-
Hamas yaghadhabishwa na Google, Apple kuiondoa 'Palestina' katika ramani
Jul 01, 2021 03:10Ofisi ya Habari ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imekosoa vikali hatua ya mashirika ya Kimarekani ya Google na Apple ya kuliondoa neno 'Palestina' katika ramani zao za dunia. Kwa mujibu wa mashirika hayo, hivi sasa hakuna pahala duniani panapotambulika kama Palestina.
-
Viongozi wa Hamas, Jihad Islami wakutana, wasisitiza umoja wa Palestina
Jun 30, 2021 22:53Viongozi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) na Harakati ya Jihadi Islami ya Palestina wamekutana na kusisitiza ulazima wa kuimarisha na kudumisha umoja baina ya Wapalestina.
-
Ushirikiano wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina na Israel katika kuwakandamiza Wapalestrina
Jun 27, 2021 04:44Kuuawa shahidi mwanaharakati wa Kipalestina Nizar Banat mwenye umri wa miaka 42 na askari wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina kumeongeza mashinikizo dhidi ya mamlaka hiyo na mkuu wake Mahmoud Abbas, ambapo sasa Wapalestina wanataka malaka hiyo ivunjwe na Rais Mahmoud Abbas ajiuzulu.
-
Palestina yataka kuwekwa vikwazo vya kimataifa dhidi ya Israel
Jun 26, 2021 22:07Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Palestina imelaani uhalifu unaoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya raia wa Palestina na kutoa wito wa kuwekwa vikwazo vya kimataifa dhidi ya utawala huo.
-
Palestina, OIC zailaani Honduras kwa kuuhamishia ubalozi wake Quds
Jun 26, 2021 08:12Wizara ya Mambo ya Nje ya Palestina imekosoa vikali hatua ya serikali ya Honduras ya kuuhamishia ubalozi wake Quds Tukufu kutoka Tel Aviv.
-
Ismail Hania: Muqawama ni njia fupi zaidi kwa ajili ya kurejesha haki za Wapalestina
Jun 23, 2021 23:14Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) ambaye amefanya ziara nchini Mauritania amesisitiza juu ya ulazima wa kuendeshwa muqawama ikiwa njia fupi zaidi ya kufanikisha kupatikana haki za Wapalestina zilizoporwa.
-
Palestina yaikosoa UN kwa kutoiweka Israel katika orodha nyeusi ya wakiukaji wa haki za watoto
Jun 21, 2021 07:29Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Palestina imeukosoa Umoja wa Mataifa kwa kutoiweka Israeli kwenye orodha nyeusi ya kila mwaka ya makundi na nchi zinazohusika na ukiukaji mkubwa wa haki za watoto, ikisema kupuuza jinai za utawala huo kunawapa kinga ya kuhukumiwa Wazayuni wanaoua watoto.
-
Makundi ya muqawama ya Palestina yautahadharisha utawala wa Kizayuni
Jun 20, 2021 03:45Makundi ya muqawama ya Palestina yametangaza kuwa hayautauruhusu utawala ghasibu wa Kizayuni uutwishe muqawama masharti yake au kuufanya Ukanda wa Ghaza uwe katika hali ya kutengwa.
-
Shakhsia 682 wa kisiasa wataka Biden akomeshe dhulma za Israel
Jun 19, 2021 21:53Mamia ya shakhsia wa kisiasa, wanaakademia, wanaharakati wa amani na washindi wa Tuzo ya Nobel wamemtaka Rais Joe Biden wa Marekani atimize ahadi yake ya kulinda haki za Wapalestina, na kukomesha dhulma za Israel.
-
Wapalestina 160 wanateseka katika jela za Saudi Arabia hivi sasa
Jun 19, 2021 21:53Shirika la habari la "Palestine Today" limetangaza kuwa, sasa hivi kuna Wapalestina 160 wanaoteseka katika jela za ukoo wa Aal Saud nchini Saudi Arabia. Wapalestina hao wanashikiliwa kwenye jela hizo za Saudi Arabia kwa tuhuma za kuwa wanachama wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS.