-
Abbas: Utawala wa Kizayuni umeangamiza asilimia 75 ya Ukanda wa Gaza
Apr 28, 2024 23:07Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina amesema kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel umeangamiza asilimia 75 ya nyumba, miundombinu ya barabara, vyuo vikuu, misikiti na miundo msingi mingine ya Ukanda wa Gaza.
-
Viongozi wa makundi ya Palestina wakutana Istanbul, Uturuki kujadili yanayojiri Ghaza
Apr 28, 2024 08:23Viongozi wa Harakati za Hamas, Jihadul-Islami na Vuguvugu la Wananchi la Ukombozi wa Palestina wamekutana kujadili yanayojiri kwenye medani za mapambano na za kisiasa za Palestina na vita katika Ukanda wa Ghaza.
-
Uwezekano wa ICC kutoa waranti wa kukamatwa Netanyahu kwa mauaji ya Ghaza umeitia tafrani Israel
Apr 28, 2024 08:15Baraza la mawaziri la utawala haramu wa Kizayuni wa Israel limeingiwa na tafrani na wasi wasi mkubwa juu ya uwezekano wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) kutoa waranti wa kukamatwa waziri mkuu wa utawala huo Benjamin Netanyahu na maafisa wengine waandamizi kwa kuhusika na jinai za vita vya miezi kadhaa vya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Ghaza uliozingirwa.
-
Kushadidi mgogoro wa kisiasa katika baraza la mawaziri la utawala wa Kizayuni
Apr 28, 2024 07:22Kuendelea maandamano ya mitaani huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu (Israel), tofauti za kimtazamo kati ya wapinzani na baraza la mawaziri na kuongezeka uwezekano wa Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu kutoa amri ya kumkamata Benjamin Netanyahu kumezidisha mzozo wa kisiasa huko Tel Aviv.
-
Wapalestina 37 wauawa shahidi katika mashambulio ya Israel huko Gaza
Apr 28, 2024 03:50Wapalestina 37 wameuawa shahidi katika mashambulio ya anga ya utawala wa Kizayuni wa Israel katikati na kusini mwa Ukanda wa Gaza.
-
Amnesty International: Ubaguzi wa apartheid wa Israel dhidi ya Wapalestina hauwezi kukanushwa
Apr 28, 2024 00:57Katibu Mkuu wa Shirika la Msamaha Duniani la Amnesty International amesema kuwa, utawala wa Israel umetekeleza ubaguzi wa apartheid dhidi ya Wapalestina. Agnes Callamard amesema kuwa, ameshangazwa mno na utumiaji mabavu wa kimfumo wa utawala ghasibu wa Israel.
-
UN yaunga mkono maandamano ya wanafunzi wa vyuo vikuu Marekani ya kuwatetea watu wa Gaza
Apr 28, 2024 00:56Stephen Dujaric Msemaji wa Umoja wa Mataifa jana Ijumaa alisema katika radiamali yake kwa maandamano yanayoendelea kufanywa na wanafunzi wa vyuo vikuu huko Marekani katika kuwaunga mkono watu wa Gaza na kupinga mauaji ya kimbari dhidi ya wakazi wa eneo hilo kwamba: Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ni mfuasi na mungaji mkono mkubwa wa uhuru wa kujieleza, ikiwa ni pamoja na huko Marekani; na anaunga mkono haki ya wananchi ya kufanya maandamano kwa amani.
-
Yemen yashambulia Meli za Uingereza katika Bahari Nyekundu
Apr 27, 2024 04:50Shirika la Operesheni za Baharini la Uingereza (UKMTO) lilitangaza jana Ijumaa, kwamba meli yake karibu na pwani ya Yemen imelengwa na kuharibiwa kwa takribani makombora mawili.
-
Kufuatia jinai za Israel, Gaza inahitaji miaka 14 kutegua mabomu na kuwa salama
Apr 27, 2024 04:34Kwa muda wa karibu miezi saba sasa, utawala katili wa Israel umekuwa ukidondosha mabomu kila siku katika Ukanda wa Gaza na sasa Umoja wa Mataifa unasema zoezi la kutegua mabomu ambayo hayajalipuka eneo hilo linaweza kuchukua muda miaka 14.
-
Mbali na walionyofolewa viungo, Wapalestina wengine walizikwa wakiwa hai kwenye makaburi ya halaiki Ghaza
Apr 26, 2024 23:17Wahudumu wa afya, timu za uokoaji na mashirika ya kutetea haki za binadamu yanawashutumu askari vamizi wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kuwanyofoa viungo Wapalestina na hata kuwazika baadhi yao wakiwa hai kwenye makaburi ya halaiki yaliyogunguliwa kwenye eneo la karibu na Hospitali ya Nasser huko Ukanda wa Ghaza, baada ya askari hao katili kuondoka katika eneo hilo Aprili 7 kufuatia mashambulizi ya ardhini ya miezi minne.