-
Kuendelea jinai za Israel: Unyakuzi mkubwa zaidi wa ardhi za Ukingo wa Magharibi tangu 1993
Mar 26, 2024 09:02Licha ya kuwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limetangaza kuwa mpango wa Israel wa kupanua vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu ni kinyume cha sheria, lakini katika hatua mpya, utawala unaokalia kwa mabavu Quds Tukufu umenyakua ardhi ya hekta 800 katika Bonde la Jordan kwenye Ukingo wa Magharibi kwa ajili ya ujenzi wa mamia ya nyumba za walowezi.
-
Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa: Israel inatekeleza vitendo vya mauaji ya kimbari Gaza
Mar 26, 2024 07:16Mtaalamu wa haki za binadamu katika Umoja wa Mataifa amesema kuna sababu za msingi za kuthibitisha kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel unatekeleza mauaji ya kimbari na ya kizazi katika mashambulizi yake dhidi ya Gaza.
-
Kambi ya Muqawama yawakosoa waungaji mkono wa jinai na uhalifu wa Israel
Mar 25, 2024 23:25Baraza Kuu la Kisiasa la Yemen na Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) zimekosoa uungaji mkono na himaya kubwa ya Marekani kwa utawala wa Kizayuni wa Israel na kimya cha viongozi wa nchi za Kiislamu kuhusiana na jinai zinazofanywa na utawala huo ghasibu.
-
Al-Azhar: Hatua za kimataifa mkabala wa jinai za Israel Ukanda wa Gaza zinakatisha tamaa
Mar 25, 2024 08:05Imamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Al Azhar cha Misri amesema kuwa radiamali za jamii ya kimataifa mkabala wa vita vya Israel dhidi ya Gaza zinakatisha tamaa.
-
'Siku ya Kimataifa ya Quds ni siku ya kutangaza mshikamano na Wapalestina'
Mar 25, 2024 02:43Mwanaharakati mmoja na mtafiti wa Chuo Kikuu raia wa Nigeria amewataka wananchi wa nchi za Afrika wajitokeze kwa wingi kwenye maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Quds ambayo ni Ijumaa ya mwisho ya mwezi huu mtukufu wa Ramadhani akisisitiza kuwa hiyo ni siku ya kutangaza uungaji mkono kwa wananchi madhlumu wa Palestina wanaofanyiwa ukatili wa kutisha na Israel.
-
Saraya Al-Quds yaangamiza Afisa mmoja na wanajeshi 3 wa Israel katika shambulizi la kuvizia huko Tulkarm
Mar 24, 2024 22:42Brigedi za al Quds (Saraya al Quds) Batalioni ya Tulkarm imetangaza kuwa wanachama wake wamevamia gari lililokuwa na afisa mmoja na wanajeshi watatu wa Israel kaskazini mwa Tulkarm katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na kuwaangamiza wote.
-
Shahidi: Wanajeshi wa Israel wamewabaka wanawake wa Kipalestina kabla ya kuwaua katika Hospitali ya al-Shifa
Mar 24, 2024 22:41Mwanamke wa Kipalestina amesimulia matukio ya kutisha baada ya wanajeshi wa Israel kuvamia Hospitali ya al-Shifa katika mji wa Gaza wiki iliyopita, na kusema kuwa wanajeshi wa utawala huo ghasibu wanawabaka wanawake wa Kipalestina kabla ya kuwaua.
-
Kufeli propaganda dhidi ya Hamas na kuongezeka umaarufu wa harakati hiyo huko Gaza
Mar 24, 2024 22:39Licha ya kuenea propaganda sumu za vyombo vya habari vya Magharibi na baadhi ya nchi za Kiarabu, lakini kura za uchunguzi wa maoni zinaonyesha kuwa wakazi wengi wa Ukanda wa Gaza wanaridhishwa na utendaji wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu wa Palestina (Hamas).
-
Hamas yalaani kimya cha dunia kuhusu uvamizi wa Israel kwenye hospitali ya al-Shifa ya Gaza
Mar 24, 2024 07:55Harakati ya Mapambano ya Kiislamu (muqawama) ya Palestina, Hamas, imelaani vikali jamii ya kimataifa kwa "ukimya wake wa aibu" juu ya uvamizi wa jeshi la utawala wa Israel dhidi ya hospitali ya al-Shifa ya Gaza ambako maelfu ya Wapalestina waliokimbia makwao wanapata hifadhi.
-
Jeshi la Anga la Syria latungua makombora ya Israel karibu na Damascus
Mar 24, 2024 07:35Vikosi vya ulinzi wa anga vya Syria vimefanikiwa kutungua makombora mengi yaliyovurumishwa na jeshi la Israel karibu na mji mkuu wa nchi hiyo Damascus.