-
Albanese: Magharibi haiwi na uwezo wowote wa kutekeleza sheria za kimataifa inapohusu Israel
Aug 03, 2025 02:11Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa wa hali ya haki za binadamu katika maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu amesema, nchi za Magharibi haziwi na uwezo wowote wa kutekeleza sheria za kimataifa inapohusu utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Umoja wa Mataifa unaunga mkono kuanzishwa kwa taifa la Palestina
Aug 02, 2025 23:02Msemaji wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, kwa mtazamo wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, kiwango cha uungwaji mkono mpana kutoka kwa mataifa ya dunia katika suluhu ya mataifa mawili na kuanzishwa kwa taifa huru la Palestina ni muhimu.
-
Sweden: Ukraine lazima iseme 'ndiyo' kwa ndoa za jinsia moja kama sharti la kujiunga na EU
Aug 02, 2025 08:18Waziri Mkuu wa Sweden Ulf Kristersson amesema, Ukraine inapaswa kutoa ulinzi kamili wa kisheria kwa 'mashoga', ikiwa ni pamoja na wa ndoa za jinsia moja, kama sehemu ya juhudi zake za kupigania kuwa mwanachama wa Umoja wa Ulaya,
-
Viongozi wa chama cha Democratic wanamtaka Trump kukomesha vita dhidi ya Gaza
Aug 02, 2025 03:35Viongozi wa chama cha Democratic katika Baraza la Wawakilishi la Marekani wametoa wito kwa Rais Donald Trump wakimtaka akomeshe vita vya Israel dhidi ya watu wa Gaza kwa kufanya kazi haraka na pande zote ili kuanza tena mazungumzo.
-
Je, matakwa ya wabunge wa Ulaya ya kuwawekea vikwazo maafisa wa Israel yatatekelezwa?
Aug 01, 2025 23:11Wabunge 40 wa Ulaya wametoa wito wa kuwekewa vikwazo maafisa wa serikali ya Israel.
-
Ureno pia kulitambua taifa la Palestina
Aug 01, 2025 23:11Serikali ya Ureno pia imetangaza uamuzi wake wa kuitambua Palestina wakati wa mkutano wa kilele wa Umoja wa Mataifa mwezi ujao wa Septemba.
-
Baada ya Canada kutangaza kuitambua Palestina sasa yakabiliwa na ushuru mkali wa Marekani
Aug 01, 2025 23:09Rais Donald Trump wa Marekani almezidisha vita vya kibiashara na Kanada baada ya nchi hiyo wa kutangaza kuwa tayari kuitambua Palestina, akisema kwamba hatutatia saini makubaliano na nchi inayoiunga mkono Palestina.
-
Russia: Njia ya sasa ya Ujerumani na Ulaya inauelekeza ulimwengu kwenye Vita vya Tatu vya Dunia
Aug 01, 2025 09:58Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema: "Viongozi wa sasa wa Ujerumani na nchi nyingine za Ulaya wanageuka kuwa Reich ya Nne, na njia yao ya sasa itauelekeza ulimwengu katika vita vikuu vya tatu."
-
Mamia ya watu mashuhuri Ujerumani watoa wito wa kusitishwa uuzaji wa silaha kwa Israel
Aug 01, 2025 09:57Gazeti la Ujerumani la Der Spiegel limeandika kuwa, zaidi ya shakhsia 200 mashuhuri wa vyombo vya habari, utamaduni na sanaa wameitaka serikali ya Ujerumani kusitisha uuzaji wa silaha kwa utawala wa Israel.
-
UNRWA: Hali mbaya ya kibinadamu ya Ghaza haiwezi kutatuka bila ya kusimamishwa vita
Aug 01, 2025 03:47Mshauri wa vyombo vya habari wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina UNRWA amesisitiza kuwa, haiwezekani kutatua hali mbaya ya kibinadamu katika Ukanda wa Ghaza bila ya kusitishwa mapigano.