-
Waziri Mkuu wa Qatar: Benjamin Netanyahu anapasa 'kufikishwa mbele ya sheria'
Sep 11, 2025 07:34Waziri Mkuu wa Qatar Mohammed bin Abdulrahman bin Jassim Al-Thani amelaani mashambulizi ya juzi ya Israel dhidi ya Doha na kuyataja kuwa ni "ugaidi wa kiserikali,". Amesema kuwa Waziri Mkuu wa utawala wa Israel Benjamin Netanyahu anapasa "kufikishwa mbele ya sheria."
-
UNRWA: Zaidi ya wakimbizi laki moja wa Gaza hawajapokea msaada wowote tangu miezi 6 iliyopita
Sep 11, 2025 07:34Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) limetangaza kuwa, zaidi ya watu laki moja wanaendelea kutaabika na njaa katika maeneo ya kuwahifadhi wakimbizi ya shirika hilo huko Gaza, na hakuna msaada wa kibinadamu ambao umeruhusiwa kuingia katika eneo hilo kwa zaidi ya miezi 6 sasa.
-
Baada ya kuzuia mashambulizi mengi ya Israel; Yemen yatoa onyo kali kwa Tel Aviv, yasema Wazayuni wajiandae
Sep 11, 2025 03:51Yemen imetoa onyo kali kwa utawala wa Kizayuni kuhusu uwezekano wa Sana’a kulipiza kisasi vikali dhidi ya mashambulizi ya kinyama ya Tel Aviv huko Yemen.
-
Wakati ulimwengu ukiendelea kulaani shambulio la Israel, Qatar yasema ina haki ya kujibu
Sep 11, 2025 00:41Sambamba na kauli mbalimbali uulimwenguni za kulaani shambulio la Israel, Qatar imetangaza kuwa, ina haki ya kujibu jinai hiyo ya Israel huko Doha iliyowalenga viongozi waandamizi wa HAMAS.
-
Rais wa Croatia akataa kukutana na Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Israel
Sep 10, 2025 23:46Rais wa Croatia Zoran Milanovic amekataa kukutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel Gideon Saar wakati wa ziara yake rasmi huko Zagreb siku ya Jumanne, akitaja mauaji ya Israel huko Gaza kama sababu ya kukataa kukutana na mwanadiplomasia huyo wa Israel.
-
Kwa nini maelfu ya Wazayuni wanataka kusimamishwa vita vya Gaza?
Sep 10, 2025 10:07Maelfu ya Wazayuni wamefanya maandamano ya kumpinga Benjamin Netanyahu Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni na kutaka kusitishwa mara moja vita vya Ukanda wa Gaza na kukombolewa mateka wa Kizayuni.
-
Rais wa Iran: Nchi za Kiislamu zilaani kwa kauli na vitendo uhalifu wa Utawala wa Kizayuni
Sep 10, 2025 07:29Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Dkt. Masoud Pezeshkian, amesema kwa masikitiko kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel hauheshimu misingi yoyote ya sheria za kimataifa na ameongeza kuwa mwenendo huo unafanyika kwa msaada na uungaji mkono wa Marekani.
-
Somalia, Muqawama walaani shambulio dhidi ya Hamas nchini Qatar
Sep 10, 2025 03:34Somalia imelaani shambulio la Israel katika mji mkuu wa Qatar, Doha ambalo liliwalenga viongozi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas, ikisema kuwa hujuma hiyo ni "ukiukwaji mkubwa wa sheria za kimataifa" na tishio kwa amani na usalama wa kikanda na kimataifa.
-
UNICEF: Ulimwengu hauchukui hatua za kweli kuokoa Gaza
Sep 09, 2025 23:24Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) umetangaza kuwa, ulimwengu hauchukui hatua za kweli kuokoa Gaza.
-
Israel yafanya shambulio la kigaidi Qatar na kulenga ujumbe wa Hamas
Sep 09, 2025 10:27Shambulio la kigaidi lililotekelezwa na utawala ghasibu wa Israel huko Doha mji mkuu wa Qatar limelenga maeneo ya makazi yanayohusishwa na wajumbe wa ngazi ya juu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS.