-
Jeshi la Israel lakiri askari wake 5 wameangamizwa, 14 wamejeruhiwa Ghaza
Jul 08, 2025 08:52Jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel limetangaza kuwa askari wake watano wameuawa na wengine 14 wamejeruhiwa katika mapigano kaskazini mwa Ukanda wa Ghaza.
-
Askari wa Israel aliyekuwa vitani Ghaza na Lebanon ajiua ndani ya gari lake
Jul 07, 2025 15:34Tovuti ya Kiebrania ya Walla imeripoti kuwa, mwanajeshi wa utawala wa Kizayuni Israel, Daniel Edri, amejiua kwa kujichoma moto ndani ya gari lake kwenye msitu karibu na eneo la Safed, kutokana na msongo mkali wa mawazo baada ya kuhudumu kwenye vita vya kinyama vya utawala huo dhidi ya Ghaza na Lebanon.
-
Umoja wa Mataifa waonya juu ya mgogoro wa njaa Gaza; misaada inaendelea kuzuiwa
Jul 07, 2025 08:31Ofisi ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa (OCHA) imeonya kwamba, mfumo wa chakula wa Gaza uko kwenye ukingo wa kuporomoka kabisa, huku hatua ya kuzuiwa msaada wa kibinadamu kuingia katika eneo hilo kukitishia maisha zaidi.
-
Hamas yakaribisha mwito wa BRICS wa kuondoka vikosi vya Israel huko Palestina
Jul 07, 2025 07:20Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas imekaribisha kwa mikono miwili wito wa kundi la nchi zinazoinukia kiuchumi BRICS kwa utawala haramu wa Israel, wa kukomesha vita vyake vya mauaji ya halaiki dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza, na kuondokaa kikamilifu katika eneo hilo la pwani lililozingirwa, na ardhi zote za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu.
-
Duru ya kwanza ya mazungumzo ya kusitisha vita Kati ya Hamas, Israel yagonga mwamba
Jul 07, 2025 04:03Duru ya kwanza ya mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja ya kusitisha mapigano kati ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas na utawala wa Kizayuni wa Israel, iliyofanyika nchini Qatar, imemalizika bila mafanikio yoyote, kwa mujibu wa vyanzo viwili vya Palestina vinavyofahamu majadiliano hayo.
-
Jeshi la Yemen lajibu mapigo kwa kushambulia maeneo kadhaa ya Israel
Jul 07, 2025 02:49Jeshi la Yemen limefanya mashambulizi mapya ya makombora katika maeneo mbali mbali ya Israel katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu, ili kulipiza kisasi cha mashambulizi ya anga ya utawala huo pandikizi dhidi ya nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Israel yaharakisha kuifanya kaskazini ya Ghaza ibaki bila wakazi kabla vita kusimamishwa
Jul 06, 2025 16:04Duru za kuaminika za Palestina zimeripoti kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel unaharakisha kuhawamisha wakazi wa kaskazini ya Ghaza ili eneo hilo libaki tupu kabla ya kusimamishwa vita endapo mwafaka utafikiwa.
-
Ansarullah: Katika Uislamu wa Imamu Hussein (AS), kujisalimisha hakuna nafasi
Jul 06, 2025 15:03Kiongozi wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema, katika Uislamu wa Imamu Hussein (AS), kujidhalilisha na kusalimu amri hakuna nafasi hata chembe.
-
Sheikh Naim Qassem: Chaguo letu ni njia ya Imam Hussein, si udhalilifu na kusalimu amri
Jul 06, 2025 11:47Katibu Mkuu wa Hizbullah Sheikh Naim Qassem ametangaza kuwa, watu wa Lebanon kamwe hawatakubali kudhalilishwa au kusalimu amri mbele ya adui mzayuni, na kwamba njia yao itaendelea kubaki kuwa ya Imam Hussein iliyokita mizizi katika heshima, kutokubali kudhalilishwa na kujitolea muhanga.
-
Ben Gurion yafungwa tena kutokana na shambulio la kombora la Yemen
Jul 06, 2025 10:57Mamlaka ya anga ya Israel imesitisha safari zote za ndege za kuwasili na kuondoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Ben Gurion na kusema kuwa kituo hicho kitaendelea kufungwa "kwa muda usiojulikana" baada ya Vikosi vya Wanajeshi wa Yemen kufanya shambulio la kombora, kulipiza kisasi vita vya mauaji ya halaiki vinavyoendelea vya utawala wa Tel Aviv dhidi ya Wapalestina huko Gaza.