-
Intelijinsia ya Israel: Jeshi la Marekani linaweza kumudu mashambulizi dhidi ya Iran kwa siku kadhaa tu
Feb 25, 2026 05:35Maafisa wa ujasusi wa Israel wanakadiria kuwa Marekani inaweza kuendeleza mashambulio ya kijeshi kwa "siku nne hadi tano" pekee dhidi ya Iran ikiwa itaanzisha mashambulizi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu. Hii ni kwa mujibu wa ripoti mpya.
-
Afisa mwandamizi wa PLO asema, HAMAS si kundi la kigaidi, apinga mpango wa kuipokonya silaha
Feb 25, 2026 03:28Katibu Mkuu wa Kamati ya Utendaji ya Chama cha Ukombozi wa Palestina (PLO), Azzam al-Ahmad amesema, Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS si shirika la kigaidi na ameukataa wito wa kupokonywa silaha zake huku akibainisha kuwepo mipango ya kufanya mazungumzo kuhusu uwezekano wa harakati hiyo kujumuishwa katika PLO.
-
Ripoti: Israel iliwamiminia risasi, kuwaua wafanyakazi wa misaada Tel al Sultan, Gaza
Feb 24, 2026 22:56Karibu risasi elfu moja zilifyatuliwa na wanajeshi wa Israel katika mauaji ya kiholela dhidi ya wafanyakazi wa misaada huko Tel al-Sultan, Gaza, huku baadhi yao wakiuawa kwa kupigwa risasi kwa karibu, kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa hivi karibuni.
-
Iraq yamueleza mjumbe wa Marekani: Uundaji wa serikali ni 'suala letu la ndani'
Feb 24, 2026 08:22Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq, Fuad Hussein amesema, uundaji wa serikali mpya ya nchi hiyo ni "suala la ndani," ukiwa ni mjibizo uliotolewa wiki chache baada ya Marekani kutishia kufuta msaada na uungaji mkono wake kwa nchi hiyo ya Asia Magharibi.
-
Israel imepeleka Ghaza maboksi yenye mafuvu na miili iliyonyofolewa ya wanawake Wapalestina
Feb 24, 2026 07:45Mbunge wa kujitegemea, ambaye pia ni kiongozi wa zamani wa chama cha Leba nchini Uingereza Jeremy Corbyn, ametoa simulizi za kutisha zilizotokana na maelezo ya mkurugenzi wa Hospitali ya Al-Shifa katika Ukanda wa Ghaza uliozingirwa, zinazobainisha kwa undani jinsi utawala wa kizayuni wa Israel ulivyopeleka katika eneo hilo masanduku kadhaa yenye mafuvu ya vichwa na mabaki ya Wapalestina yaliyokatwakatwa.
-
Netanyahu kuunda 'muungano' utakaoshirikisha Waarabu kukabiliana na mihimili ya Sunni na Shia
Feb 24, 2026 07:42Waziri mkuu wa utawala wa kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu amesema juhudi zinaendelea kufanywa za kuunda kile alichokielezea kama "muungano" wa kikanda wa kukabiliana na kile alichokiita "mihimili ya Sunni na Shia".
-
Wapalestina wanakoseshwa kufunga na kufungua Saumu kwa wakati kwenye jela za Israel
Feb 24, 2026 00:36Tume moja ya Palestina inayoshughulikia masuala ya Wapalestina wanaoshikiliwa kwenye jela za utawala wa kizayuni wa Israel imezishutumu mamlaka za jela hizo kwa kuwafanya Wapalestina hao washindwe kufunga Saumu zao "kwa wakati sahihi" katika mfungo huu wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
Mkutano wa dharura wa mawaziri wa mambo ya nje wa OIC kujadili unyakuzi wa Israel wa ardhi za Palestina
Feb 23, 2026 03:39Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) itafanya mkutano wa dharura katika ngazi ya mawaziri wa mambo ya nje Alhamisi ijayo kujadili maamuzi ya hivi karibuni ya Israel yanayozidisha ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni na unyakuzi wa ardhi za Palestina katika Ukingo wa Magharibi.
-
Ansarullah yalaani mauaji ya umati ya umwagaji damu ya Israel mashariki mwa Lebanon
Feb 23, 2026 00:09Harakati ya Ansarullah ya Yemen imelaani vikali "mauaji ya umati ya umwagaji damu" yaliyofanywa na utawala wa Israel katika eneo la Beqaa mashariki mwa Lebanon, na kuuwa takriban watu kumi na kujeruhi wengine wengi.
-
Kiongozi wa Ansarullah: Marekani ni mshirika wa adui Mzayuni katika jinai zake zote
Feb 23, 2026 00:08Kiongozi wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen, ameashiria kile kinachojulikana kama "Bodi ya Amani ya Trump" kwa ajili ya Gaza, na kusema: "Marekani ni mshirika wa adui Mzayuni katika jinai zake zote."