-
Iran yafanya mazishi ya pamoja ya wahanga wa ugaidi Kerman; yaahidi kuwasaka magaidi popote walipo
Jan 05, 2024 08:44Wananchi wa Iran leo Ijumaa wamefanya shughuli ya mazishi ya pamoja kwa wahanga wa miripuko miwili ya kigaidi iliyotokea Jumatano katika mji wa Kerman kusini mashariki mwa nchi huku kamanda wa ngazi ya juu wa Iran akiahidi kuwasaka magaidi popote walipo.
-
Raisi: Mamluki waliohusika na jinai ya kigaidi huko Kerman hawatakuwa na sehemu salama
Jan 05, 2024 08:39Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa hakuna uungaji mkono au msaada wowote kutoka nchi yoyote utakaowaacha salama vibaraka waliohusika katika jinai ya kigaidi huko Kerman.
-
Daesh yatangaza imehusika ya shambulizi la kigaidi Kerman, Iran
Jan 05, 2024 02:37Kundi la kigaidi la Daesh limedai kuhusika na milipuko miwili iliyoua watu 84 na kujeruhi wengine wengi katika kumbukumbu ya kamanda mkuu wa kupambana na ugaidi, Luteni Jenerali Qassem Soleimani katika mji wa Kerman, kusini mashariki mwa Iran.
-
IRGC: Shambulizi la kigaidi la Kerman limefeli kuyumbisha usalama Iran
Jan 04, 2024 23:44Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limesema shambulio la kigaidi lililoua makumi ya watu katika mji wa Kerman wa kusini mashariki mwa Iran ni jaribio lililofeli la kutaka kuvuruga na kuyumbisha usalama hapa nchini.
-
Spika: Shahidi Soleimani ni nembo ya umma wa Kiislamu
Jan 04, 2024 23:01Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema Luteni Jenerali Qassem Soleimani, aliyekuwa Kamanda Mkuu wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) hakuwa tu shakhsia wa kidini na kitaifa wa Iran, lakini pia alikuwa nembo ya umma wa Kiislamu.
-
Abdollahian: Tunafuata taratibu za kisheria na kimataifa kuhusu shambulio la kigaidi la Kerman
Jan 04, 2024 08:58Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema leo kuwa, wizara yake kwa kuzingatia data za awali zilizopatikana kutoka vyanzo rasmi, imeanza kuchukua hatua za haraka za kisheria na kimataifa kupitia Umoja wa Mataifa kuhusu tukio la kigaidi lililotokea jana katika mji wa Kerman.
-
Ugaidi, njama iliyoshindwa ya maadui dhidi ya Iran ya Kiislamu
Jan 04, 2024 08:31Maadui wa Iran ya Kiislamu kwa mara nyingine tena wamewaua shahidi na kuwajeruhi mamia ya raia katika kitendo cha kigaidi.
-
Raisi: Mauaji ya kigaidi hayatatizi umoja, usalama na stratejia ya taifa la Iran
Jan 04, 2024 03:15Rais Sayyid Ebrahim Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amezungumza kwa simu na mwenzake wa Uturuki na kueleza kuwa: Maadui wa taifa la Iran wanadhani kuwa kwa kustafidi na wenzo wa mauaji ya kigaidi wanaweza kufikia malengo yao haramu lakini taifa la Iran limethibitisha kuwa jinai za aina hiyo haziwezi kuvuruga umoja, usalama na stratejia ya taifa hili.
-
Waziri wa Mambo ya Ndani: Iran itatoa jibu kali na la haraka kwa mashambulizi ya kigaidi ya Kerman
Jan 04, 2024 03:04Waziri wa Mambo ya Ndani wa Iran amesema kuwa vikosi vya usalama na ulinzi vya nchi hii vitatoa jibu la haraka na kali kwa wahusika wa mashambulizi ya kigaidi yaliyoua watu zaidi ya 100 katika mji wa Kerman kusini mashariki mwa Iran.
-
Kiongozi: Watenda jinai watambue kuwa, wanamapambano wa njia ya Solaimani hawahimili jinai zao
Jan 04, 2024 00:02Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametoa ujumbe maalumu kufuatia kuuawa shahidi makumi ya wafanya ziara wa Shahid Qassem Soleimani na kusisitiza kuwa, wanaotenda jinai watambue kuwa wanamapambano wa njia ya Soleimani hawawezi kuhimili na kuvumilia jinai zao.