-
Mashirika ya haki Palestina yaonya kuhusu 'Nakba ya Pili' Gaza
Dec 05, 2023 03:22Mashirika matatu ya kutetea haki za binadamu ya Palestina yameashiria hatua ya Israel ya kuwafukuza kwa umati Wapalestina katika Ukanda wa Gaza na kutahadharisha kuwa, utawala huo wa Kizayuni unapanga kukariri Nakba ya pili katika eneo hilo lililozingirwa.
-
Vifaru na askari jeshi wa Kizayuni wawindwa na wapiganaji shujaa wa Kipalestina
Dec 05, 2023 01:51Katika muda wa saa 24 zilizopita, wapiganaji wa muqawama wa Palestina wameharibu magari 28 ya kijeshi ya utawala wa Kizayuni vikiwemo vifaru, magari ya kivita na ya kubeba wanajeshi.
-
Vyombo vya habari vya Marekani vyafichua jinamizi la mashambulizi ya Hizbullah kwa Israel
Dec 04, 2023 08:40Televisheni ya Bloomberg ya Marekani imefichua kuwa, mashambulio ya Hizbullah ya Lebanon huko kaskazini mwa ardhi za Palestina zilizopachikwa jina bandia la Israel, yamekuwa jinamizi kwa walowezi wa Kizayuni wanaoishi kwenye maeneo hayo.
-
Balaa la mashambulizi ya Yemen kwa bandari ya Eilat, utawala wa Kizayuni wafikiria kuifunga
Dec 04, 2023 08:38Mashambulizi ya wanamapambano wa Yemen dhidi ya maeneo ya utawala wa Kizayuni ikiwa ni sehemu ya kuwasaidia ndugu zao wa Ghaza, yameisababishia hasara bandari muhimu ya Eilat ya utawala wa Kizayuni kiasi kwamba hivi sasa bandari hiyo imekaribia kufungwa.
-
Piga nikupige baada ya usitisjai vita wa muda katika Ukanda wa Ghaza
Dec 04, 2023 03:57Hatua ya utawala wa Kizayuni wa Israel ya kushambulia kinyama kambi ya wakimbizi ya Jabalia katika Ukanda wa Ghaza kwa kutumia mabomu ya fosforasi na sambamba na kutumwa mabomu mapya kutoka Marekani kwa utawala huo ghasibu ni miongoni mwa matukio ya hivi karibuni kuhusiana na Palestina.
-
Utawala wa Kizayuni wakiri kupata pigo la kihistoria katika saa 24 zilizopita
Dec 04, 2023 02:49Vyanzo vya Kizayuni, baada ya kipindi kirefu cha kudhibiti na kuficha habari kuhusiana na vifo na majeruhi wake vitani, hatimaye vimekiri kuuawa askari jeshi wake 75 katika saa 24 zilizopita.
-
Kuanza tena kesi ya Netanyahu kuhusu tuhuma za ufisadi.
Dec 04, 2023 02:40Vyombo vya habari vya Kizayuni vimeripoti kuwa kikao cha kufuatilia kesi ya Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala huo kitafanyika leo Jumatatu.
-
Walenga shaba wa Muqawama wanawasubiri wanajeshi wa Israeli
Dec 03, 2023 07:42Utawala wa Kizayuni ulianzisha tena mashambulizi yake katika maeneo mengi ya Ukanda wa Ghaza mara tu baada ya kumalizika usitishaji vita siku ya Alkhamisi, ambapo vikosi vya nchi kavu vya jeshi la Israel vinajiandaa kuingia katika maeneo mengine ya kaskazini mwa Ukanda wa Gaza.
-
Askari 60 wa Kizayuni waangamizwa katika operesheni ya HAMAS
Dec 03, 2023 07:13Makumi ya wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wameangamizwa katika operesheni ya Brigedi za Izzuddin al Qassam, Tawi la Kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu HAMAS.
-
Mufti wa Yemen: Kimbunga cha al-Aqsa, kipigo cha karne dhidi ya Uzayuni
Dec 03, 2023 07:11Mufti Mkuu wa Yemen amesema Operesheni ya Kimbunga cha al-Aqsa imedhihirisha msimamo thabiti na uwezo mkubwa wa mrengo wa muqawama wa Palestina, na kwamba operesheni hiyo kilikuwa kipigo cha karne dhidi ya utawala wa Kizayuni.