-
Ben Gurion yafungwa tena kutokana na shambulio la kombora la Yemen
Jul 06, 2025 10:57Mamlaka ya anga ya Israel imesitisha safari zote za ndege za kuwasili na kuondoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Ben Gurion na kusema kuwa kituo hicho kitaendelea kufungwa "kwa muda usiojulikana" baada ya Vikosi vya Wanajeshi wa Yemen kufanya shambulio la kombora, kulipiza kisasi vita vya mauaji ya halaiki vinavyoendelea vya utawala wa Tel Aviv dhidi ya Wapalestina huko Gaza.
-
Sababu za Marekani na Israel kuwapiga risasi Wapalestina kwenye safu za misaada huko Gaza
Jul 05, 2025 22:55Wakandarasi wa usalama wa Marekani wanatumia risasi za moto, maguruneti, na gesi ya kuwasha dhidi ya raia katika vituo vya usambazaji wa misaada ya kibinadamu katika Ukanda wa Gaza.
-
Israel yaua shahidi Wapalestina 64 katika Ukanda wa Gaza
Jul 05, 2025 11:55Mashambulizi ya Israel yamesababisha kuuawa shahidi Wapalestina 64 katika maeneo mbalimbali ya Ukanda wa Gaza tangu alfajiri ya leo Jumamosi, huku makumi ya waliouawa wakitambuliwa kama waombaji misaada, kwa mujibu wa ripoti kutoka hospitali za eneo hilo lililozingirwa.
-
Hamas yaonya, Msikiti wa al-Aqsa ni mstari mwekundu wa Muqawama
Jul 05, 2025 11:55Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas imeonya kuwa, Msikiti wa al-Aqsa ni "mstari mwekundu," na kuahidi kulinda eneo hilo takatifu dhidi ya mashambulizi ya mara kwa mara ya utawala wa Israel na uvamizi wa walowezi wa Kizayuni.
-
Hizbullah: Muqawama nchini Lebanon kamwe hautasalimu amri
Jul 05, 2025 11:52Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon, Sheikh Naim Qassem amepinga mwito wa serikali ya Beirut wa kuweka chini silaha kundi hilo la Muqawama na kusema kuwa, "sisi si watu wa kusalimu amri."
-
Bidhaa za Israel zasusiwa katika maduka ya nchi za Ulaya
Jul 05, 2025 11:52Maduka makubwa katika nchi kadhaa za Ulaya yameacha kuuza bidhaa za Israel ili kujibu ghadhabu za wanunuzi za bidhaa hizo kutokana na vita vya utawala wa Kizayuni dhidi ya Gaza.
-
Askari wapatao 40 wa Israel waangamizwa na kujeruhiwa katika mzingiro Ghaza
Jul 05, 2025 03:59Kamanda mwandamizi wa Sarayal-Quds, tawi la kijeshi la Harakati ya Jihadul-Islami ya Palestina ametangaza kuwa, askari wapatao 40 wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel wameuawa au kujeruhiwa katika operesheni ya kijeshi iliyoratibiwa na wapiganaji wa Muqawama mashariki ya Ghaza.
-
Barua ya siri ya Trump itairuhusu Israel kuanzisha vita tena Ghaza hata vikisitishwa
Jul 05, 2025 03:55Ripoti za kuaminika zilizotolewa na duru za habari zinasema, utawala wa Kizayuni wa Israel unamtaka rais Donald Trump wa Marekani aupe hakikisho kuwa utaruhusiwa kuanzisha tena vita na mauaji ya kimbari Ghaza ikiwa matakwa yake hayatatekelezwa, hata kama mazungumzo ya usitishaji vita kwa muda wa siku 60 yatakuwa yanaendelea.
-
Nafasi ya Uingereza katika vita vya Gaza yamulikwa; Mashinikizo yashtadi kwa ajili ya kufanyika uchunguzi
Jul 05, 2025 00:46Huku idadi ya Wapalestina wanaouawa shahidi ikiongezeka huko Gaza, mashinikizo ya kuitaka serikali ya Uingereza kufanya uchunguzi huru kuhusina na mchango wa nchi hiyo katika vita vya Gaza yanazidi kuongezeka.
-
UNRWA: Watu wa Gaza wanazirai mitaani kwa sababu ya njaa
Jul 04, 2025 11:53Shirika la Umoja wa Mataifa la Misaada kwa Ajili ya Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) limetangaza leo Ijumaa kwamba Ukanda wa Gaza unasumbuliwa na hali mbaya na kwamba njaa imekithiri katika eneo hilo, na watu wanazimia barabarani kutokana na njaa kali.