-
Russia yakanusha madai ya Marekani kwamba imeipatia Korea Kaskazini teknolojia ya makombora
Jan 18, 2019 12:08Balozi wa Russia nchini Korea Kaskazini amekanusha tuhuma za viongozi wa Marekani dhidi ya nchi yake kwamba Moscow imeipatia Pyongyang teknolojia ya makombora na kuongeza kwamba, tuhuma hizo ni za kuudhi kama ambavyo hazina msingi wowote.