-
Orban: Hungary haitaruhusu Ukraine kujiunga na EU miaka 100 ijayo
Jan 24, 2026 02:47Waziri Mkuu wa Hungary, Viktor Orban amesema kwamba Ukraine inajaribu kushawishi na kuathiri matokeo ya uchaguzi ujao wa bunge nchini Hungary, akisitiza kuwa nchi yake haitaruhusu Ukraine kujiunga na Umoja wa Ulaya katika miaka 100 ijayo.
-
Bunge la EU lasimamisha makubaliano ya biashara na US; kisa vitisho vya Trump
Jan 22, 2026 05:51Bunge la Ulaya limesimamisha rasmi mchakato wa kuidhinisha makubaliano yake ya kibiashara na Marekani, kutokana na vitisho vya Rais Donald Trump vya kutoza ushuru wa asilimia 10 kwa bidhaa za EU zinazoenda Marekani, iwapo umoja huo hautaafiki azma ya Washington ya kuitwaa Greenland.
-
"Haiwezi Tena Kuvumilika", asema Waziri Mkuu wa Ubelgiji akiitaka Ulaya iamue moja kuhusu Trump
Jan 21, 2026 10:39Waziri Mkuu wa Ubelgiji Bart De Wever amesema, ni lazima Ulaya imueleze wazi Rais wa Marekani Donald Trump kwamba hali ilipofikia hivi sasa "Haiwezi Tena Kuvumilika".
-
Russia: Badala ya Ulaya kuzungumzia hali ya Iran ifuatilie kuiokoa Greenland
Jan 15, 2026 10:27Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia, Maria Zakharova amesema, badala ya viongozi wa Umoja wa Ulaya, EU kutoa matamshi ya kuzungumzia hali ya Iran, ingekuwa bora kama wanegejikita kushughulikia kadhia ya Greenland, ambayo sasa hivi Marekani inafanya juu chini kuitia mkononi.
-
Mkuu wa zamani wa Sera za Nje wa EU: Ulaya iache kuifanya Marekani muitifaki wake mkuu
Jan 07, 2026 15:00Josep Borrell, mwanadiplomasia mkuu wa zamani wa Umoja wa Ulaya (EU) amesema, kambi hiyo inapaswa iache kuichukulia Marekani kama mshirika wake mkuu, huku Washington na Brussels zikiwa zinazozana hivi sasa kuhusu sera za kidijitali na udhibiti wa eneo la Greenland.
-
Baraza la Makanisa Duniani lataka kuwekewa vikwazo Israel kutokana na vita vya Gaza
Jan 02, 2026 02:48Baraza la Makanisa Duniani (WCC) limeutaka Umoja wa Ulaya (EU) kuiwekea Israel vikwazo vikiwemo vya silaha kutokana na mauaji ya kimbari yaliyofanywa na utawala wa Kizayuni huko Gaza, na ukiukaji wa haki dhidi ya Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan unaokaliwa kwa mabavu.
-
WHO: Unywaji wa pombe unaua watu 800,000 kila mwaka Ulaya
Dec 28, 2025 06:35Unywaji wa pombe unasababisha vifo vya watu zaidi ya 800,000 kila mwaka barani Ulaya, na kusababisha kifo kimoja kati ya kila vifo kumi na moja, kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Afya Duniani (WHO).
-
Nchi 14 zikiwemo za EU zalaani mpango wa ujenzi haramu Ukingo wa Magharibi
Dec 25, 2025 06:40Kundi la nchi 14 zikiwemo za Ulaya limetoa taarifa ya pamoja ya kulaani vikali uamuzi wa Israel wa kuanzisha ujenzi mpya wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan unaokaliwa kwa mabavu, na kuitaja hatua hiyo kuwa ni ukiukaji wa sheria za kimataifa.
-
Sambamba na kuanza tena chokochoko za Trump, EU yasema iko pamoja na Denmark, Greenland
Dec 23, 2025 11:18Umoja wa Ulaya umeonyesha mshikamano na Denmark na eneo la Greenland kufuatia tangazo la Rais wa Marekani Donald Trump la kuteua mjumbe wake maalumu katika eneo hilo.
-
Kikao cha Brussels na kurudi nyuma Ulaya inayosokotwa na tofauti za ndani, katika mpango wake wa unyang'anyi wa mali za Russia
Dec 21, 2025 02:39Licha ya viongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya kuandamwa na mashinikizo ya kisiasa ya Marekani ya kuwataka watoe msukumo wa kuvipatia suluhisho la haraka vita vya Ukraine, viongozi hao waliokutana kwenye makao makuu ya umoja huo mjini Brussels, wameamua kurudi nyuma na kulegeza msimamo katika uchukuaji uamuzi wenye gharama kubwa na hasi wa kunyakua mali za Russia,