-
Yemen yashambulia Meli za Uingereza katika Bahari Nyekundu
Apr 27, 2024 04:50Shirika la Operesheni za Baharini la Uingereza (UKMTO) lilitangaza jana Ijumaa, kwamba meli yake karibu na pwani ya Yemen imelengwa na kuharibiwa kwa takribani makombora mawili.
-
Kufuatia jinai za Israel, Gaza inahitaji miaka 14 kutegua mabomu na kuwa salama
Apr 27, 2024 04:34Kwa muda wa karibu miezi saba sasa, utawala katili wa Israel umekuwa ukidondosha mabomu kila siku katika Ukanda wa Gaza na sasa Umoja wa Mataifa unasema zoezi la kutegua mabomu ambayo hayajalipuka eneo hilo linaweza kuchukua muda miaka 14.
-
Mbali na walionyofolewa viungo, Wapalestina wengine walizikwa wakiwa hai kwenye makaburi ya halaiki Ghaza
Apr 26, 2024 23:17Wahudumu wa afya, timu za uokoaji na mashirika ya kutetea haki za binadamu yanawashutumu askari vamizi wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kuwanyofoa viungo Wapalestina na hata kuwazika baadhi yao wakiwa hai kwenye makaburi ya halaiki yaliyogunguliwa kwenye eneo la karibu na Hospitali ya Nasser huko Ukanda wa Ghaza, baada ya askari hao katili kuondoka katika eneo hilo Aprili 7 kufuatia mashambulizi ya ardhini ya miezi minne.
-
Hamas: Miili ya makaburi ya umati Gaza ifanyiwe uchunguzi
Apr 26, 2024 23:17Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imetoa wito wa kutumwa timu za uchunguzi ili kutambua miili iliyogunduliwa kwenye makaburi ya halaiki katika Ukanda wa Gaza.
-
Vikosi vya Yemen vyashambulia meli ya Israel, Bandari ya Eilat kuonyesha mshikamano na Gaza
Apr 26, 2024 04:11Vikosi vya Wanajeshi wa Yemen vimefanikiwa kulenga meli ya utawala wa Israel katika Ghuba ya Aden pamoja na Bandari ya Eilat katika sehemu ya kusini ya maeneo yanayokaliwa kwa mabavu (Israel) katika operesheni mpya zinazoiunga mkono Palestina.
-
Amir-Abdollahian: White House inapasa kusitisha haraka uungaji mkono wake kwa jinai za kivita za Israel
Apr 25, 2024 23:39Akikosoa ukandamizaji na unyanyasaji wa askari usalama vya Marekani dhidi ya wahadhiri na wanafunzi wanaopinga jinai za kivita za utawala ghasibu wa Israel, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema: Ikulu ya Marekani inapasa kusitisha haraka iwezekanavyo uungaji mkono wake kwa jinai za kivita za utawala ghasibu wa Israel.
-
UN: Hatuwezi kuwaambia Wapalestina wasubiri misaada
Apr 25, 2024 23:36Jumuiya ya kimataifa ina jukumu na wajibu wa kufanya kazi kufanikisha kukwamua Gaza lakini hatuwezi kuwaambia raia Wapalestina wanaoteseka wasubiri, amesema afisa wa Umoja wa Mataifa anayehusika na ufikishaji wa misaada kwenye eneo hilo linalokabiliwa na mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na utawala haramu wa Israel.
-
Hizbullah: Tumeua na kujeruhi askari 2,000 wa Israel katika operesheni 1,650 tangu vilipoanza vita vya Ghaza
Apr 25, 2024 08:46Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon imesema imeua na kujeruhi zaidi ya wanajeshi 2,000 wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika operesheni zake 1,650 ilizotekeleza katika maeneo yanayokaliwa kwa mabavu tangu kuanza kwa vita vya mauaji ya kimbari vya utawala huo katika Ukanda wa Ghaza.
-
Afrika Kusini yataka uchunguzi wa haraka kuhusu makaburi ya halaiki Ukanda wa Gaza
Apr 25, 2024 04:02Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Afrika Kusini imetoa mwito wa kufanyika uchunguzi wa haraka na wa kina kuhusu makaburi ya umati yaliyogunduliwa katika Ukanda wa Gaza.
-
Maandamano dhidi ya Netanyahu yageuka kuwa ya ghasia
Apr 25, 2024 03:57Maandamano ya kupinga baraza la mawaziri la Benjamin Netanyahu huko Tel Aviv yageuka kuwa ya ghasia na vurugu kali.