-
Ukosoaji wa Umoja wa Ulaya dhidi ya mpango wa Marekani wa 'Muamala wa Karne'
Feb 06, 2020 03:50Wiki moja baada ya Rais Donald Trump wa Marekani kuzindua mpango unaotajwa kuwa 'Muamala wa Karne,' kuhusiana na mzozo wa Palestina na utawala haramu wa Israel, Mkuu wa Siasa za Kigeni wa Umoja wa Ulaya ametoa taarifa akisema kuwa mpango huo unakinzana wazi na mikataba ya kimataifa na kutambua rasmi utawala wa Israel juu ya ardhi zilizoghusubiwa na utawala huo mwaka 1967.
-
Shamkhani: Muamala wa Karne ni mwendelezo wa uwepo wa Daesh kwa ajili ya kueneza chuki dhidi ya Uislamu
Feb 04, 2020 10:27Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema kuwa Muamala wa Karne ni mchezo wa Marekani na utawala haramu wa Kizayuni kwa lengo la kuendelea kuwepo kundi la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) kwa ajili ya kueneza chuki dhidi ya Uislamu.
-
Usama Hamdan: Muamala wa Karne ni sehemu ya njama za Marekani za kuiangamiza Palestina
Feb 03, 2020 23:11Mjumbe wa ngazi za juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amesisitiza kuwa, mpango wa Muamala wa Karne ni sehemu ya njama za Marekani zenye lengo la kuiangamiza kadhia ya Palestina na kuhalalisha uwepo wa utawala vamizi wa Israel katika Asia Magharibi.
-
Jumuiya ya Kukurubisha Madhehebu ya Kiislamu: Palestina ndio mpaka wa ulimwengu wa Kiislamu
Feb 02, 2020 23:37Katibu wa Jumuiya ya Kukurubisha Madhehebu ya Kiislamu amesema kuwa, Palestina ndio mpaka wa ulimwengu wa Kiislamu na kwamba suala la kuilinda na kuihami Palestina ni wajibu wa Kiqur'ani wa kila Muislamu.
-
Baraza la Mamufti wa Russia: Nchi za Kiislamu ziungane kupambana na "Muamala wa Karne"
Feb 01, 2020 23:11Mkurugenzi wa Baraza la Mamufti wa Russia ambacho ndicho chombo kikubwa zaidi ya Kiislamu nchini humo amesema kuwa, kuna wajibu wa nchi zote za Kiislamu kuungana na kuwa kitu kimoja ili kupambana na mpango wa Kimarekani-Kizayuni wa "Muamala wa Karne."