-
Miili 10,000 iliyozikwa chini ya vifusi vya Gaza, inaoza na kueneza magonjwa
May 01, 2024 00:33Shirika la Ulinzi wa kiraia la Gaza limeonya kuhusu maafa ya kiafya yanayokuja katika Ukanda uliozingirwa kutokana na kuoza maiti zilizo chini ya vifusi vya majengo yaliyoharibiwa na mashambulizi ya mabomu ya utawala katili wa Israel.
-
Kukaribia muda wa kutolewa hukumu ya mahakama mbili za kimataifa dhidi ya utawala wa Kizayuni
Apr 30, 2024 22:53Sambamba na kuongezeka uwezekano wa Mahakama ya Kimataifa ya Haki ICJ kutoa hukumu ya kukamatwa maafisa kadhaa wa utawala wa Kizayuni kwa tuhuma za kufanya jinai za kivita huko Gaza, gazeti la Times lilimeandika kuwa, kuna uwezekano pia kwamba Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC inajiandaa kutoa hati ya kukamatwa Netanyahu na maafisa wengine wa ngazi za juu wa Israel akiwemo Waziri wa Vita, Mkuu wa Majeshi na baadhi ya maafisa wa usalama wa utawala huo kwa kuhusika na vita hivyo.
-
Ujumbe wa Hamas umeondoka Cairo kwa ajili ya mashauriano zaidi
Apr 30, 2024 07:42Ujumbe wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) umeondoka Cairo, mji mkuu wa Misri ili kufanya mashauriano zaidi kuhusu pendekezo jipya lililotolewa kwa ajili ya kubadilishana mateka.
-
Vituo vya utafiti vya Ulaya vyaiunga mkono Palestina na kuiwekea vikwazo Israel
Apr 30, 2024 07:41Vituo vya utafiti barani Ulaya vimeuwekea vikwazo utawala wa Kizayuni na kuunga mkono malengo ya Palestina. Viituo hivyo vya utafiti vya Ulaya pia vimelaani jinai za utawala huo unaotekeleza mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Gaza.
-
Balozi zote za Israel zawekwa kwenye hali ya tahadhari kuhofia waranti wa ICC wa jinai za vita vya Ghaza
Apr 29, 2024 23:17Wizara ya Mambo ya Nje ya utawala wa Kizayuni wa Israel imeziagiza balozi zake duniani kote kuwa tayari kwa madhara yanayoweza kutokea iwapo Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) itatoa waranti wa kukamatwa maafisa wa utawala huo kwa uhalifu wa kivita na ukiukaji wa haki za binadamu dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza.
-
Wapalestina zaidi ya 8,500 wametiwa nguvuni Ukingo wa Magharibi tangu Oktoba 7 hadi sasa
Apr 29, 2024 23:16Jumuiya ya kushughulikia mateka wa Kipalestina imetangaza katika ripoti yake kwamba utawala ghasibu wa Kizayuni wa Israel umewatia nguvuni Wapalestina 8,505 katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan tangu tarehe 7 Oktoba 2023 mara baada ya kutekelezwa operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa.
-
Kuharibiwa Gaza; Jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya kizazi cha sasa na kijacho
Apr 29, 2024 23:14Mwezi wa saba wa vita unamalizika tangu utawala wa Kizayuni uanzishe vita na mauaji ya kimbari dhidi ya Ukanda wa Gaza, huku mashambulizi ya kila siku ya utawala huo yakisababisha maafa na uharibifu mkubwa wa miundombinu ya mji na afya katika ukanda huo.
-
Wanajeshi 14 wa Israel waangamizwa, wajeruhiwa katika operesheni ya muqawama Gaza
Apr 29, 2024 07:49Takriban wanajeshi watatu wa utawala katili wa Israel wameangamizwa na wengine 11 kujruhiwa vibaya katika eneo la vita kati kati mwa Ukanda wa Gaza, huku vikosi vya muqawama au mapambano ya Kiisalmu Palestina vikiendelea kulisababishia hasara kubwa jeshi katili la utawala huo.
-
UNRWA: Takriban watoto 17,000 wametenganishwa na familia zao Gaza kufuatia vita vya Israeli
Apr 29, 2024 07:33Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) limebainisha wasiwasi wake juu ya hali inayozidi kuzorota ya watoto wa Kipalestina katika Ukanda wa Gaza, huku Israel ikiendeleza vita vyake vya mauaji ya kimbari dhidi ya eneo hilo linalozingirwa.
-
Rais wa Syria: Mshikamano wa nchi za Kiarabu unapelekea kupatikana utulivu katika eneo
Apr 28, 2024 23:36Rais wa Syria amesema kuwa kuwepo mshikamamo baina ya nchi za Kiarabu na kutekeleza hatua za pamoja kutapelekea kupatikana amani na uthabiti katika eneo.