-
Iran yalaani vitisho vya kijeshi vya wazi vya Trump; yalitaka Baraza la Usalama kuchukua hatua
Dec 31, 2025 23:13Iran imelaani rasmi vitisho "vikubwa na vya wazi" vya vita vya Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu uwezo wa kiulinzi na miraidi ya nyuklia ya nchi hii inayotekelezwa mwa malengo ya amani na kulitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kulaani vitisho hivyo.
-
Vitisho vipya vya Trump dhidi ya Iran; ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa na mkataba wa Umoja wa Mataifa
Dec 31, 2025 08:58Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu amesema kuwa, vitisho vya Trump dhidi ya Iran ni ukiukaji mkubwa wa sheria za kimataifa na Mkataba wa Umoja wa Mataifa.
-
Bunge la Iran lapongeza kurushwa kwa mafanikio satelaiti tatu katika anga za mbali
Dec 31, 2025 08:56Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) imepongeza kurushwa kwa satelaiti tatu zilizotengenezwa zilizotengenezwa na wataalamu wa hapa nchini, na kuitaja hatua hiyo kuwa mafanikio ya kihistoria katika mpango wa anga za mbali wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Rais Pezeshkian: Iran itatoa jibu kali na la kumjutisha adui
Dec 31, 2025 07:59Rais wa Iran amesisitiza kwamba, jibu la Jamhuri ya Kiislamu kwa uchokozi wowote litakuwa kali na litamfanya adui ajute.
-
Iran yajibu mapigo, yalitambua jeshi la majini la Canada kama shirika la kigaidi
Dec 30, 2025 23:29Iran imetangaza kulitambua Jeshi la Wanamaji la Canada kama shirika la kigaidi, ikijibu uamuzi wa huko nyuma wa Ottawa wa kuliorodhesha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) kama kundi la kigaidi, Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ilisema hayo jana Jumanne.
-
Velayati: Maadui walikosea sana kutweza nguvu za kijeshi za Iran
Dec 30, 2025 23:00Katibu Mkuu wa Majlisi ya Uamsho ya Kiislamu Duniani amesema kuwa, maadui wa Iran walikosea sana katika mahesabu yao juu ya nguvu za kijeshi za Jamhuri ya Kiislamu, kwani makombora yenye usahihi mkubwa ya Iran yalipenya safu nyingi za mifumo ya ulinzi na kupiga kwa usahihi shabaha zilizokusudiwa, na kubadilisha kikamilifu mlingano wa nguvu katika eneo la Magharibi mwa Asia.
-
Araghchi: Wananchi wa Venezuela watalinda uhuru wao mkabala wa uhalifu wa US
Dec 30, 2025 22:57Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi amesisitiza upinzani wa moja kwa moja wa Tehran dhidi ya hatua yoyote ya vitisho dhidi ya ardhi, uhuru na mamlaka ya kujitawala Venezuela, akisisitiza kuwa ana imani kuwa taifa hilo la Amerika Kusini litalinda uhuru wake.
-
Araqchi: Jenerali Soleimani alikuwa 'Mbunifu wa Mhimili wa Muqawama' Magharibi mwa Asia
Dec 29, 2025 08:21Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amemsifu shahidi na kamanda wa vita dhidi ya ugaidi, Luteni Jenerali Qassim Soleimani na kumtaja kuwa "mbunifu wa Mhimili wa Muqawama" katika eneo Magharibi mwa Asia.
-
Jeshi la Iran: Tupo katika hali bora zaidi kumkabili adui
Dec 29, 2025 06:23Jeshi la Iran limeonya kwamba, hatua yoyote ya uadui kutoka kwa maadui itakabiliwa na jibu kali, huku likisisitiza juu ya utayarifu wake wa kulilinda na kulihami taifa.
-
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Qatar wajadili matukio ya kikanda hasa hali ya Yemen
Dec 28, 2025 06:59Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Qatar wamezungumza kwa njia ya simu na kubadilishana mawazo kuhusu matukio ya kikanda hususan matukio ya karibuni huko Yemene. Wamesema kuwa ipo haja ya kulindwa mamlaka ya kujitawal ya ardhi nzima ya nchi hiyo.