-
Araghchi: Uhusiano wa Iran na Russia umeingia hatua mpya
Dec 18, 2025 03:05Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesema ushirikiano wa kimkakati kati ya Iran na Russia umeingia “hatua mpya na ya kasi zaidi” kufuatia kutiwa saini kwa ramani ya ushirikiano ya miaka mitatu pamoja na mwenzake wa Russia, Sergei Lavrov.
-
Mtafiti wa Iran ashinda dhahabu katika tamasha la uvumbuzi la Silicon Valley kwa dawa ya saratani
Dec 18, 2025 03:04Mtafiti mmoja kutoka Iran ametwaa medali ya dhahabu katika Tamasha la Kimataifa la Uvumbuzi la Silicon Valley (SVIIF) 2025 huko California, Marekani kufuatia utengenezaji wa dawa bunifu inayochangia katika matibabu ya saratani.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran awaonya mahasimu kutorudia makosa ya zamani
Dec 17, 2025 12:52Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesema vitisho vipya vya mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Iran ni sehemu kubwa ya vita vya kisaikolojia, akisisitiza kuwa majaribio ya awali ya kuitisha Iran kwa nguvu za kijeshi au vikwazo hayakuwahi kuzaa matokeo yaliyotarajiwa.
-
Maduro wa Venezuela aisifu Iran kama mfano wa kupigania utawala wa sheria kimataifa
Dec 17, 2025 12:50Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro, ameitaja Iran kuwa mfano bora duniani katika kutetea sheria za kimataifa, akishukuru Jamhuri ya Kiislamu kwa msimamo wake thabiti wa kuiunga mkono Caracas wakati ambapo vitisho kutoka Marekani vinaongezeka.
-
Kushtakiwa viongozi wa utawala wa Kizayuni; takwa la pamoja la mataifa ya Kiislamu
Dec 17, 2025 12:43Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amelaani jinai zinazoendelea kufanywa na Israel huko Ghaza na mashambulizi yake dhidi ya Lebanon, na amezitaka nchi za ukanda huu na jamii ya kimataifa ichukue hatua kali za kukabiliana na tishio la mara kwa mara la utawala wa Kizayuni dhidi ya amani na utulivu wa eneo hili na dunia nzima kwa ujumla.
-
Waziri wa Mambo ya Nje asisitizia tena azma ya Iran ya kutetea haki zake za kisheria za nyuklia
Dec 17, 2025 06:39Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Sayyid Abbas Araghchi amesisitizia azma ya Jamhuri ya Kiislamu ya kutetea haki zake za kisheria za nyuklia kulingana na Mkataba wa Kuzuia Usambazaji wa Silaha za Nyuklia (NPT), akisema sera za nyuklia za Tehran zingali zinaendana na mfumo wa sheria za kimataifa.
-
Qalibaf asisitiza umuhimu wa utafiti katika kutatua matatizo ya kitaifa
Dec 17, 2025 02:51Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza umuhimu wa utafiti katika kutatua changamoto na matatizo ya kitaifa.
-
Baghaei: Jamii ya kimataifa ichukue hatua dhidi Israel
Dec 16, 2025 11:46Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani jinai zinazoendelea kufanywa na Israel huko Ghaza na mashambulizi yake dhidi ya Lebanon, na amezitaka nchi za ukanda huu na jamii ya kimataifa ichukue hatua kali za kukabiliana na tishio la mara kwa mara la utawala wa Kizayuni dhidi ya amani na utulivu wa eneo hili na dunia nzima kwa ujumla.
-
Iran yaitaka dunia izuie kuendelea mauaji ya Wapalestina Gaza
Dec 16, 2025 06:49Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmail Baghaei, amelaani vikali kuendelea kwa mauaji ya halaiki ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, akiashiria mashambulizi ya mabomu yanayoendelea kufanywa na Wazayuni na kuzuiwa kwa misaada ya kibinadamu.
-
Mauzo ya chai ya Iran nje ya nchi yaongezeka kwa 48%
Dec 16, 2025 06:42Mkuu wa Shirika la Chai la Iran, Habib Jahansaz amesema mauzo ya chai ya Jamhuri ya Kiislamu nje ya nchi katika miezi minane ya kwanza ya mwaka huu wa kalenda ya Iran (ulioanza Machi 21) yameongezeka kwa asilimia 48, ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka jana.