-
Rais wa Senegal atangaza msamaha kwa kinara wa upinzani
Sep 30, 2019 07:33Rais Macky Sall wa Senegal ametangaza msahama kwa kiongozi wa upinzani nchini humo, Khalifa Sall ambaye alikuwa anatumikia kifungo cha miaka mitano jela tokea mwaka jana 2018 baada ya kupatikana na hatia katika kesi ya ufisadi iliyokuwa ikimkabili.
-
Kuendelea mazungumzo ya serikali ya Venezuela na wapinzani licha ya vitisho vya Wamagharibi
Jul 21, 2019 07:49Mashinikizo na vitisho vya Marekani na nchi za Ulaya dhidi ya Venezuela, vimeongezeka huku mazungumzo ya kutafuta njia ya kuiodoa nchi hiyo kwenye mgogoro wa kisiasa yakiwa yanaendelea kati ya serikali na wapinzani.
-
Wapinzani Sudan: Wanajeshi wasipewe kinga ya kushtakiwa
Jul 17, 2019 07:32Muungano mkuu wa upinzani nchini Sudan umepinga vikali mpango wa kuwapa wanajeshi wa nchi hiyo kinga mutlaki ya kushtakiwa, ukisisitiza kuwa waliohusika na vitendo vya jinai wanapaswa kubebeshwa dhima.
-
Sisitizo la wapinzani wa Venezuela la kuendelea kushiriki katika mazungumzo na serikali ya Caracas
Jul 17, 2019 02:30Baada ya duru tatu za mazungumzo baina ya serikali ya Venezuela na wapinzani yenye lengo la kufikia utatuzi wa pamoja na kuikwamua nchi hiyo katika kinamasi cha mgogoro wa kisiasa, wapinzani wa nchi hiyo wamethibitisha kwamba, wataendelea kushiriki katika mazungumzo na wawakilishi wa serikali huko nchini Barbados katika Bahari ya Caribbean.
-
Rais wa Venezuela asisitiza kuunga mkono mazungumzo na wapinzani
Jul 06, 2019 08:16Rais Nicolas Maduro wa Venezuela amesisitiza kuwa, serikali yake inaunga mkono na kuheshimu mchakato wa kuendelezwa mazungumzo na wapinzani wake kwa usimamizi wa Norway.
-
Mazungumzo baina ya serikali na wapinzani nchini Venezuela kuanza karibuni hivi
Jul 01, 2019 01:31Mazungumzo baina ya wawakilishi wa serikali na wapinzani nchini Venezuela yanatarajiwa kuanza hivi karibuni lengo likiwa ni kufanya juhudi za kuupatia ufumbuzi mgogoro wa nchi hiyo.
-
Wapinzani Sudan kuwateua watu 8 kuongoza Baraza la Mpito
Jun 11, 2019 08:19Makundi ya upinzani yanayoongoza maandamano na uasi wa kiraia nchini Sudan yanapanga kuteua watu wanane katika Baraza la Mpito, huku yakimteua mchumi mashuhuri nchini kuwa kiongozi wa serikali hiyo ya muda.
-
Ukwamishaji mambo wa Juan Guaidó kuhusu mgogoro wa kisiasa wa Venezuela
Jun 09, 2019 12:35Kuendelea mgogoro wa kisiasa nchini Venezuela na kadhalika kushindwa wapinzani wa nchi hiyo kumng'oa madarakani Rais Nicolás Maduro, kumepelekea Juan Guaidó, kiongozi wa upinzani kukubali pendekezo la upatanishi wa Norway na kuanza mazungumzo ya wawakilishi wa serikali na wapinzani huko mjini Oslo.
-
Viongozi watatu wa upinzani nchini Sudan watiwa mbaroni baada ya kukutana na Abiy Ahmed
Jun 09, 2019 03:31Jeshi la Sudan limewatia mbaroni viongozi watatu wa upinzani muda mfupi baada ya viongozi hao kukutana na Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed.
-
Wapinzani nchini Sudan wapinga mpango wa jeshi wa kukabidhi madaraka
Jun 04, 2019 13:30Wapinzani nchini Sudan wametangaza kuwa wanapinga mpango wa kukabidhi madaraka uliotangazwa na Baraza la Mpito la Kijeshi lililotwaa madaraka ya nchi baada ya kujiri maandamano yaliyompindua rais Omar al Bashir wa nchi hiyo mwezi Aprili mwaka huu.