-
Answarullah ya Yemen: Damu ya Jenerali Qasem Soleimani imeainisha njia ya kuhitimisha uwepo wa Marekani katika eneo
Jan 06, 2020 13:37Salim Al-Mughlis, Mjumbe wa Ofisi ya Kisiasa wa Harakati ya Wananchi ya Answarullah ya nchini Yemen amesema kuwa shahidi Qassem Soleimani ameainisha njia ya kuhitimisha uwepo wa Marekani katika eneo hili.
-
Mamilioni ya Wairani wauaga mwili wa Jenerali Qassem Soleimani na mashahidi wenzake
Jan 06, 2020 13:22Marasimu ya kuuaga mwili wa shahidi Qassem Soleimani, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu IRGC, yamefanyika kwa kuhudhuriwa na mamilioni ya watu mjini Tehran.
-
Korea Kaskazini yatoa radiamali yake kufuatia kuuawa kigaidi na Marekani Jenerali Soleimani
Jan 06, 2020 13:15Vyombo vya habari nchini Korea Kaskazini vimetoa radiamali kufuatia kuuawa shahidi na askari magaidi wa Marekani Luteni Jenerali Qassem Soleimani na kuitaja Washington kuwa muhusika mkuu wa ongezeko la mizozo katika eneo la Asia Magharibi.
-
Kiongozi wa kidini Pakistan ataka ulipizaji kisasi dhidi ya Marekani kwa damu ya Jenerali Soleimani
Jan 06, 2020 13:08Mmoja wa viongozi wakubwa wa kidini nchini Pakistan amesisitizia ulazima wa kulipizwa kisasi kwa damu iliyomwagwa na Marekani ya Luteni Jenerali Qassem Soleimani.
-
Sababu na taathira za mauaji ya kigaidi ya kamanda Qassem Soleimani kwa mtazamo wa Sayyid Hassan Nasrullah
Jan 06, 2020 11:12Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon, Sayyid Hassan Nasrullah amebainisha sababu, matokeo na taathira za jinai iliyofanywa na Marekani, ya kumuua kigaidi kamanda wa kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Luteni Jenerali Qassem Soleimani, Naibu Mkuu wa Al-Hashdu-Sha'abi ya Iraq Abu Mahdi Al-Muhandis pamoja na wanamuqawama wengine kadhaa; na akasisitiza kwamba, jinai hiyo ya Washington itapelekea kuanza historia mpya Asia Magharibi.
-
Kiongozi Muadhamu asalisha Sala ya Maiti ya Luteni Jenerali Soleimani na mashahidi wenzake + Video
Jan 06, 2020 08:16Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu leo asubuhi amesalisha Sala ya Maiti ya Luteni Jenerali Qassem Soleimani, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH na mashahidi wenzake waliouliwa kigaidi na Marekani nchini Iraq, usiku wa kuamkia Ijumaa ya tarehe 3 Januari 2020.
-
Rouhani: Inabidi tusimame imara katika kukabiliana na uingiliaji wa Marekani
Jan 06, 2020 08:15Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, usiku wa kuamkia leo amefanya mazungumzo ya simu na Rais Barham Salih wa Iraq na kusisitiza kuwa, ni jambo zito mno kwa mataifa makubwa ya Iran na Iraq kuweza kuvumilia mauaji ya kigaidi waliyofanyiwa Alhaj Qassem Soleimani, Abu Mahdi al Muhandis na wanamapambano wenzao waliokuwa wamefuatana nao.
-
Hatua ya kwanza nchini Iraq, mwanzo wa historia mpya magharibi mwa Asia
Jan 06, 2020 08:15Bunge la Iraq jana lilipasisha muswada wa kuwafukuza askari wa Marekani nchini humo. Hatua hiyo imechukuliwa baada ya wito uliotolewa na wananchi, wanasiasa na makundi mbalimbali ya Iraq baada ya jeshi la Marekani kumuua kigaidi Jemedari Qassem Solaimani na naibu kamanda wa kikosi cha kujitolea cha wananchi wa Iraq, al Hashdul Shaabi, Abu Mahdi al Muhandes.
-
Iran: Marekani ikitushambulia tutaingamiza Israel na kuifuta katika uso wa dunia
Jan 06, 2020 08:14Katibu wa Halmashauri ya Kuainisha Maslahi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika maombolezo ya kukumbuka kuuawa shahidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani; Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH kwamba, iwapo Marekani itatekeleza vitisho vinavyotolewa na Trump vya kuishambulia Iran, basi wawe na yakini kwamba miji ya Haifa na Tel Aviv na maeneo mengine muhimu ya Israel yataangamizwa kikamilifu na kusawazisha na ardhi.
-
Waziri Mkuu wa Iraq: Soleimani alikuwa mgeni wangu rasmi aliyekuja na ujumbe wa Saudi Arabia
Jan 06, 2020 08:13Kaimu Waziri Mkuu wa Iraq, Adel Abdul Mahdi amesema kuwa, Luteni Jenerali Qassem Soleimani alielekea nchini Iraq akiwa mgeni rasmi wa serikali na alikwenda na ujumbe wa Saudi Arabia kuhusu mazungumzo.