-
Vyombo vya habari vya Uingereza: Athari mbaya za uchokozi wa Marekani na Israel dhidi ya Iran kwa maisha ya Wamarekani
Mar 31, 2026 02:57Gazeti la Uingereza la The Guardian limeandika katika ripoti yake kwamba vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran vimetoa mashinikizo makubwa kwa Wamarekani na kuongeza pakubwa gharama za maisha yao ya kila siku.
-
Vyombo vya habari vya Marekani: Uungaji mkono wa Yemen kwa Iran katika mashambulizi ya Marekani na Israel umeongeza bei ya mafuta duniani
Mar 31, 2026 02:48Tovuti ya CNBC imeandika kwamba uungaji mkono wa vikosi vya Yemen kwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika mashambulizo ya kichokozi ya Marekani na Israel dhidi yake na urushaji wa makombora wa Wayemen kuelekea Palestina inayokaliwa kwa mabavu umepelekea bei ya mafuta kuongezeka sana katika soko la kimataifa.
-
Uhispania yafunga anga yake kwa ndege zenye uhusiano na mashambulizi dhidi ya Iran
Mar 31, 2026 00:28Serikali ya Uispania imetangaza kufunga anga ya nchi hiyo kwa ndege zote za kijeshi zinazohusiana na mashambulizi dhidi ya Iran, kama ishara ya kupinga vita vinavyoongozwa na Marekani na Israel.
-
Senator Mdemocrat wa Marekani: Uwongo wa Trump ni ujumbe kwa Iran kuhusu namna alivyokwama
Mar 30, 2026 07:11Chris Murphy Seneta wa chama cha Democratic nchini Marekani amesema kuwa uongo wa Rais Donald Trump wa nchi hiyo kwamba anafanya mazungumzo na Iran unatoa ujumbe kwa Tehran kwamba amekwama kwenye kinamasi na amezongwa na mashinikizo.
-
Mamilioni ya Wamarekani waandamana kupinga vita vya Trump dhidi ya Iran
Mar 30, 2026 04:24Mamilioni ya Wamarekani wameandamana katika miji zaidi ya 50 kote Marekani mwishoni mwa juma kupinga uvamizi wa pamoja wa Marekani na Israel dhidi ya Iran, wakati mzozo huo ukiingia mwezi wake wa pili.
-
Papa Leo XIV audhihaki utawala wa Trump: Mungu hayuko pamoja na wapenda vita
Mar 29, 2026 09:12Papa Leo wa 14 amepinga majaribio ya kutaka kuhalalisha vita na mauaji kwa kutumia vibaya jina la Mungu, katika matamshi ambayo, kwa mujibu wa Televisheni ya CNN, yamerudi na kupinga madai yaliyotolewa na utawala wa Donald Trump.
-
Russia: Mashambulizi dhidi ya vituo vya amani vya nyuklia nchini Iran yanapaswa kulaaniwa kimataifa/Grossi achukue msimamo ulio wazi
Mar 29, 2026 03:06Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imesema mashambulizi mapya ya Ijumaa kwenye vituo vya amani vya nyuklia nchini Iran yanapasa kulaaniwa kimataifa. Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia amesema kuwa, mashambulizi mapya dhidi ya vituo vya amani vya nyuklia nchini Iran siku ya Ijumaa yanapasa kulaaniwa kimataifa, na kumtaka Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki kuwa na msimamo wa wazi na kubainisha bayana kwamba wavamizi wa Marekani na Wazayuni wamevuka mipaka.
-
Baraza la Haki za Binadamu la UN lalaani kwa kauli moja shambulio la Marekani na Israel dhidi ya shule Minab, Iran
Mar 28, 2026 07:52Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa (UNHRC) limelaani shambulio la Marekani na Israel dhidi ya Shule ya Shajareh Tayyebeh katika mji wa Minab, kusini mwa Iran, ambapo kwa uchache wanafunzi na wafanyakazi wa shule 175 waliuawa kikatili tarehe 28 Februari.
-
Russia: Uchokozi wa Marekani na Israel dhidi ya Iran unahusiana na rasilimali za nishati
Mar 28, 2026 04:42Maria Zakharova, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia, amesema kupitia taarifa akiashiria hujuma za kijeshi za Marekani na utawala wa Kizayuni dhidi ya Iran kwamba: "Sababu ya mashambulio dhidi ya nchi hii inahusiana moja kwa moja na tamaa ya madola ya kigeni ya kutaka kupora na kudhibiti rasilimali zake za mafuta na gesi."
-
Uungaji mkono wa mabunge ya CSTO kwa Iran dhidi ya uchokozi wa Marekani na Israel
Mar 28, 2026 04:37Baraza la Mabunge ya Jumuiya ya Makubaliano ya Usalama wa Pamoja (CSTO) limetoa taarifa ya pamoja likitangaza mshikamano wake na serikali pamoja na watu wa Iran katika kukabiliana na hujuma za kijeshi za Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel. Limesema: "Matumizi au tishio la nguvu dhidi ya nchi huru ni jambo lisilokubalika na kitendo hicho ni tishio kubwa kwa amani na usalama wa kimataifa."