-
Yemen yaonya Saudi Arabia kuhusu ‘matokeo mabaya’ iwapo uchokozi na kuzingirwa vitaendelea
Jul 21, 2026 11:28Wizara ya Mambo ya Nje ya Yemen imeonya utawala wa Saudi Arabia kuhusu “matokeo mabaya na makubwa” iwapo utaendelea kuongeza mashambulizi yake kwa kulenga miundombinu ya kiraia, na kuimarisha sera ya kuzingira bandari na viwanja vya ndege nchini Yemen.
-
Israel yafanya uharibifu mkubwa kusini mwa Lebanon huku ndege zisizo na rubani zikiruka katika anga ya Beirut
Jul 21, 2026 03:09Jeshi la Israel jana lilifanya operesheni kubwa ya ubomoaji kusini mwa Lebanon siku ya Jumatatu huku ndege zisizo na rubani za utawala huo ghasibu zikiruka katika anga ya mji mkuu wa chi hiyo Beirut na vitongoji vyake.
-
Ansarullah: Mzingiro wa baharini dhidi ya Saudia ni matokeo ya kukataa Riyadh kutoa jibu kwa matakwa halali ya Yemen
Jul 21, 2026 02:58Mohammed Abdulsalam, Mkuu wa timu ya mazungumzo ya Yemen, amesisitiza kuwa tangazo la vikosi vya ulinzi vya Yemen kuhusu marufuku ya usafiri wa baharini dhidi ya Saudi Arabia ilikuwa hatua ambayo Sana'a ililazimika kuichukua kujibu hatua ya Riyadh kukataa kujibu kwa njia ya amani matakwa halali ya Yemen.
-
Ndege za Marekani za kuongeza mafuta angani zahamishiwa Israel kwa hofu ya mashambulizi ya Iran
Jul 20, 2026 10:59Ndege za Marekani za kuongeza mafuta angani (refuelling aircraft) zimehamishiwa katika eneo la Palestina inayokaliwa, kutokana na hofu ya mashambulizi yanayoweza kufanywa na Iran.
-
Walowezi wa Kizayuni wachoma moto nyumba mbili na msikiti wa Wapalestina
Jul 20, 2026 10:33Walowezi wa Kizayuni wamechoma moto nyumba mbili pamoja na msikiti mmoja wa Wapalestina, katika tukio lililotajwa kuwa sehemu ya mashambulizi dhidi ya mali za Wapalestina.
-
Askari mwingine wa Marekani auawa nchini Iraq huku idadi ya majeruhi ikipanda katika vita na Iran
Jul 20, 2026 04:10Jeshi la Marekani limekiri Jumapili kwamba askari wake mwingine ameuawa kufuatia shambulio la ndege isiyo na rubani ya Iran, huku operesheni za kulipiza kisasi za Jamhuri ya Kiislamu zikiendelea kuwasababishia hasara kubwa askari wa jeshi katili Marekani katika kanda nzima.
-
Wanazuoni wa Bahrain waonya kuhusu ukiukwaji wa haki za binadamu
Jul 20, 2026 04:09Wanazuoni wa Bahrain wametoa onyo kuhusu kuendelea ukiukwaji wa haki za binadamu nchini humo, wakisema hali hiyo inazidi kuzorota na kuhatarisha haki za msingi za wananchi.
-
Waziri wa zamani wa Vita wa Israel: Tulishindwa kufikia malengo katika vita dhidi ya Iran
Jul 20, 2026 04:06Moshe Ya'alon, Waziri wa zamani wa vita wa utawala wa Israel, amekiri kuwa mashambulizi yaliyoelekezwa dhidi ya Iran hayakufanikiwa kufikia malengo yaliyokuwa yamekusudiwa.
-
Ansarullah ya Yemen: Saudi Arabia inahudumia miradi ya Wamarekani-Wazayuni
Jul 19, 2026 03:24Mjumbe wa ngazi za juu wa harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema kwamba Saudi Arabia imeweka uwezo na suhula zake za kisiasa, kifedha na kijeshi katika huduma ya miradi ya Marekani eneo la Asia Magharibi na inafanya kazi ya kudhoofisha mataifa ambayo yana misimamo dhidi ya Israel.
-
Israel yafanya mauaji makubwa huko Nuseirat, janga la binadamu linazidi kuwa baya Gaza
Jul 18, 2026 10:59Wapalestina 14 wameuawa na wengine 37 kujeruhiwa, wengi wao wakiwa katika kambi ya Nuseirat katikati mwa Ukanda wa Gaza, kutokana na mashambulizi mtawalia ya Israel yaliyolenga maeneo mbalimbali ya ukanda huo, huku hali ya kibinadamu ikizidi kuwa mbaya.