-
Palestina: Safari za Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani katika eneo hazina tija yoyote
Mar 21, 2024 10:37Wizara ya Mambo ya Nje ya Palestina imesema diplomasia inayofanywa na Waziri wa Mambo ya Nje ya Marekani Anthony Blinken katika Mashariki ya Kati (Asia Magharibi) bado haijatoa "matokeo yoyote ya kuonekana" kwa ajili ya Ghaza.
-
Utafiti: Aghalabu ya Wasaudia wanapinga uhusiano wa Waarabu na Israel
Mar 21, 2024 07:34Uchunguzi mpya wa maoni unaonyesha kuwa, akthari ya wananchi wa Saudi Arabia si tu wanapinga nchi yao kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel, bali pia wanataka nchi zote za Kiarabu zivunje mahusiano yao na utawala wa Kizayuni.
-
Kan TV: Askari 17 wa Israel wameuawa katika mashambulizi ya Hizbullah
Mar 21, 2024 06:42Vyombo vya habari vya Kizayuni vimetangaza kuwa, wanajeshi 17 wa utawala wa haramu wa Israel wameangamizwa katika mashambulizi ya Harakati ya Hizbullah ya Lebanon.
-
Wahudumu zaidi ya 100 wa kugawa chakula wameuwa Gaza
Mar 21, 2024 04:45Idara ya Habari ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina katika Ukanda wa Gaza imetangaza kuwa zaidi ya wasambazaji 100 wa chakula katika Ukanda wa Gaza wameuawa shahidi katika mashambulizi ya utawala ghasibu wa Israel.
-
Muqawama wa Iraq washambulia uwanja wa ndege Tel Aviv
Mar 20, 2024 23:23Kwa mara nyingine tena wanamuqawama wa Iraq wameshambulia Uwanja wa Ndege wa Ben Gurion katika mji mkuu wa utawala haramu wa Israel, Tel Aviv.
-
Israel: Tumeua watu 90 katika Hospitali ya al-Shifa
Mar 20, 2024 22:41Jeshi la utawala haramu wa Israel limekiri na kutangaza wazi kuwa askari wake wameua Wapalestina 90 katika uvamizi na hujuma ya siku mbili katika Hospitali ya al-Shifa huko katika Ukanda wa Gaza.
-
Mshauri wa zamani wa White House ametaka Wapalestina wahamishwe Ghaza na kupelekwa jangwani
Mar 20, 2024 08:03Mshauri wa zamani wa Ikulu ya Marekani (White House) Jared Kushner amesema, utawala wa Kizayuni wa Israel inapasa uwaondoe Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza na kuwahamishia kwenye jangwa la Negev kusini mwa ardhi zilizopachikwa jina bandia la Israel.
-
Qatar: Tuna matumaini ya kupatikana usitishaji vita Ukanda wa Ghaza
Mar 19, 2024 23:28Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar amesema kuwa, kumeshuhudiwa maendeleo mazuri kwenye mazungumzo ya kusimamisha vita na ana matumaini mazungumzo hayo yatazaa matunda mazuri.
-
Yemen: Oparesheni dhidi ya meli za Israel zitaendelea
Mar 19, 2024 08:17Wizara ya Mambo ya Nje ya serikali ya uokovu wa kitaifa ya Yemen imesisitiza leo katika radiamali yake kwa taarifa ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu oparesheni za kijeshi za vikosi vya ulinzi vya nchi hiyo katika Bahari Nyekundu kuwa oparesheni hizo zitaendelea dhidi ya utawala wa Kizayuni hadi hapo utawala huo utakapositisha jinai zake katika Ukanda wa Gaza.
-
Thomas Friedman: Netanyahu ndiye kiongozi mbaya zaidi katika historia ya Kiyahudi
Mar 19, 2024 04:26Mwandishi na mwanahabari wa Marekani, Thomas Friedman, amesema kuwa Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ataingia katika historia kama kiongozi mbaya zaidi katika historia ya Kiyahudi.