-
Baqaei: Njia ya mawasiliano iko wazi kati ya Iran na Marekani ili kubadilishana jumbe
Jan 13, 2026 03:40Esmail Baqaei Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa njia ya mawasiliano iko wazi kati ya Abbas Aragchi Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Steve Witkoff Mjumbe Maalumu wa Marekani ili kubadilishana jumbe kila inapohitajika.
-
Uingiliaji kati wa Marekani nchini Iran; mfano wazi wa kuyumbisha usalama na kuhimiza vurugu
Jan 12, 2026 12:51Iran imeeleza malalamiko yake makali dhidi ya kauli za Marekani za uingiliaji kati katika barua yake kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Mamilioni ya Wairani washiriki maandamano ya kitaifa kulaani ghasia zinazoungwa mkono na Marekani, Israel
Jan 12, 2026 10:15Wairani kutoka makundi yote ya jamii wameanza maandamano ya kitaifa kulaani ghasia za karibuni zinazodaiwa kuungwa mkono na mataifa ya nje, wakionesha mshikamano wao na Jamhuri ya Kiislamu.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Hakuna taifa linaloweza kuvumilia ugaidi dhidi ya raia wake na majeshi yake
Jan 12, 2026 10:13Waziri wa Mambo ya Nje ya Iran, Abbas Araghchi, amelaani vikali mashambulizi ya kigaidi yanayochochewa na Marekani na Israel, ambayo yamekuwa yakiwalenga raia wa Iran pamoja na vikosi vya usalama. Amesisitiza kuwa hakuna nchi inayoweza kufumbia macho ukatili wa aina hiyo, ambao unavunja misingi ya utu na utulivu wa taifa.
-
IRGC yalaani uingiliaji wa wazi wa Trump katika masuala ya ndani ya Iran
Jan 12, 2026 10:11Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limelaani vikali ugaidi wa hivi karibuni katika ghasi za Iran sambam,ba na kumkosoa vikali Rais wa Marekani, Donald Trump kwa kuingia mausala ya ndani ya Iran.
-
Iran yatangaza siku tatu za kuwaomboleza waliouawa shahidi katika jinai zilizochochewa na US na Israel
Jan 12, 2026 06:39Serikali ya Iran imetangaza siku tatu za maombolezo kwa ajili ya kuwakumbuka waathiriwa, wakiwemo askari wa vikosi vya usalama na wa jeshi la kujitolea, ambao wameuliwa shahidi na wafanyaji fujo na vurugu wanaoungwa mkono na Marekani na utawala wa kizayuni wa Israel, waliojaribu kuteka nyara maandamano ya amani ya wananchi ya kulalamikia hali ya uchumi nchini.
-
Araghchi: Kuna ushahidi unaowahusisha magaidi wa Mossad na vurugu za mauaji zilizofanywa Iran
Jan 12, 2026 06:39Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Abbas Araghchi amesema, kuna ushahidi wa wazi unaohusisha vurugu za mauaji zilizofanywa hapa nchini na magaidi wenye mfungamano na shirika la ujasusi la utawala wa kizayuni wa Israel, Mossad.
-
Pezeshkian: Waliofanya fujo na machafuko Iran si wananchi; ni magaidi kutoka nje
Jan 12, 2026 03:15Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, adui amewaingiza Iran magaidi waliopewa mafunzo maalumu ya kigaidi ili kufanikisha malengo yake na kwamba waliofanya fujo, machafuko na uharibifu katika kona mbalimbali za Iran, si katika wananchi waliokuwa wanaandamana.
-
Baraza la Kulinda Katiba la Iran laitaka polisi kuchukua hatua kali dhidi ya wanaoibua ghasia
Jan 12, 2026 03:14Baraza la Kulinda Katiba la Iran limelaani vikali waibua ghasia na fujo ambao wameharibu mali za umma na kuvunjia heshima misikiti katika maeneo mbalimbali ya nchi, likizitaka taasisi za usalama na mamlaka husika kuchukua hatua zote muhimu kurejesha utulivu na sheria kufuatia matukio ya vurugu.
-
Kwa nini wananchi wa Iran hawana imani na vyombo vya habari vyenye uadui na Jamhuri ya Kiislamu?
Jan 12, 2026 02:40Wananchi wa Iran walio macho na ambao siku zote hujitokeza kwenye medani za harakati, kwa mara nyingine tena wamezima kwa umakini malengo maovu na njama chafu zilizoongozwa kwa ushirikiano wa utawala wa kizayuni na Marekani kupitia vyombo vya habari vyenye uadui na taifa hili.