-
Marandi: Matukio kuhusu Bolton na Salman Rushdie yanatia shaka
Aug 13, 2022 06:41Mshauri wa timu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika mazungumzo ya uondoaji vikwazo huko Vienna ameshangazwa na sadfa ya matukio mawili ya hivi karibuni huko Marekani, na kuashiria kuwa yumkini matukio hayo yanafungamana na mazungumzo ya kujaribu kuhuisha makubaliano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Russia yaonya juu ya uwezekano wa kuvunja uhusiano na Marekani
Aug 13, 2022 03:43Afisa mmoja katika wizara ya mambo ya nje ya Russia ameonya kuwa uhusiano wa nchi hiyo na Marekani unaweza ukafika kwenye "nukta isiyoweza kurudishika nyuma" na mbaya zaidi kuliko ya hivi sasa.
-
Iran: Marekani haiwezi kuficha jinai zake kwa kuibua madai bandia
Aug 12, 2022 21:02Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kitendo cha Marekani cha kuibua tuhuma na madai yasiyo na msingi wala mashiko yoyote hakiwezi kuficha wala kuhalalisha jinai za serikali ya Washington.
-
Bloomberg: China ina uwezo wa kuteketeza kwa muda mfupi ndege 900 za kivita za Marekani
Aug 12, 2022 21:01Jarida la Bloomberg linalochapishwa Marekani limeandika kuwa, endapo vitazuka vita baina ya Marekani na China kwa sababu ya Taiwan, Wachina wataweza kwa muda mfupi kuziangamiza ndege za kivita 900 za Marekani, yaani nusu ya uwezo wote wa kikosi cha anga cha nchi hiyo.
-
China: Marekani inataka vita vya Ukraine vichukue muda mrefu bila ya kumalizika
Aug 11, 2022 21:57Balozi wa China nchini Russia amesema kuwa, hatua ya Marekani ya kuendelea kumimina silaha huko Ukraine ni ushahidi tosha unaothibitisha kuwa hamu ya Washington ni kuona vita vya Ukraine vinachukua muda mrefu bila ya kumalizika.
-
Iran yajitenga na madai ya kijuba ya kutaka kumuua Bolton
Aug 11, 2022 02:54Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imepinga madai ya kiwendawazimu na yasiyo na msingi yaliyotolewa na serikali ya Washington ikidai kuwa raia mmoja wa nchi hii alikula njama ya kumuua John Bolton, mshauri wa zamani wa Usalama wa Kitaifa wa Ikulu ya White House ya Marekani.
-
Marekani yatiwa kiwewe na hatua ya Iran kurusha satalaiti anga za mbali
Aug 10, 2022 06:51Marekani imeghadhabishwa na hatua ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ya kurusha satalaiti katika anga za mbali kwa mafanikio, kwa kutumia roketi la Russia.
-
Russia: Kuondoka majeshi ya Marekani Syria kutarahisisha na kuharakisha kuangamizwa magaidi
Aug 10, 2022 03:14Mwakilishi wa kudumu wa Russia katika Umoja wa Mataifa amesema, kuondoka majeshi ya Marekani Syria kutarahisisha na kusahilisha kwa haraka zaidi kuangamizwa magaidi katika nchi hiyo.
-
Taiwan yadai kuwa China inataka kuivamia kijeshi
Aug 09, 2022 20:51Taipei imedai kuwa China inapanga njama ya kukivamia kisiwa cha Taiwan, baada ya Beijing kutangaza duru mpya ya mazoezi ya kijeshi katika maji ya kisiwa hicho, ukiwa ni muendelezo wa kujibu mapigo kwa ziara iliyofanywa na Spika wa Baraza la Wawakilishi la Marekani, Nancy Pelosi katika kisiwa hicho hivi karibuni.
-
China yamuwekea vikwazo Pelosi, yafuta baadhi ya ushirikiano na US
Aug 06, 2022 06:18China imetangaza kuwa itasimamisha ushirikiano na Marekani katika mambo kadhaa hasasi, ukiwa ni muendelezo wa kujibu mapigo kwa ziara iliyofanywa na Spika wa Baraza la Wawakilishi la Marekani, Nancy Pelosi katika kisiwa cha Taiwan hivi karibuni.