-
Amir Abdollahian: Kuna ulazima wa jamii ya kimataifa kukabiliana ipasavyo na ugaidi
Jan 07, 2024 04:43Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Hossein Amir Abdollahian, amesitiza ulazima wa kufanyika juhudi kubwa zaidi za jamii ya kimataifa kwa ajili ya kukabiliana ipasavyo na ugaidi.
-
Ebrahim Raisi: Sera ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni kutetea madhulumu
Jan 07, 2024 01:02Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, siasa za Iran ni kuwatetea na kuwalinda wanaodhulumiwa na kupaza sauti dhidi ya madhalimu.
-
Magaidi wote waliohusika katika shambulio la Kerman wakamatwa
Jan 07, 2024 01:00Magaidi wote waliohusika katika shambulio la kigaidi la hivi karibuni katika mji wa Kerman kusini mashariki mwa Iran wamekamatwa.
-
Kikosi cha Wanamaji cha IRGC Iran chapokea meli mpya ya kivita yenye uwezo mkubwa kiteknolojia
Jan 06, 2024 07:31Kikosi cha Wanamaji cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) kimepokea zana mbalimbali za kijeshi zilizoundwa nchini ikiwa ni pamoja na meli ya kivita ya Abu Mahdi al-Muhandis ambayo ina teknolojia ya hali ya juu ya kukwepa rada.
-
Mtaalamu wa UN alaani vikali hujuma ya kigaidi katika mji wa Kerman
Jan 06, 2024 07:22Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya haki za binadamu nchini Iran Javaid Rehman amelaani vikali shambulio dhidi ya mjumuiko wa kumbukumbu ya kifo cha aliyekuwa kamanda wa ngazi za juu nchini Iran Shahidi Qassem Soleimani katika mji wa Kerman.
-
Ebrahim Raisi: Usalama wa ukanda huu mzima una deni kwa Luteni Jenerali Soleimani
Jan 06, 2024 03:22Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, usalama na amani iliyopo leo katika eneo hili inatokana na jihadi kubwa ya Luteni Jenerali Qassem Soleimani, Kamanda wa zamani wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH.
-
Iran yawakamata washukiwa kadhaa wanaohusishwa na hujuma ya kigaidi Kerman
Jan 05, 2024 23:39Waziri wa Mambo ya Ndani wa Iran Ahmad Vahidi ametangaza kukamatwa kwa washukiwa kadhaa wa shambulio la kigaidi la Januari 3 katika mji wa Kerman, ambapo watu 89 waliuawa shahidi na wengine wasiopungua 285 walijeruhiwa.
-
Iran inaitaka jamii ya kimataifa kuchukua hatua kali dhidi ya ugaidi
Jan 05, 2024 23:29Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Hossein Amir-Abdollahian amesema jamii ya kimataifa inahitaji kuchukua hatua kali ili kupambana na ugaidi.
-
Khatibu wa Swala ya Ijumaa Tehran: Kundi la kigaidi la Daesh ni chombo cha Marekani na Israel
Jan 05, 2024 11:52Khatibu wa Swala ya Ijumaa ya Tehran amezungumzia jinai ya kigaidi ya Kerman na kukiri kundi la kigaidi la ISIS au Daesh kuhusika na hujuma hiyo na kusema: ISIS ni chombo cha Marekani na utawala wa Kizayuni.
-
Iran yafanya mazishi ya pamoja ya wahanga wa ugaidi Kerman; yaahidi kuwasaka magaidi popote walipo
Jan 05, 2024 08:44Wananchi wa Iran leo Ijumaa wamefanya shughuli ya mazishi ya pamoja kwa wahanga wa miripuko miwili ya kigaidi iliyotokea Jumatano katika mji wa Kerman kusini mashariki mwa nchi huku kamanda wa ngazi ya juu wa Iran akiahidi kuwasaka magaidi popote walipo.