-
Hamas: Takwa la kukabidhi silaha ni kisingizio cha Israel cha kukwepa wajibu
May 03, 2026 10:15Mjumbe wa Idara ya Siasa ya Hamas, Mohammed Nazzal, amesema kuwa ombi la kukabidhiwa silaha za harakati hiyo ni kisingizio kinachotumiwa na utawala wa Kizayuni wa Israel ili kukwepa utekelezaji wa majukumu yake.
-
Manowari kubwa na ya kisasa zaidi ya Marekani yaondoka kwa fedheha katika vita dhidi ya Iran
May 02, 2026 11:31USS Gerald R. Ford, meli kubwa zaidi ya kivita na ya gharama ya juu kuwahi kuundwa na Marekani, imelazimika kujiondoa kutoka ukanda wa Asia Magharibi baada ya siku 309 za operesheni endelevu baharini, ikiwa katika jukumu la kuunga mkono vita dhidi ya Iran.
-
Viongozi wa Kikristo wamlaani Muisraeli aliyemshambulia mtawa wa kike katika mji wa al-Quds
May 02, 2026 11:24Malalamiko yameendelea kumiminika baada ya Muisraeli mwenye misimamo mikali kumshambulia mtawa wa kike raia wa Kifaransa, huku Waisraeli Wazayuni wakishadidisha mashambulizi dhidi ya Waislamu na Wakristo pamoja na maeneo matakatifu katika ardhi za Palestina zinazokoloniwa na utawala wa Israel.
-
Mwakilishi wa Palestina akataa ombi la rais wa FIFA la kupiga picha na Muisraeli
May 02, 2026 09:43Mkuu wa Shirikisho la Soka la Palestina amekataa ombi la rais wa FIFA, Gianni Infantino la kupiga picha na mwakilishi wa utawala haramu wa Israel.
-
Israel yapewa kichapo Lebanon, wanajeshi wasiopungua 2 wauawa
May 02, 2026 07:19Wanajeshi wasiopungua wawili wa Israel wameuawa na wengine zaidi ya 27 kujeruhiwa katika mashambulizi kadhaa ya ndege zisizo na rubani za harakati ya Hizbullah kusini mwa Lebanon, huku Israel ikiitonya Washington kwamba uwezo wake wa kukabiliana na harakati ya mapambano ya Lebanon unakaribia kusambaratika.
-
Vyombo vya habari vya Kizayuni: Jina la Netanyahu ni "Shetani" kwa wengi duniani
Apr 30, 2026 10:14Chombo cha habari cha Kizayuni kimechambua kuporomoka kwa nafasi ya utawala wa Israel duniani na kubadilika fikra za umma kuhusu utawala huo.
-
Afisa wa Hizbullah: Mapambano yataendelea hadi ukombozi kamili wa ardhi ya Lebanon
Apr 30, 2026 07:42Makamu wa Mwenyekiti wa Baraza la Kisiasa la harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesisitiza msimamo wa msingi wa harakati hiyo kuhusu uvamizi wa utawala wa Kizayuni wa Israel na kusema kuwa Muqawama na mapambano yataendelea hadi ardhi yote ya nchi hiyo itakapokombolewa kikamilifu.
-
Yemen yamtahadharisha Trump/ Sana'a : Tunaunga mkono hatua za Iran katika Mlango Bahari wa Hormuz
Apr 29, 2026 10:00Wizara ya Mambo ya Nje ya Yemen imetahadharisha kuhusu hatua zozote za uchokozi na ukatili za serikali ya Trump katika Ghuba ya Uajemi na kutangaza kuwa Sana'a inaunga mkono hatua za Iran katika Mlango wa Bahari wa Hormuz.
-
Kamanda wa Kikosi cha Quds cha IRGC asisistiza kuhusu uungaji mkono imara kwa Hizbullah
Apr 28, 2026 09:17Kamanda mkuu wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amekanusha vikali propaganda za Israel zinazolenga kupunguza nguvu za harakati ya Hizbullah, huku akisisitiza uungaji mkono kamili wa mhimili wa muqawama kwa harakati hiyo.
-
Rais wa Iraq amteua al-Zaidi kuwa Waziri Mkuu
Apr 28, 2026 09:15Rais wa Iraq, Nizar Amedi, ambaye amechaguliwa hivi karibuni, ametangaza rasmi kumteua Ali al Zaidi kuwa waziri mkuu mteule wa nchi hiyo na kumpa jukumu la kuunda serikali ijayo.