:20Vyombo vya habari vya kimataifa viimefichua uhusiano unaokua kati ya utawala haramu wa Israel na mrengo wa kulia barani Ulaya, hasa katika kupiga vita Uislamu na Waislamu katika nchi za bara hilo.
-
Waislamu waadhimisha siku ya kuzaliwa Mwokozi wa Akheri Zamani
Feb 04, 2026 04:27Waislamu wa madhehebu ya Shia katiika maeneo mbalimbali ya dunia Leo Jumatano mwezi 15 Shaaban wanaadhimisha kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa Imam wa Zama, Imam Mahdi AS, Imam wa 12 wa katika kizazi cha Mtume wetu Muhammad (SAW).
-
Russia yakosoa vitisho vya Marekani dhidi ya Iran yasema 'havikubaliki'
Feb 03, 2026 09:29Waziri wa Mambo ya Nje wa Ruussiia amesoa vitisho vya Marekani dhidi ya Iran akisema 'havikubaliki' huku Moscow ikitaka kupunguzwa mashinikizo ya Marekani dhiidi ya Iran.