-
Mossad na Shabak zapinga mpango wa kuikalia kwa mabavu Gaza
Aug 09, 2025 11:49Wakuu wa Shirika la Ujasusi la Israel (MOSSAD) na Idara ya Ujasusi wa Ndani Shin Bet (SHABAK) zimepinga mpango wa kuukalia kwa mabavu mji wa Gaza kutokana na taathira zake mbaya.
-
OIC yaonya: Mpango wa Israel wa kuikalia kwa mabavu Gaza ni "jinai za kivita"
Aug 09, 2025 07:00Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imelaani vikali uamuzi wa Israel wa kukalia kwa mabavu Ukanda wa Gaza na kuwaondoa kwa nguvu karibu Wapalestina milioni moja kutoka Gaza City na maeneo ya kaskazini mwa kusini, na kuuita mpango huo kuwa ni "jinai dhidi ya ubinadamu."
-
UEFA yamuenzi 'Pele wa Palestina' aliyeuliwa na jeshi la Israel Ghaza wakati anangojea chakula
Aug 09, 2025 04:11Muungano wa Vyama vya Soka vya Ulaya UEFA, umemuenzi nahodha na nyota wa zamani wa timu ya taifa ya Palestina Suleiman al-Obeid, ambaye aliuawa shahidi katika shambulizi la kinyama la utawala wa kizayuni wa Israel alipokuwa akisubiri msaada wa chakula huko Ghaza siku ya Jumatano.
-
Mbunge wa Hizbullah: Kukubali tupokonywe silaha ni sawa na kujinyonga
Aug 09, 2025 03:52Mbunge wa Lebanon kutoka mrengo wa kisiasa wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya nchi hiyo Hizbullah amelipinga vikali dai la kuitaka harakati hiyo iweke chini silaha zake kufuatia shinikizo la Marekani kwa serikali la kuitaka iipokonye silaha harakati hiyo.
-
Israel yasaini makubaliano ya kihistoria ya kuiuzia Misri gesi yenye thamani ya dola bilioni 35
Aug 09, 2025 03:27Utawala wa kizayuni wa Israel umetangaza kusainiwa mkataba mkubwa utakaogharimu dola bilioni 35 wa kuiuzia Misri gesi asilia, unaotajwa kuwa ni "mkubwa zaidi katika historia ya Israel". Hayo yameelezwa na Eli Cohen, waziri wa nishati wa utawala huo ghasibu.
-
Umoja wa Mataifa: Mpango wa kuikalia kwa mabavu Gaza usitishwe mara moja
Aug 08, 2025 23:02Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, mpango wa Israel wa kuikalia kwa mabavu Gaza unapaswa kusitishwa mara moja.
-
Netanyahu na genge lake wapitisha mpango wa kuikalia Ghaza City, Hamas yatoa mjibizo mkali
Aug 08, 2025 07:55Liitwalo 'baraza la mawaziri la kisiasa na kiusalama' la utawala haramu wa kizayuni wa Israel limeidhinisha mpango wa waziri mkuu wa utawala huo ghasibu Benjamin Netanyahu wa kulikalia kwa mabavu eneo lote la Ukanda wa Ghaza kwa kuwahamisha kwanza kwa nguvu makumi ya maelfu ya Wapalestina wa Ghaza City.
-
Trump atumia lugha ya uamrishaji kuzitaka nchi za Asia Magharibi zianzishe uhusiano na Israel
Aug 08, 2025 07:12Rais Donald Trump wa Marekani amezitaka nchi za Asia Magharibi zianzishe uhusiano rasmi wa kidiplomasia na utawala wa kizayuni wa Israel.
-
Hamas yamjibu Netanyahu: Gaza itasalia kuwa mwiba kwa utawala vamizi
Aug 08, 2025 04:19Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesema kuwa matamshi ya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, kuhusu kukaliwa kwa mabavu Ukanda wa Gaza ni kubatilisha waziwazi mwenendo wa mazungumzo, na yanafichua nia ya kweli ya kujiondoa kwake katika duru ya mwisho ya mazungumzo, licha ya kukaribia makubaliano ya mwisho.
-
Idadi ya Wapalestina walioaga dunia kutokana na njaa Ukanda wa Gaza imeongezeka hadi 197
Aug 07, 2025 22:52Wizara ya Afya ya Palestina katika Ukanda wa Gaza imetangaza kuwa Wapalestina wengine wanne wameaga dunia kutokana na njaa iliyosababishwa na kukosa chakula, na hivyo kuifanya idadi ya wahanga walipoteza maisha kutokana na njaa katika Ukanda wa Gaza kuongezeka na kufikia 197.