-
Qalibaf: Iran hivi sasa inapigana vita na adui katika pande 4
Jan 11, 2026 10:58Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa: Leo tunapigana vita na adui wa Kizayuni na Marekani katika pande nne za kiuchumi, kiuelewa, kijeshi na kigaidi.
-
Waziri Araghchi aanika nafasi ya Marekani, Israel katika ghasia za Iran
Jan 11, 2026 06:55Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi amezionya vikali Marekani na utawala haramu wa Israel juu ya matokeo mabaya ya uchochezi na uungaji mkono wao kwa wafanya fujo na wazua rabsha hapa nchini, akisisitiza kuwa Washington na Tel Aviv zinataka kuyageuza maandamano ya kiuchumi ya wananchi wa Iran kuwa machafuko na ghasia.
-
Wairani kufanya maandamano kote nchini kupinga ghasia na fujo
Jan 11, 2026 06:36Baraza la Uratibu wa Uenezi wa Kiislamu la Iran limetangaza kuwa, wananchi Waislamu wa Jamhuri ya Kiislamu kesho Jumatatu watafanya maandamano katika pembe zote za nchi kulaani ghasia na fujo zilizochochewa hapa nchini na Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Rais Pezeshkian asisitiza azma ya Iran ya kutekeleza makubaliano yake na Oman
Jan 11, 2026 04:18Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza umuhimu wa kupanua na kuendeleza uhusiano na majirani na nchi za Kiislamu kama kipaumbele cha kimkakati cha Tehran.
-
Setilaiti ya kwanza ya rada ya Iran kuzinduliwa karibuni hivi
Jan 11, 2026 03:53Mkuu wa Shirika la Anga za Mbali la Iran ametangaza kuwa: Setilaiti ya kwanza ya rada ya Iran ambayo imebuniwa na kutengenezwa na Shirika la Anga za Mbali la Sairan la Iran itazinduliwa karibuni hivi.
-
Dakta Larijani: Mamluki wa Marekani na Israel wanahusika katika machafuko nchini Iran
Jan 10, 2026 12:11Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema kuwa, mikono ya Marekani na utawala wa Kizayuni katika matukio haya iko wazi na dhahiri.
-
Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran na Oman wasisitiza kuimarisha uhusiano wa nchi zao
Jan 10, 2026 12:11Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Oman wamesisitiza azma thabiti ya nchi zao ya kuimarisha na kupanua uhusiano wa nchi zao katika nyanja mbalimbali.
-
Marekani inahusika katika kugeuza maandamano ya amani kuwa machafuko nchini Iran
Jan 10, 2026 09:22Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Bw. Amir-Saeid Iravani katika Umoja wa Mataifa ameliandikia barua Baraza la Usalama la umoja huo akisema Marekani imeyageuza malalamiko na maandamano ya amani ya wananchi wa Iran kuwa ghasia na machafuko.
-
Balozi wa Iran UN: Marekani inahusika na machafuko ya sasa nchini Iran
Jan 10, 2026 04:58Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa ameliandikia barua Baraza la Usalama la umoja huo akisema Marekani imeyageuza maandamano ya amani ya wananchi wa Iran kuwa ghasia na machafuko.
-
Baraza la Usalama wa Taifa: Wafanya uharibifu watachukuliwa hatua bila ya kuonewa huruma
Jan 10, 2026 04:26Baraza la Usalama wa Taifa la Iran limetoa taarifa, -ambayo mbali na kuashiria kuwa tangu baada ya vita vya siku 12 Marekani na utawala wa kizayuni wa Israel hazijaacha kufanya chokochoko za vita na uadui dhidi ya taifa la Iran-, imesisitiza kwamba: taifa linaloheshimika la Iran litazivunja mbinu za kihujuma na ufanyaji uharibifu wa adui kwa umoja na mshikamano wa kitaifa.